Kilniojo Korano reikšmių vertimas - Suahilių k. vertimas - Abdullah Muchammed ir Naser Khamis * - Vertimų turinys


Reikšmių vertimas Aja (Korano eilutė): (41) Sūra: Sūra Al-Ma’idah’
۞ يَٰٓأَيُّهَا ٱلرَّسُولُ لَا يَحۡزُنكَ ٱلَّذِينَ يُسَٰرِعُونَ فِي ٱلۡكُفۡرِ مِنَ ٱلَّذِينَ قَالُوٓاْ ءَامَنَّا بِأَفۡوَٰهِهِمۡ وَلَمۡ تُؤۡمِن قُلُوبُهُمۡۛ وَمِنَ ٱلَّذِينَ هَادُواْۛ سَمَّٰعُونَ لِلۡكَذِبِ سَمَّٰعُونَ لِقَوۡمٍ ءَاخَرِينَ لَمۡ يَأۡتُوكَۖ يُحَرِّفُونَ ٱلۡكَلِمَ مِنۢ بَعۡدِ مَوَاضِعِهِۦۖ يَقُولُونَ إِنۡ أُوتِيتُمۡ هَٰذَا فَخُذُوهُ وَإِن لَّمۡ تُؤۡتَوۡهُ فَٱحۡذَرُواْۚ وَمَن يُرِدِ ٱللَّهُ فِتۡنَتَهُۥ فَلَن تَمۡلِكَ لَهُۥ مِنَ ٱللَّهِ شَيۡـًٔاۚ أُوْلَٰٓئِكَ ٱلَّذِينَ لَمۡ يُرِدِ ٱللَّهُ أَن يُطَهِّرَ قُلُوبَهُمۡۚ لَهُمۡ فِي ٱلدُّنۡيَا خِزۡيٞۖ وَلَهُمۡ فِي ٱلۡأٓخِرَةِ عَذَابٌ عَظِيمٞ
Ewe Mtume! Wasikuhuzunishe wale ambao wanakimbilia kuukanusha unabii wako miongoni mwa wanafiki ambao wameonyesha Uislamu na huku nyoyo zao ni tupu, kwani mimi ni Mwenye kukuokoa na wao. Na lisikuhuzunishe lile la kukimbilia kwa Mayahudi kuukanusha unabii wako, kwani wao ni watu wanaosikiliza urongo, wanayakubali yanayozuliwa na wanavyuoni wao na wanawasikiliza watu wengine wasiohudhuria kwenye baraza yako; na wengine hawa wanayageuza maneno ya Mwenyezi Mungu baada ya kuyaelewa na wanasema, «Yakiwajia kutoka kwa Muhammad yanayolingana na yale tuliyoyageuza na tukayapotosha katika hukumu za Taurati, basi yatumieni. Na yakiwajia kutoka kwake yanayokwenda kinyume na hayo, basi jihadharini kuyakubali na kuyatumia.» Na ambaye Mwenyezi Mungu Ataka apotee, basi hutaweza, ewe Mtume, kulizuia hilo lisiwe kwake na wala huwezi kumuongoza.. Na hakika hawa wanafiki na Mayahudi, Mwenyezi Mungu Hakutaka kuzitakasa nyoyo zao na uchafu wa ukafiri, wana udhalilifu na fedheha hapa duniani, na watapata, huko Akhera, adhabu kubwa.
Tafsyrai arabų kalba:
 
Reikšmių vertimas Aja (Korano eilutė): (41) Sūra: Sūra Al-Ma’idah’
Sūrų turinys Puslapio numeris
 
Kilniojo Korano reikšmių vertimas - Suahilių k. vertimas - Abdullah Muchammed ir Naser Khamis - Vertimų turinys

Kilniojo Korano reikšmių vertimas į suahilių k., išvertė Dr. Abdullah Muchammed Abu Bakr ir šeichas Naser Khamis.

Uždaryti