Check out the new design

Kilniojo Korano reikšmių vertimas - Vertimas į suahilių k. - Ali Muhsin Al-Barvani * - Vertimų turinys

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Reikšmių vertimas Sūra: Az-Zukhruf   Aja (Korano eilutė):
وَلِبُيُوتِهِمۡ أَبۡوَٰبٗا وَسُرُرًا عَلَيۡهَا يَتَّكِـُٔونَ
Na milango ya nyumba zao na vitanda wanavyo egemea juu yake,
Na tungeli wafanyia milango ya nyumba zao na vitanda kuwa ni vya fedha wakineemeka navyo na wakiegemea juu yake. Na tungeli wafanyia mapambo ya kila kitu. Na starehe zote hizo tulizo kusifia si chochote ila ni starehe za kupita njia, ni za uhai huu tu wa duniani. Na malipo ya Akhera mbele ya Muumba wako na Mlezi wako yameandaliwa kwa wanao jilinda na ushirikina, na wakayaepuka maasi ya kuangamiza.
Tafsyrai arabų kalba:
وَزُخۡرُفٗاۚ وَإِن كُلُّ ذَٰلِكَ لَمَّا مَتَٰعُ ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَاۚ وَٱلۡأٓخِرَةُ عِندَ رَبِّكَ لِلۡمُتَّقِينَ
Na mapambo. Lakini hayo si chochote ila ni starehe ya maisha ya dunia tu, na Akhera iliyoko kwa Mola wako Mlezi ni ya wenye kumchamngu.
Na tungeli wafanyia milango ya nyumba zao na vitanda kuwa ni vya fedha wakineemeka navyo na wakiegemea juu yake. Na tungeli wafanyia mapambo ya kila kitu. Na starehe zote hizo tulizo kusifia si chochote ila ni starehe za kupita njia, ni za uhai huu tu wa duniani. Na malipo ya Akhera mbele ya Muumba wako na Mlezi wako yameandaliwa kwa wanao jilinda na ushirikina, na wakayaepuka maasi ya kuangamiza.
Tafsyrai arabų kalba:
وَمَن يَعۡشُ عَن ذِكۡرِ ٱلرَّحۡمَٰنِ نُقَيِّضۡ لَهُۥ شَيۡطَٰنٗا فَهُوَ لَهُۥ قَرِينٞ
Anaye yafanyia upofu maneno ya Rahmani tunamwekea Shet'ani kuwa ndiye rafiki yake.
Na mwenye kujitia upofu na Qur'ani aliyo iteremsha Mwenyezi Mungu Mwingi wa Rehema kuwa ni kumbusho kwa walimwengu wote, tunamsalitisha na Shetani, anakuwa naye daima, akimpoteza na akimzuzua.
Tafsyrai arabų kalba:
وَإِنَّهُمۡ لَيَصُدُّونَهُمۡ عَنِ ٱلسَّبِيلِ وَيَحۡسَبُونَ أَنَّهُم مُّهۡتَدُونَ
Na hakika wao wanawazuilia Njia na wenyewe wanadhani kuwa wameongoka.
Na hakika Mashetani wanao jitia upofu na Qur'ani huwazuia na Njia anayo itia Rahmani. Na hao wanao tumiliwa wanadhani kwa kuwafuata rafiki zao kwamba wao wamo katika uwongofu.
Tafsyrai arabų kalba:
حَتَّىٰٓ إِذَا جَآءَنَا قَالَ يَٰلَيۡتَ بَيۡنِي وَبَيۡنَكَ بُعۡدَ ٱلۡمَشۡرِقَيۡنِ فَبِئۡسَ ٱلۡقَرِينُ
Hata atakapo tujia atasema: Laiti ungeli kuwako baina yangu na wewe kama umbali baina ya mashariki na magharibi. Rafiki mwovu mno wewe!
Hata yule aliye jipa upofu na Qur'ani atapo fika kwa Mwenyezi Mungu Siku ya Kiyama, na akaona matokeo ya kule kujitia kwake upofu, atamwambia rafiki yake kwa majuto: Laiti wewe nami tungeli kuwa mbali mbali duniani umbali wa mashariki na magharibi! Ama wewe ulikuwa sahibu muovu mno kwangu, mpaka umekuja nitumbukize katika shimo la Motoni!
Tafsyrai arabų kalba:
وَلَن يَنفَعَكُمُ ٱلۡيَوۡمَ إِذ ظَّلَمۡتُمۡ أَنَّكُمۡ فِي ٱلۡعَذَابِ مُشۡتَرِكُونَ
Na kwa kuwa mlidhulumu, haitakufaeni kitu leo kwamba nyinyi mnashirikiana katika adhabu.
Na hapo wataambiwa kwa kuwahizi: Leo hamtapunguziwa adhabu, kwani mmejidhulumu wenyewe kwa ukafiri wenu, kwa sababu mlishirikiana na mashetani wenu. Kwani kila mmoja anateseka kwa adhabu ya kumtosha mwenyewe.
Tafsyrai arabų kalba:
أَفَأَنتَ تُسۡمِعُ ٱلصُّمَّ أَوۡ تَهۡدِي ٱلۡعُمۡيَ وَمَن كَانَ فِي ضَلَٰلٖ مُّبِينٖ
Je! Unaweza kuwasikilizisha viziwi, au unaweza kuwaongoa vipofu na waliomo katika upotofu ulio wazi?
Je! Unaweza kumwongoa aliye pita mipaka katika upotovu? Je! Unaweza kumfanya asikie aliye kiziwi hasikii la kweli, kipofu hazingatii, na ambaye katika ujuzi wa Mwenyezi Mungu atakufa katika upotovu? Huwezi hayo! Kwa sababu hao wamekwisha thibiti katika ukafiri wao, basi hawanafiiki kwa wanayo yasikia, wala wanayo yaona.
Tafsyrai arabų kalba:
فَإِمَّا نَذۡهَبَنَّ بِكَ فَإِنَّا مِنۡهُم مُّنتَقِمُونَ
Na hata tukikuondoa, Sisi tutalipiza kisasi chetu kwao.
Basi tukikushika tukakufisha kabla hatuja kuonyesha adhabu yao, na kifua chako kikatua kwa hayo, na pia vifua vya Waumini, alaa kulli hali, Sisi bila ya shaka tutawaadhibu duniani na Akhera.
Tafsyrai arabų kalba:
أَوۡ نُرِيَنَّكَ ٱلَّذِي وَعَدۡنَٰهُمۡ فَإِنَّا عَلَيۡهِم مُّقۡتَدِرُونَ
Au tutakuonyesha tulio waahidi. Nasi bila ya shaka tuna uweza juu yao.
Au unataka tukuonyeshe adhabu tuliyo waahidi kabla ya kufa kwako, tutakuonyesha, kwani Sisi tunawaweza hao kwa uweza wetu na nguvu zetu.
Tafsyrai arabų kalba:
فَٱسۡتَمۡسِكۡ بِٱلَّذِيٓ أُوحِيَ إِلَيۡكَۖ إِنَّكَ عَلَىٰ صِرَٰطٖ مُّسۡتَقِيمٖ
Basi wewe yashike yaliyo funuliwa kwako. Hakika wewe uko kwenye Njia Iliyo Nyooka.
Ikiwa moja ya mawili haya lazima liwe bila ya shaka, basi shikamana na Qur'ani tuliyo kufunulia, na simama imara katika kuitekeleza, kwani hakika wewe uko katika Njia ya Haki Iliyo Nyooka.
Tafsyrai arabų kalba:
وَإِنَّهُۥ لَذِكۡرٞ لَّكَ وَلِقَوۡمِكَۖ وَسَوۡفَ تُسۡـَٔلُونَ
Na hakika haya ni ukumbusho kwako na kwa kaumu yako. Na mtakuja ulizwa.
Na hakika hii Qur'ani ni utukufu mkubwa juu yako, ewe Muhammad, na wa Umma wako, kwa kuwa umeteremshiwa kwa lugha ya Kiarabu, na mtakuja kuhojiwa Siku ya Kiyama juu ya haki yake, na shukrani za neema zake.
Tafsyrai arabų kalba:
وَسۡـَٔلۡ مَنۡ أَرۡسَلۡنَا مِن قَبۡلِكَ مِن رُّسُلِنَآ أَجَعَلۡنَا مِن دُونِ ٱلرَّحۡمَٰنِ ءَالِهَةٗ يُعۡبَدُونَ
Na waulize Mitume wetu tulio watuma kabla yako: Je! Tulifanya miungu mingine iabudiwe badala ya Rah'mani?
Na hebu angalia katika sharia za Mitume wetu tulio watuma kabla yako. Ati umekuja humo wito wa kuwaita watu wende kuabudu vitu visio kuwa Mwenyezi Mungu? Haukuja! Basi hao wanao abudu asiye kuwa Mwenyezi Mungu mmoja hadi wamepita mipaka katika upotovu wao!
Tafsyrai arabų kalba:
وَلَقَدۡ أَرۡسَلۡنَا مُوسَىٰ بِـَٔايَٰتِنَآ إِلَىٰ فِرۡعَوۡنَ وَمَلَإِيْهِۦ فَقَالَ إِنِّي رَسُولُ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Na bila ya shaka tulimtuma Musa kwa Ishara zetu ende kwa Firauni na waheshimiwa wake, na akasema: Hakika mimi ni Mtume wa Mola Mlezi wa walimwengu wote!
Na bila ya shaka Sisi tulimtuma Musa tukampa miujiza yenye kuthibitisha ukweli wake, ende kwa Firauni na watu wake. Akasema: Hakika mimi ni Mtume wa Muumba wa walimwengu wote na Mlezi wao nimetumwa kwenu. Wakamtaka aonyeshe miujiza.
Tafsyrai arabų kalba:
فَلَمَّا جَآءَهُم بِـَٔايَٰتِنَآ إِذَا هُم مِّنۡهَا يَضۡحَكُونَ
Lakini alipo wajia na Ishara zetu wakaingia kuzicheka.
Alipo wajia kwa miujiza ya kuthibitisha Utume wake mara wakampokea kwa kumcheka, na kumfanyia tashtiti, na kumcheza shere, bila ya kuzingatia maneno yake.
Tafsyrai arabų kalba:
 
Reikšmių vertimas Sūra: Az-Zukhruf
Sūrų turinys Puslapio numeris
 
Kilniojo Korano reikšmių vertimas - Vertimas į suahilių k. - Ali Muhsin Al-Barvani - Vertimų turinys

Išvertė Ali Muhsin Al-Barvani.

Uždaryti