Kilniojo Korano reikšmių vertimas - Suahilių k. vertimas - Ali Muchsen Al-Beruany * - Vertimų turinys

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Reikšmių vertimas Aja (Korano eilutė): (122) Sūra: Sūra Al-An’am
أَوَمَن كَانَ مَيۡتٗا فَأَحۡيَيۡنَٰهُ وَجَعَلۡنَا لَهُۥ نُورٗا يَمۡشِي بِهِۦ فِي ٱلنَّاسِ كَمَن مَّثَلُهُۥ فِي ٱلظُّلُمَٰتِ لَيۡسَ بِخَارِجٖ مِّنۡهَاۚ كَذَٰلِكَ زُيِّنَ لِلۡكَٰفِرِينَ مَا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ
Je, aliye kuwa maiti kisha tukamhuisha, na tukamjaalia nuru inakwenda naye mbele za watu, mfano wake ni kama aliyoko gizani akawa hata hawezi kutoka humo? Kama hivyo makafiri wamepambiwa waliyo kuwa wakiyafanya.
Na nyinyi kwa Imani yenu si mfano wa washirikina hata kidogo. Basi haiwezi kuwa hali ya aliye kama maiti katika kupotea kwake, na Mwenyezi Mungu akampa nuru ya kuhidika, ambayo ni kama uhai, na akampa nuru ya Imani na hoja zilizo wazi, na kwa mwangaza wa nuru hiyo akaongoka na akawa anatembea nayo, haiwezi kuwa hali hiyo mfano wa hali ya ambaye kwamba anaishi katika giza lilio gubika. Na kama Mwenyezi Mungu alivyo ipamba Imani katika nyoyo za watu wa Imani, vile vile Shetani ameipamba shirki katika nafsi za madhaalimu wapinzani.
Tafsyrai arabų kalba:
 
Reikšmių vertimas Aja (Korano eilutė): (122) Sūra: Sūra Al-An’am
Sūrų turinys Puslapio numeris
 
Kilniojo Korano reikšmių vertimas - Suahilių k. vertimas - Ali Muchsen Al-Beruany - Vertimų turinys

Kilniojo Korano reikšmių vertimas į suahilių k., išvertė Ali Muchsin Al-Birvany.

Uždaryti