Wale walio kufuru na kuzuilia Njia ya Mwenyezi Mungu tutawazidishia adhabu juu ya adhabu, kwa walivyo kuwa wakifisidi.
Walio kufuru na wakawazuia wengine kufuata Njia ya Mwenyezi Mungu, nayo ndiyo Njia ya kheri na haki, tutawazidishia adhabu juu ya adhabu wanayo stahiki kwa ukafiri wao, kwa walivyo kusudia kuwafisidi na kuwapotosha waja wa Mwenyezi Mungu!
Na (waonye) siku tutakapo wainua mashahidi katika kila umma wakiwashuhudia kwa yanayo tokana na wao, na tutakuleta wewe uwe shahidi juu ya hao. Na tumekuteremshia Kitabu hiki kinacho bainisha kila kitu, na ni uwongofu,na rehema, na bishara kwa Waislamu.
Ewe Nabii! Wahadharishe makafiri katika kaumu yako kwa yatakayo wapata Siku tutapo watolea kila umma shahidi wa kuwashuhudia, naye ndiye Nabii wao, ambaye atakuwa ni mmoja wao, ili wawe hawana kisingizio. Na wewe, ewe Nabii, tutakuleta uwashuhudie hao walio kukadhibisha. Na tangu hivi sasa yawapasa wazingatie! Sisi tumekuteremshia wewe Qur'ani, ambayo ndani yake kila kitu kimebainishwa kwa haki. Na ndani yake umo uwongofu, na rehema, na bishara ya Pepo kwa wenye kuifuata na kuiamini.
Hakika Mwenyezi Mungu anaamrisha kufanya uadilifu, na hisani,na kuwapa jamaa; na anakataza uchafu, na uovu, na dhulma. Anakuwaidhini ili mpate kukumbuka.
Mwenyezi Mungu anawaamrisha waja wake uadilifu wa maneno na vitendo, na katika kila jambo wakusudie lilio bora, na walifadhilishe kuliko jenginelo. Kama anavyo amrisha kuwapa jamaa zenu wanacho hitajia, ili kuzidi kutia nguvu makhusiano ya mapenzi kati ya ukoo. Na Mwenyezi Mungu anakataza kutenda kila la makosa, na khasa madhambi yaliyo pita mpaka kwa ubaya, na kila kisicho pendeza katika sharia na akili nzuri. Hali kadhaalika anakataza kumfanyia uadui mtu. Na Mwenyezi Mungu Aliye takasika anakukumbusheni haya, na anakuelekezeni kwenye mambo mema, mpate kukumbuka fadhila zake kwa maelekezo yake mema,basi ndio mfanye anavyo kwambieni.
Na timizeni ahadi ya Mwenyezi Mungu mnapo ahidi, wala msivunje viapo baada ya kuvithibitisha, ilihali mmekwisha mfanya Mwenyezi Mungu ndiye mdhamini wenu. Hakika Mwenyezi Mungu anayajua myatendayo.
Na timizeni ahadi mlizo jitolea nafsi zenu kwa kumshuhudisha Mwenyezi kuwa mtazitekeleza, maadamu ahadi hizo ni kwa mujibu wa sharia ya Mwenyezi Mungu. Wala msivunje viapo vyenu kwa kutotimiza baada ya kuvitilia nguvu kwa kumtaja Mwenyezi Mungu, na kuazimia kikweli kutimiza. Nanyi mlipo toa ahadi mlitia maanani kuwa Mwenyezi Mungu ndiye dhamini wenu kwamba mtatekeleza, na kwamba Mwenyezi Mungu anakuangalieni na kukuoneni. Basi shikamaneni na ahadi zenu na viapo vyenu, kwani Mwenyezi Mungu Subhanahu anakujueni yupi katika nyinyi anaye timiza na anaye kwenda kinyume, yupi anaye tekeleza na yupi anaye vunja. Basi atakulipeni kwa mnayo yafanya.
Wala msiwe kama mwanamke anaye uzongoa uzi wake baada ya kwisha usokota ukawa mgumu. Mnavifanya viapo vyenu kuwa ni njia ya kudanganyana baina yenu kwa kuwa ati taifa moja lina nguvu zaidi kuliko jengine? Hakika Mwenyezi Mungu anakujaribuni kwa njia hiyo. Na bila ya shaka atakubainishieni Siku ya Kiyama mliyo kuwa mkikhitalifiana.
Wala msiwe katika kwenda kinyume na viapo vyenu baada ya kuvithibitisha mfano wa mwanamke mwendawazimu anaye sokoto sufi, ikisha kuwa nyuzi akazifumua tena. Mkafanya viapo vyenu kuwa ni njia ya kudanganya na kukhadaa watu, na huku mkijitafutia udhuru kwa kuwa ama nyinyi ni wengi zaidi au mna nguvu zaidi kuliko wao, au mnakusudia kuwaunga mkono maadui wenye nguvu zaidi kuliko wao, au kwa kuwa mnataraji kuzidi nguvu kwa khiana! Na hakika Mwenyezi Mungu anakufanyieni mtihani. Mkikhiari kutimiza ahadi mtapata mavuno ya duniani na Akhera. Mkielekea khiana, basi ni khasara yenu. Na hakika Siku ya Kiyama atakubainishieni ukweli wa khitilafu zenu za duniani, na atakulipeni kwa mujibu wa vitendo vyenu. Aya mbili hizi zinaonyesha kuwa msingi wa makhusiano baina ya Waislamu na wengineo pamoja na uadilifu ni kutimiza ahadi, na kwamba makhusiano baina ya mataifa hayasimami sawa ila kwa kutimiza ahadi, na kwamba dola za Kiislamu zikijifunga kwa mapatano basi zijifunge kwa jina la Mwenyezi Mungu. Maana ya hayo ni kuwa inakuwapo yamini ya Mwenyezi Mungu na kuwa Yeye ndiye dhamini. Na Aya inafahamisha mambo matatu, ambayo lau kuwa mataifa yangeli yatimiza basi amani ingeli enea: Kwanza: Haifai mapatano kuwa ndio njia ya kufanya khadaa. Ikiwa hivyo inakuwa ni udanganyifu. Na udanganyifu haufai katika makhusiano baina ya wanaadamu, sawa sawa ikiwa baina ya mtu na mtu, au kikundi na kikundi, au baina ya madola. Pili: Kutimiza ahadi peke yake ni nguvu. Na mwenye kuvunja ahadi ni kama mwenye kuvunja alicho kijenga kwa sababu za nguvu. Basi anakuwa kama mpumbavu anaye tatua uzi wake kila akisha usokota. Tatu: Haimfalii mtu kuvunja ahadi kwa sababu ya kutafuta nguvu au kutaka kuzidisha kipande cha ardhi.
Na Mwenyezi Mungu angeli taka, kwa yakini angeli kufanyeni umma mmoja. Lakini anamwachia kupotea anaye mtaka, na anamwongoa amtakaye. Na hakika mtaulizwa kwa yale mliyo kuwa mkiyafanya.
Mwenyezi Mungu ange taka angeli kufanyeni nyote umma wa namna moja kwa jinsi, na rangi, na imani, bila ya khitilafu. Na hayo ni kwa kukupeni umbo jengine, mkawa kama Malaika wasio na uwezo wa kukhiari watakalo. Lakini ametaka muwe jinsi na rangi mbali mbali, na akakupeni uwezo wa kukhiari wenyewe. Mwenye kukhiari matamanio ya dunia kuliko kumridhi Mwenyezi Mungu, anaachwa kwa ayatakayo. Na mwenye kutaka kumridhi Mwenyezi Mungu kwa vitendo vyema, anasahilishiwa kwa anayo yataka. Na kuweni na yakini kuwa nyote nyinyi mtakuja ulizwa Siku ya Kiyama juu ya mliyo yatenda duniani, na mtalipwa kwa vitendo vyenu.
Contents of the translations can be downloaded and re-published, with the following terms and conditions:
1. No modification, addition, or deletion of the content.
2. Clearly referring to the publisher and the source (QuranEnc.com).
3. Mentioning the version number when re-publishing the translation.
4. Keeping the transcript information inside the document.
5. Notifying the source (QuranEnc.com) of any note on the translation.
6. Updating the translation according to the latest version issued from the source (QuranEnc.com).
7. Inappropriate advertisements must not be included when displaying translations of the meanings of the Noble Quran.
തിരയൽ ഫലങ്ങൾ:
API specs
Endpoints:
Sura translation
GET / https://quranenc.com/api/v1/translation/sura/{translation_key}/{sura_number} description: get the specified translation (by its translation_key) for the speicified sura (by its number)
Parameters: translation_key: (the key of the currently selected translation) sura_number: [1-114] (Sura number in the mosshaf which should be between 1 and 114)
Returns:
json object containing array of objects, each object contains the "sura", "aya", "translation" and "footnotes".
GET / https://quranenc.com/api/v1/translation/aya/{translation_key}/{sura_number}/{aya_number} description: get the specified translation (by its translation_key) for the speicified aya (by its number sura_number and aya_number)
Parameters: translation_key: (the key of the currently selected translation) sura_number: [1-114] (Sura number in the mosshaf which should be between 1 and 114) aya_number: [1-...] (Aya number in the sura)
Returns:
json object containing the "sura", "aya", "translation" and "footnotes".