Vertaling van de betekenissen Edele Qur'an - Swahili vertaling,Abdallah Mohammed Abubaker en Nassor Khamis Abdarahman * - Index van vertaling


Vertaling van de betekenissen Vers: (15) Surah: Soerat Joenoes (Jonas)
وَإِذَا تُتۡلَىٰ عَلَيۡهِمۡ ءَايَاتُنَا بَيِّنَٰتٖ قَالَ ٱلَّذِينَ لَا يَرۡجُونَ لِقَآءَنَا ٱئۡتِ بِقُرۡءَانٍ غَيۡرِ هَٰذَآ أَوۡ بَدِّلۡهُۚ قُلۡ مَا يَكُونُ لِيٓ أَنۡ أُبَدِّلَهُۥ مِن تِلۡقَآيِٕ نَفۡسِيٓۖ إِنۡ أَتَّبِعُ إِلَّا مَا يُوحَىٰٓ إِلَيَّۖ إِنِّيٓ أَخَافُ إِنۡ عَصَيۡتُ رَبِّي عَذَابَ يَوۡمٍ عَظِيمٖ
Na wasomewapo washirikina aya za Mwenyezi Mungu zilizo wazi tulizokuteremshia wewe, ewe Mtume, husema wale ambao hawaogopi Hesabu wala hawatarajii malipo wala hawaamini Siku ya kufufuliwa na kuhuishwa, «Lete qur’ani isiyokuwa hii, au tugeuze hii Qur’ani: uifanye halali kuwa haramu na haramu kuwa halali, ahadi kuwa onyo na onyo kuwa ahadi, na uondoe yaliyomo ndani yake ya kukashifu waungu wetu na kuzifanya za kipumbavu akili zetu.» Waambie, ewe Mtume,»Hilo haliko kwangu. Kwani mimi nafuata, katika kila ninalowaamrisha na ninalowakataza, yale ambayo Mola wangu Ameniteremshia na kuniamrisha kwayo. Mimi naogopa kutoka kwa Mwenyezi Mungu, nikienda kinyume na amri Yake, adhabu ya siku iliyo kubwa , nayo ni Siku ya Kiyama.
Arabische uitleg van de Qur'an:
 
Vertaling van de betekenissen Vers: (15) Surah: Soerat Joenoes (Jonas)
Surah's Index Pagina nummer
 
Vertaling van de betekenissen Edele Qur'an - Swahili vertaling,Abdallah Mohammed Abubaker en Nassor Khamis Abdarahman - Index van vertaling

De vertaling van de betekenissen van de Heilige Koran naar het Swahili, vertaald door Dr. Abdullah Mohammed Abu Bakr en Sheikh Naser Khamis.

Sluit