Vertaling van de betekenissen Edele Qur'an - Swahili vertaling,Abdallah Mohammed Abubaker en Nassor Khamis Abdarahman * - Index van vertaling


Vertaling van de betekenissen Vers: (90) Surah: Soerat De bij (an-Nahl)
۞ إِنَّ ٱللَّهَ يَأۡمُرُ بِٱلۡعَدۡلِ وَٱلۡإِحۡسَٰنِ وَإِيتَآيِٕ ذِي ٱلۡقُرۡبَىٰ وَيَنۡهَىٰ عَنِ ٱلۡفَحۡشَآءِ وَٱلۡمُنكَرِ وَٱلۡبَغۡيِۚ يَعِظُكُمۡ لَعَلَّكُمۡ تَذَكَّرُونَ
Hakika Mwenyezi Mungu, kutakata na sifa za upungufu ni Kwake na kutukuka ni Kwake, Anawaamrisha waja Wake ndani ya Qur’ani hii wawe waadilifu, wafanye usawa katika kutunza haki Yake, kwa kumpwekesha Yeye na kutomshirikisha, na haki ya waja Wake, kwa kumpa haki yake kila mwenye haki. Na Anaamrisha kufanya wema katika kutekeleza haki Yake, kwa kumuabudu na kutekeleza faradhi Zake kwa namna ilivyopasishwa na Sheria, na kuwafanyia wema viumbe Wake katika maneno na vitendo. Na Anaamrisha kuwapa walio na ukaribu wa ujamaa kitu cha kuwaunga na kuwatendea wema. Na Anakataza kila ambalo ni ovu, likiwa ni neno au ni tendo, na ambalo Sheria inalipinga na haikubaliani nalo la ukafiri na maasia, na kuwadhulumu watu na kuwafanyia maonevu. Na Mwenyezi Mungu, kwa maamrisho haya na makatazo haya, Anawaidhia na kuwakumbusha mwisho mbaya, ili mzikumbuke amri za Mweneyzi Mungu na mnufaike nazo.
Arabische uitleg van de Qur'an:
 
Vertaling van de betekenissen Vers: (90) Surah: Soerat De bij (an-Nahl)
Surah's Index Pagina nummer
 
Vertaling van de betekenissen Edele Qur'an - Swahili vertaling,Abdallah Mohammed Abubaker en Nassor Khamis Abdarahman - Index van vertaling

De vertaling van de betekenissen van de Heilige Koran naar het Swahili, vertaald door Dr. Abdullah Mohammed Abu Bakr en Sheikh Naser Khamis.

Sluit