Check out the new design

Vertaling van de betekenissen Edele Qur'an - Swahili vertaling - Abdoellah Mohammed en Nasser Khamees * - Index van vertaling


Vertaling van de betekenissen Surah: al-Kahf   Vers:
۞ قَالَ أَلَمۡ أَقُل لَّكَ إِنَّكَ لَن تَسۡتَطِيعَ مَعِيَ صَبۡرٗا
Akasema Al-Khiḍr kumwambia Mūsā kwa kumlaumu na kumkumbusha, «Je, sikukwambia kuwa wewe hutoweza kuvumilia pamoja na mimi kwa matendo unayoyaona kutoka kwangu katika yale ambayo hayakuzungukwa na ujuzi wako?»
Arabische uitleg van de Qur'an:
قَالَ إِن سَأَلۡتُكَ عَن شَيۡءِۭ بَعۡدَهَا فَلَا تُصَٰحِبۡنِيۖ قَدۡ بَلَغۡتَ مِن لَّدُنِّي عُذۡرٗا
Mūsā akamwambia, «Nikikuuliza kitu baada ya mara hii, niache na usifuatane na mimi, utakuwa ushapata sababu kuhusu mimi na hutakuwa umefanya kasoro, kwa kuwa ulinambia kwamba mimi sitaweza kuvumilia pamoja na wewe.»
Arabische uitleg van de Qur'an:
فَٱنطَلَقَا حَتَّىٰٓ إِذَآ أَتَيَآ أَهۡلَ قَرۡيَةٍ ٱسۡتَطۡعَمَآ أَهۡلَهَا فَأَبَوۡاْ أَن يُضَيِّفُوهُمَا فَوَجَدَا فِيهَا جِدَارٗا يُرِيدُ أَن يَنقَضَّ فَأَقَامَهُۥۖ قَالَ لَوۡ شِئۡتَ لَتَّخَذۡتَ عَلَيۡهِ أَجۡرٗا
Mūsā akaenda na Al-Khiḍr mpaka wakafika kwa watu wa kijiji, wakataka wapewe chakula kwa njia ya makaribisho. Watu wa kijijini walikataa kuwakaribisha. Kisha wao wawili walipata hapo ukuta ulioinama uliokaribia kuanguka, Al-Khiḍr akaulinganisha mpaka ukawa uko sawa. Mūsā akamwambia, «Lau ungalitaka ungalichukua kwa kazi hii malipo ukayatumia kujipatia chakula chetu kwa kuwa wao hawakutukaribisha.»
Arabische uitleg van de Qur'an:
قَالَ هَٰذَا فِرَاقُ بَيۡنِي وَبَيۡنِكَۚ سَأُنَبِّئُكَ بِتَأۡوِيلِ مَا لَمۡ تَسۡتَطِع عَّلَيۡهِ صَبۡرًا
Al-Khiḍr akamwambia Mūsā, «Huu ndio wakati wa kupambanukana mimi na wewe. Nitakuelezea habari ya matendo yangu niliyoyafanya ambayo wewe ulinipinga nayo na ambayo hukuweza kuwa na uvumilivu wa kutoyauliza na kutonipinga mimi kuhusu hayo.
Arabische uitleg van de Qur'an:
أَمَّا ٱلسَّفِينَةُ فَكَانَتۡ لِمَسَٰكِينَ يَعۡمَلُونَ فِي ٱلۡبَحۡرِ فَأَرَدتُّ أَنۡ أَعِيبَهَا وَكَانَ وَرَآءَهُم مَّلِكٞ يَأۡخُذُ كُلَّ سَفِينَةٍ غَصۡبٗا
«Ama mashua ambayo nilitoboa tundu, ilikuwa ni ya watu masikini wanaofanya kazi baharini wakiwa ndani yake wakijitafutia riziki, nikataka kuitia kombo kwa kuitoboa, kwa kuwa mbele yao kulikuwa na mfalme anayechukuwa kila mashua nzuri kwa kuwanyang’anya wenyewe.
Arabische uitleg van de Qur'an:
وَأَمَّا ٱلۡغُلَٰمُ فَكَانَ أَبَوَاهُ مُؤۡمِنَيۡنِ فَخَشِينَآ أَن يُرۡهِقَهُمَا طُغۡيَٰنٗا وَكُفۡرٗا
Na ama mvulana niliyemuua alikuwa, katika ujuzi wa Mwenyezi Mungu, ni kafiri, na babake na mamake walikuwa Waumini, tukaogopa lau huyu mvulana ataendelea kuishi atawatia wazazi wake kwenye ukafiri na udhalimu wenye kupita kiasi kwa kumpenda kwao au kwa kumuhitajia.
Arabische uitleg van de Qur'an:
فَأَرَدۡنَآ أَن يُبۡدِلَهُمَا رَبُّهُمَا خَيۡرٗا مِّنۡهُ زَكَوٰةٗ وَأَقۡرَبَ رُحۡمٗا
«Tukataka Mwenyezi Mungu Ampe badala yake aliyetengenea zaidi kwa wema , dini na utiifu kwa wao wawili.
Arabische uitleg van de Qur'an:
وَأَمَّا ٱلۡجِدَارُ فَكَانَ لِغُلَٰمَيۡنِ يَتِيمَيۡنِ فِي ٱلۡمَدِينَةِ وَكَانَ تَحۡتَهُۥ كَنزٞ لَّهُمَا وَكَانَ أَبُوهُمَا صَٰلِحٗا فَأَرَادَ رَبُّكَ أَن يَبۡلُغَآ أَشُدَّهُمَا وَيَسۡتَخۡرِجَا كَنزَهُمَا رَحۡمَةٗ مِّن رَّبِّكَۚ وَمَا فَعَلۡتُهُۥ عَنۡ أَمۡرِيۚ ذَٰلِكَ تَأۡوِيلُ مَا لَمۡ تَسۡطِع عَّلَيۡهِ صَبۡرٗا
«Na ama ukuta nilioulinganisha, baada ya kuwa umeinama, mpaka ukawa sawa, ulikuwa ni wa wavulana wawili mayatima hapo kijijini, na chini yake kulikuwa na hazina yao ya dhahabu na fedha, na baba yao alikuwa mtu mwema, Mola wako Akataka wawe wakubwa, wapate nguvu na waitoe hazina yao kwa rehema itokayo kwa Mola wako. Na mimi sikuyafanya yote haya, ewe Mūsā, kwa amri yangu na kivyangu, kwa hakika nimeyafanya kwa amri ya Mwenyezi Mungu. Hayo niliyokueleza sababu zake ndiyo mwisho wa mambo ambayo hukuweza kuyavumilia kwa kuacha kuyauliza na kunipinga kwayo.»
Arabische uitleg van de Qur'an:
وَيَسۡـَٔلُونَكَ عَن ذِي ٱلۡقَرۡنَيۡنِۖ قُلۡ سَأَتۡلُواْ عَلَيۡكُم مِّنۡهُ ذِكۡرًا
Na hawa washiriikina wa watu wako wanakuuliza, ewe Mtume, kuhusu habari ya Dhulqarnain, mfalme aliye mwema, waambie, «Nitawapa habari kuhusu yeye ya kuwaachia kumbukumbu mupate kuikumbuka na kuizingatia.»
Arabische uitleg van de Qur'an:
 
Vertaling van de betekenissen Surah: al-Kahf
Surah's Index Pagina nummer
 
Vertaling van de betekenissen Edele Qur'an - Swahili vertaling - Abdoellah Mohammed en Nasser Khamees - Index van vertaling

Vertaald door Dr. Abdoellah Mohammed Aboe Bakr en Sheikh Nasser Khamees.

Sluit