Vertaling van de betekenissen Edele Qur'an - Swahili vertaling,Abdallah Mohammed Abubaker en Nassor Khamis Abdarahman * - Index van vertaling


Vertaling van de betekenissen Vers: (275) Surah: Soerat Albaqarah (De Koe)
ٱلَّذِينَ يَأۡكُلُونَ ٱلرِّبَوٰاْ لَا يَقُومُونَ إِلَّا كَمَا يَقُومُ ٱلَّذِي يَتَخَبَّطُهُ ٱلشَّيۡطَٰنُ مِنَ ٱلۡمَسِّۚ ذَٰلِكَ بِأَنَّهُمۡ قَالُوٓاْ إِنَّمَا ٱلۡبَيۡعُ مِثۡلُ ٱلرِّبَوٰاْۗ وَأَحَلَّ ٱللَّهُ ٱلۡبَيۡعَ وَحَرَّمَ ٱلرِّبَوٰاْۚ فَمَن جَآءَهُۥ مَوۡعِظَةٞ مِّن رَّبِّهِۦ فَٱنتَهَىٰ فَلَهُۥ مَا سَلَفَ وَأَمۡرُهُۥٓ إِلَى ٱللَّهِۖ وَمَنۡ عَادَ فَأُوْلَٰٓئِكَ أَصۡحَٰبُ ٱلنَّارِۖ هُمۡ فِيهَا خَٰلِدُونَ
Wale wenye kuamiliana kwa riba- nayo ni nyongeza juu ya rasilmali-, hawainuki kutoka kwenye makaburi yao Siku ya Mwisho isipokuwa ni kama anavyoinuka yule anayepigwa na Shetani akapatwa na wazimu. Hivo ni kwa kuwa wao walisema kwamba biashara ni kama riba, kwa kuwa yote mawili ni halali na yanapelekea mali kuongezeka. Mwenyezi Mungu Akawakanusha na Akabainisha kwamba Yeye Amehalalisha biashara na Ameharamisha riba. Kwa kuwa katika kuuza na kununua kuna nafuu kwa watu binafsi na kwa jamii na katika riba kuna unyonyaji, hasara na maangamivu. Basi mwenye kumfikia yeye makatazo ya Mwenyezi Mungu ya riba akakomeka, achukue iliyopita kabla ya kumfikia yeye uharamu wake, na hana makosa kwa hilo. Na mambo yake ya siku zake za baadae yako kwa Mwenyezi Mungu. Akiwa ataendelea na toba yake, basi Mwenyezi Mungu Hapotezi malipo ya wenye kufanya wema; na akiwa atarudia kwenye riba, basi kitendo chake hiko baada ya kufikiwa na makatazo ya Mwenyezi Mungu, kitamfanya astahili mateso, kwa kuwa hoja imesimama juu yake. Kwa ajili ya hii Alisema Mwenyezi Mungu, «Basi hao ni watu wa Motoni; Wao ndani yake watakaa milele».
Arabische uitleg van de Qur'an:
 
Vertaling van de betekenissen Vers: (275) Surah: Soerat Albaqarah (De Koe)
Surah's Index Pagina nummer
 
Vertaling van de betekenissen Edele Qur'an - Swahili vertaling,Abdallah Mohammed Abubaker en Nassor Khamis Abdarahman - Index van vertaling

De vertaling van de betekenissen van de Heilige Koran naar het Swahili, vertaald door Dr. Abdullah Mohammed Abu Bakr en Sheikh Naser Khamis.

Sluit