Vertaling van de betekenissen Edele Qur'an - Swahili vertaling,Abdallah Mohammed Abubaker en Nassor Khamis Abdarahman * - Index van vertaling


Vertaling van de betekenissen Vers: (87) Surah: Soerat Al-Ani'jaa (De Profeten)
وَذَا ٱلنُّونِ إِذ ذَّهَبَ مُغَٰضِبٗا فَظَنَّ أَن لَّن نَّقۡدِرَ عَلَيۡهِ فَنَادَىٰ فِي ٱلظُّلُمَٰتِ أَن لَّآ إِلَٰهَ إِلَّآ أَنتَ سُبۡحَٰنَكَ إِنِّي كُنتُ مِنَ ٱلظَّٰلِمِينَ
Na kumbuka kisa cha mtu wa chewa, naye ni Yūnus mwana wa Mattā, amani imshukie, Mwenyezi Mungu Alimtumiliza kwa watu wake, akawalingania wasimuamini, akawaonya kuwa wataadhibiwa, lakikni hawakurudi nyuma. Na asiwavumilie kama vile Mwenyezi Mungu Alivyomuamrisha na akaondoka kutoka kwao akiwa na hasira juu yao, akiwa amebanwa na kifua kwa kuasi kwao. Na akadhani kwamba Mwenyezi Mungu Hatampa dhiki na kumuadhibu kwa ukiukaji huu. Mwenyezi Mungu Akamtahini kwa dhiki nyingi na kifungo na akamezwa na tewa baharini, na akamlingania Mola wake kwa kumuomba katika magiza ya usiku, bahari na tumbo la tewa hali ya kutubia na kukubali ukiukaji wake kwa kuacha kuwavumilia watu wake, huku akisema, «Hapana muabudiwa kwa haki isipokuwa wewe! Kutakasika na sifa za upungufu ni kwako! kwa hakika mimi nimekuwa miongoni mwa wenye kudhulumu!»
Arabische uitleg van de Qur'an:
 
Vertaling van de betekenissen Vers: (87) Surah: Soerat Al-Ani'jaa (De Profeten)
Surah's Index Pagina nummer
 
Vertaling van de betekenissen Edele Qur'an - Swahili vertaling,Abdallah Mohammed Abubaker en Nassor Khamis Abdarahman - Index van vertaling

De vertaling van de betekenissen van de Heilige Koran naar het Swahili, vertaald door Dr. Abdullah Mohammed Abu Bakr en Sheikh Naser Khamis.

Sluit