Check out the new design

Vertaling van de betekenissen Edele Qur'an - Swahili vertaling - Abdoellah Mohammed en Nasser Khamees * - Index van vertaling


Vertaling van de betekenissen Surah: Al-Ahzaab   Vers:
تَحِيَّتُهُمۡ يَوۡمَ يَلۡقَوۡنَهُۥ سَلَٰمٞۚ وَأَعَدَّ لَهُمۡ أَجۡرٗا كَرِيمٗا
Maamkizi ya hawa Waumini kutoka kwa Mwenyezi Mungu huko Peponi Siku ya wao kukutana na Yeye ni Salām na amani kwao kutokana na adhabu ya Mwenyezi Mungu. Na Amewaandalia wao malipo Mazuri, nayo ni Pepo.
Arabische uitleg van de Qur'an:
يَٰٓأَيُّهَا ٱلنَّبِيُّ إِنَّآ أَرۡسَلۡنَٰكَ شَٰهِدٗا وَمُبَشِّرٗا وَنَذِيرٗا
Ewe Nabii! Sisi tumekutumiza uwe ni shahidi juu ya ummah wako kwa kuwafikishia ujumbe, na kuwabashiria Waumini miongoni mwao rehema na Pepo, na uwe ni mwenye kuwaonya na Moto waasi na wakanushaji.
Arabische uitleg van de Qur'an:
وَدَاعِيًا إِلَى ٱللَّهِ بِإِذۡنِهِۦ وَسِرَاجٗا مُّنِيرٗا
Na uwe ni mlinganizi kwenye kumpwekesha Mwenyezi Mungu na kumuabudu Yeye Peke Yake, na uwe ni taa yenye kung’ara kwa anayetaka kupata mwangaza kwako. Kwani jambo lako la haki ambalo umekuja nalo liko wazi kama vile jua katika kuchomoza na kutoa mwangaza, hakuna mwenye kulikanusha isipokuwa mshindani.
Arabische uitleg van de Qur'an:
وَبَشِّرِ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ بِأَنَّ لَهُم مِّنَ ٱللَّهِ فَضۡلٗا كَبِيرٗا
Na uwape bishara njema, ewe Nabii, watu wa Imani kuwa watakuwa na malipo makubwa kutoka kwa Mwenyezi Mungu, nayo ni mabustani ya Peponi.
Arabische uitleg van de Qur'an:
وَلَا تُطِعِ ٱلۡكَٰفِرِينَ وَٱلۡمُنَٰفِقِينَ وَدَعۡ أَذَىٰهُمۡ وَتَوَكَّلۡ عَلَى ٱللَّهِۚ وَكَفَىٰ بِٱللَّهِ وَكِيلٗا
Na usilitii, ewe Nabii, neno la kafiri au mnafiki na uuache udhia wao, na hilo lisikuzuie kufikisha ujumbe, na kuwa na imani na Mwenyezi Mungu katika mambo yako yote, na umtegemee Yeye, kwani Yeye Atakutosheleza yanayokutia hamu miongoni mwa mambo yote ya ulimwengu na Akhera.
Arabische uitleg van de Qur'an:
يَٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ إِذَا نَكَحۡتُمُ ٱلۡمُؤۡمِنَٰتِ ثُمَّ طَلَّقۡتُمُوهُنَّ مِن قَبۡلِ أَن تَمَسُّوهُنَّ فَمَا لَكُمۡ عَلَيۡهِنَّ مِنۡ عِدَّةٖ تَعۡتَدُّونَهَاۖ فَمَتِّعُوهُنَّ وَسَرِّحُوهُنَّ سَرَاحٗا جَمِيلٗا
Enyi mliomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na mkafuata sheria Yake kivitendo, mfungapo ndoa na wanawake na msiwaingilie, kisha mkawaacha kabla hamjawaingilia, basi hawalazimiki wakae eda lenu la nyinyi kuwahesabia, basi wapeni kitu cha kuwastarehesha katika mali yenu kulingana na ukunjufu mlionao ili kuwapa maliwazo, na wafungueni washike njia waende zao pamoja na sitara nzuri, bila ya udhia wala madhara.
Arabische uitleg van de Qur'an:
يَٰٓأَيُّهَا ٱلنَّبِيُّ إِنَّآ أَحۡلَلۡنَا لَكَ أَزۡوَٰجَكَ ٱلَّٰتِيٓ ءَاتَيۡتَ أُجُورَهُنَّ وَمَا مَلَكَتۡ يَمِينُكَ مِمَّآ أَفَآءَ ٱللَّهُ عَلَيۡكَ وَبَنَاتِ عَمِّكَ وَبَنَاتِ عَمَّٰتِكَ وَبَنَاتِ خَالِكَ وَبَنَاتِ خَٰلَٰتِكَ ٱلَّٰتِي هَاجَرۡنَ مَعَكَ وَٱمۡرَأَةٗ مُّؤۡمِنَةً إِن وَهَبَتۡ نَفۡسَهَا لِلنَّبِيِّ إِنۡ أَرَادَ ٱلنَّبِيُّ أَن يَسۡتَنكِحَهَا خَالِصَةٗ لَّكَ مِن دُونِ ٱلۡمُؤۡمِنِينَۗ قَدۡ عَلِمۡنَا مَا فَرَضۡنَا عَلَيۡهِمۡ فِيٓ أَزۡوَٰجِهِمۡ وَمَا مَلَكَتۡ أَيۡمَٰنُهُمۡ لِكَيۡلَا يَكُونَ عَلَيۡكَ حَرَجٞۗ وَكَانَ ٱللَّهُ غَفُورٗا رَّحِيمٗا
Ewe Nabii! Tumekuhalalishia wake uliowapa mahari yao, na tumekuhalalishia wajakazi waliomilikiwa na mkono wako miongoni mwa wale ambao Mwenyezi Mungu Amekuneemesha nao, na tumekuhalalishia kuwaoa wana wa kike wa ami zako na wana wa kike wa shangazi zako na wana wa kike wa khalati zako waliohama (kuja Madina) pamoja na wewe, na tumekuhalalishia mwanamke Muumini aliyekutunukia nafsi yake bila mahari, iwapo unataka kumuoa, hili ni lako wewe peke yako, na haifai kwa asiyekuwa wewe kumuoa mwanamke kwa kutunukiwa. Tushajua kile tulichowalazimisha Waumini kuhusu wake zao na wajakazi wao kuwa wasioe isipokuwa wake wanne, idadi wanayoitaka ya wajakazi na ulazima wa walii, mahari na mashahidi juu yao. Lakini tumekuruhusu wewe na tumekupa nafasi ambayo hatukumpa mtu mwingine asiyekuwa wewe, ili kifua chako kisiingie dhiki juu ya kuwaoa wale uliowaoa kati ya aina hizi. Hii ni miongoni mwa ziada ya utunzi wa Mwenyezi Mungu kwa Mtume Wake, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, na takrima Yake kwake. Na Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe dhambi za waja Wake Waumini, ni Mwenye huruma kwa kuwapanulia (milango ya riziki).
Arabische uitleg van de Qur'an:
 
Vertaling van de betekenissen Surah: Al-Ahzaab
Surah's Index Pagina nummer
 
Vertaling van de betekenissen Edele Qur'an - Swahili vertaling - Abdoellah Mohammed en Nasser Khamees - Index van vertaling

Vertaald door Dr. Abdoellah Mohammed Aboe Bakr en Sheikh Nasser Khamees.

Sluit