Vertaling van de betekenissen Edele Qur'an - Swahili vertaling,Abdallah Mohammed Abubaker en Nassor Khamis Abdarahman * - Index van vertaling


Vertaling van de betekenissen Vers: (96) Surah: Soerat el-Anaam (Het vee)
فَالِقُ ٱلۡإِصۡبَاحِ وَجَعَلَ ٱلَّيۡلَ سَكَنٗا وَٱلشَّمۡسَ وَٱلۡقَمَرَ حُسۡبَانٗاۚ ذَٰلِكَ تَقۡدِيرُ ٱلۡعَزِيزِ ٱلۡعَلِيمِ
Na Mwenyezi Mungu, kutakata na sifa za upungufu ni Kwake na kutukuka ni Kwake, Ndiye Ambaye Alipasua mwangaza wa asubuhi kutoka kwenye giza la usiku, na Akaufanya usiku ni wakati wa utulivu, anatulia humo anayechoka mchana na kupata fungu lake la mapumziko, na Akalifanya jua na mwezi zinatembea katika njia zake kwa hesabu ya sawsawa iliyokadiriwa, haibadiliki wala haigongani. Hayo ndiyo makadirio ya Al- ’Azīz, Mwenye kushinda, ambaye ufalme Wake umeshinda, Al- ’Alīm, Aliye Mjuzi wa maslahi ya viumbe Wake na kuendesha mambo yao. Al- ’Azīz na Al- ’Alīm ni miongoni mwa majina ya Mwenyezi Mungu mazuri yanayoonesha ukamilifu wa ushindi na ujuzi.
Arabische uitleg van de Qur'an:
 
Vertaling van de betekenissen Vers: (96) Surah: Soerat el-Anaam (Het vee)
Surah's Index Pagina nummer
 
Vertaling van de betekenissen Edele Qur'an - Swahili vertaling,Abdallah Mohammed Abubaker en Nassor Khamis Abdarahman - Index van vertaling

De vertaling van de betekenissen van de Heilige Koran naar het Swahili, vertaald door Dr. Abdullah Mohammed Abu Bakr en Sheikh Naser Khamis.

Sluit