Vertaling van de betekenissen Edele Qur'an - Swahili vertaling,Abdallah Mohammed Abubaker en Nassor Khamis Abdarahman * - Index van vertaling


Vertaling van de betekenissen Vers: (8) Surah: Soerat At-Tahriem (Denkende dat iets Verboden is)
يَٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ تُوبُوٓاْ إِلَى ٱللَّهِ تَوۡبَةٗ نَّصُوحًا عَسَىٰ رَبُّكُمۡ أَن يُكَفِّرَ عَنكُمۡ سَيِّـَٔاتِكُمۡ وَيُدۡخِلَكُمۡ جَنَّٰتٖ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُ يَوۡمَ لَا يُخۡزِي ٱللَّهُ ٱلنَّبِيَّ وَٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ مَعَهُۥۖ نُورُهُمۡ يَسۡعَىٰ بَيۡنَ أَيۡدِيهِمۡ وَبِأَيۡمَٰنِهِمۡ يَقُولُونَ رَبَّنَآ أَتۡمِمۡ لَنَا نُورَنَا وَٱغۡفِرۡ لَنَآۖ إِنَّكَ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ قَدِيرٞ
Enyi mliomuamini Mwenyezi Mungu na mtume Wake na mkafuata Sheria Zake kivitendo! Acheni madhambi yenu na mrudi kwenye kumtii Mwenyezi Mungu, kurudi kwa mwisho kusikokuwa na ufanyaji maasia tena kwa kutarajia Mola wenu Awafutie maovu ya matendo yenu na Awaingize kwenye mabustani ya Peponi ambayo chini ya majumba yake ya fahari inapita mito ya maji, Siku ambayo Mwenyezi Mungu Hatamfedhehi Nabii na walioamini pamoja naye wala hatawatesa, bali Atavipandisha juu vyeo vyao. Nuru ya watu hawa itakuwa inatembea mbele yao na kuliani mwao huku wakisema, «Mola wetu! Tukamilishie sisi nuru yetu mpaka tuvuke Ṣirāṭ na tuongoke njia ya kwenda Peponi, na utusamehe na uyatupilie mbali madhambi yetu na uyasitiri, kwani wewe Kwa hakika ni Muweza juu ya kila kitu.»
Arabische uitleg van de Qur'an:
 
Vertaling van de betekenissen Vers: (8) Surah: Soerat At-Tahriem (Denkende dat iets Verboden is)
Surah's Index Pagina nummer
 
Vertaling van de betekenissen Edele Qur'an - Swahili vertaling,Abdallah Mohammed Abubaker en Nassor Khamis Abdarahman - Index van vertaling

De vertaling van de betekenissen van de Heilige Koran naar het Swahili, vertaald door Dr. Abdullah Mohammed Abu Bakr en Sheikh Naser Khamis.

Sluit