Vertaling van de betekenissen Edele Qur'an - Swahili vertaling,Abdallah Mohammed Abubaker en Nassor Khamis Abdarahman * - Index van vertaling


Vertaling van de betekenissen Vers: (100) Surah: Soerat at-Tauba (Berouw)
وَٱلسَّٰبِقُونَ ٱلۡأَوَّلُونَ مِنَ ٱلۡمُهَٰجِرِينَ وَٱلۡأَنصَارِ وَٱلَّذِينَ ٱتَّبَعُوهُم بِإِحۡسَٰنٖ رَّضِيَ ٱللَّهُ عَنۡهُمۡ وَرَضُواْ عَنۡهُ وَأَعَدَّ لَهُمۡ جَنَّٰتٖ تَجۡرِي تَحۡتَهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُ خَٰلِدِينَ فِيهَآ أَبَدٗاۚ ذَٰلِكَ ٱلۡفَوۡزُ ٱلۡعَظِيمُ
Wale waliowatangulia watu mwanzo kwenye kumuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake miongoni mwa Muhājirūn waliowagura watu wao na jamaa zao wakaondoka kwenda kwenye Nyumba ya Uislamu, na Anṣār waliomhami Mtume wa Mwenyezi Mungu, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, dhidi ya maadui wake makafiri, na wale waliowafuata wao kwa wema, katika usawa wa itikadi, maneno na vitendo, kwa kutafuta radhi ya Mwenyezi Mungu, Aliyetakata na sifa pungufu na kutukuka, Hao ndio ambao Mwenyezi Mungu Ameridhika na wao kwa kumtii kwao Mwenyezi Mungu na Mtume Wake, na wao wameridhika na Yeye kwa malipo mazuri mengi Aliyowapatia kwa utiifu wao na Imani yao. Amewaandalia wao mabustani ya Pepo ambayo inapita mito chini yake, hali ya kukaa milele humo daima. Huko ndiko kufaulu kukubwa. Katika aya hii pana kuwasafisha Maswahaba, radhi za Mwenyezi Mungu ziwaendee, kuwafanya waadilifu na kuwasifu. Na kwa hivyo, kuwaheshimu wao ni katika misingi ya Imani.
Arabische uitleg van de Qur'an:
 
Vertaling van de betekenissen Vers: (100) Surah: Soerat at-Tauba (Berouw)
Surah's Index Pagina nummer
 
Vertaling van de betekenissen Edele Qur'an - Swahili vertaling,Abdallah Mohammed Abubaker en Nassor Khamis Abdarahman - Index van vertaling

De vertaling van de betekenissen van de Heilige Koran naar het Swahili, vertaald door Dr. Abdullah Mohammed Abu Bakr en Sheikh Naser Khamis.

Sluit