Vertaling van de betekenissen Edele Qur'an - Kiswahili vertaling - Ali Mohsin Al-Barwani * - Index van vertaling

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Vertaling van de betekenissen Vers: (69) Surah: Soerat De bij (an-Nahl)
ثُمَّ كُلِي مِن كُلِّ ٱلثَّمَرَٰتِ فَٱسۡلُكِي سُبُلَ رَبِّكِ ذُلُلٗاۚ يَخۡرُجُ مِنۢ بُطُونِهَا شَرَابٞ مُّخۡتَلِفٌ أَلۡوَٰنُهُۥ فِيهِ شِفَآءٞ لِّلنَّاسِۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗ لِّقَوۡمٖ يَتَفَكَّرُونَ
Kisha kula katika kila matunda, na upite katika njia za Mola wako Mlezi zilizo fanywa nyepesi kuzipita. Na kutoka matumbo yao kinatoka kinywaji chenye rangi mbali mbali; ndani yake kina matibabu kwa wanaadamu.Hakika katika haya ipo Ishara kwa watu wanao fikiri.
Kisha Subhanahu akamhidi Nyuki ale matunda ya miti na mimea mbali mbali, na akamsahilishia afuate njia alizo mtengezea Mola wake Mlezi, na akatoa kutokana na matumbo yake kinywaji, nacho ni asali, chenye rangi mbali mbali. Na hiyo asali imekuwa ni dawa ya kuwaponyesha watu. Hakika katika hayo pana ufundi wa ajabu wa kuonyesha nguvu, na kuwepo Mwenye kuumba, na Mwenye kuweza, Mwenye hikima. Wenye kutumia akili zao wananufaika kwa mazingatio hayo, na watapata furaha ya daima. Asali ya nyuki ni mchanganyiko wa glucose na livulose, nayo ni namna ya sukari ambayo ni nyepesi kabisa kutumika mwilini, na madaktari wamevumbua karibu kuwa glucose ina faida kutibu maradhi mengi, kwa kupiga sindano, na kwa mdomo na kwa nyuma, kwa kuwa inatia nguvu, na inapinga sumu ya maadeni kadhaa wa kadhaa, na sumu inayo patikana kwa maradhi ya viungo, kama kuingia sumu kwa mkojo na maradhi ya kuwa manjano jaundice na mengineyo. Vile vile imethibiti kuwa Vitamin nyingi hupatikana humo, na khasa Vitamin B complex.
Arabische uitleg van de Qur'an:
 
Vertaling van de betekenissen Vers: (69) Surah: Soerat De bij (an-Nahl)
Surah's Index Pagina nummer
 
Vertaling van de betekenissen Edele Qur'an - Kiswahili vertaling - Ali Mohsin Al-Barwani - Index van vertaling

Vertaling van de betekenissen van de Heilige Koran naar het Swahili, vertaald door Ali Mohsin Al-Barwani.

Sluit