Vertaling van de betekenissen Edele Qur'an - Kiswahili vertaling - Ali Mohsin Al-Barwani * - Index van vertaling

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Vertaling van de betekenissen Vers: (24) Surah: Soerat Al-Ani'jaa (De Profeten)
أَمِ ٱتَّخَذُواْ مِن دُونِهِۦٓ ءَالِهَةٗۖ قُلۡ هَاتُواْ بُرۡهَٰنَكُمۡۖ هَٰذَا ذِكۡرُ مَن مَّعِيَ وَذِكۡرُ مَن قَبۡلِيۚ بَلۡ أَكۡثَرُهُمۡ لَا يَعۡلَمُونَ ٱلۡحَقَّۖ فَهُم مُّعۡرِضُونَ
Au wanawaabudu miungu mingine badala yake? Sema: Leteni ushahidi wenu! Haya ni ukumbusho wa hawa walio nami, na ukumbusho wa walio kabla yangu. Lakini wengi wao hawaijui kweli, na kwa hivyo wanapuuza.
Hawaujui waajibu wa Mwenyezi Mungu uliyo juu yao, ndio maana wakawa na miungu mingine isiyo kuwa Yeye wakaiabudu bila ya kuwa na ushahidi wowote wa kuingia akilini, wala uthibitisho wa kweli. Ewe Nabii! Waambie: Leteni uthibitisho wenu kama kweli Mwenyezi Mungu ana mshirika katika utawala hata akafaa kushirikishwa katika kuabudiwa. Hii Qur'ani iliyo kuja kuukumbusha umati wangu kwa linalo wajibikia, na hivi Vitabu vya Manabii wengine vilivyo kuja kukumbusha kaumu za kabla yangu, vyote hivyo vimesimama juu ya Tawhid, Upweke wa Mwenyezi Mungu. Lakini wengi wao hawajui yaliyo kuja ndani ya Vitabu hivyo, kwa sababu hawajishughulishi kuyazingatia yaliomo humo. Basi wao wamekuwa wenye kuipuuza Imani ya Mwenyezi Mungu.
Arabische uitleg van de Qur'an:
 
Vertaling van de betekenissen Vers: (24) Surah: Soerat Al-Ani'jaa (De Profeten)
Surah's Index Pagina nummer
 
Vertaling van de betekenissen Edele Qur'an - Kiswahili vertaling - Ali Mohsin Al-Barwani - Index van vertaling

Vertaling van de betekenissen van de Heilige Koran naar het Swahili, vertaald door Ali Mohsin Al-Barwani.

Sluit