Check out the new design

Vertaling van de betekenissen Edele Qur'an - De Swahili vertaling - Ali Mohsen Al-Barwani * - Index van vertaling

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Vertaling van de betekenissen Surah: Al-Qasas   Vers:

Al-Qasas

طسٓمٓ
T'A SIN MIM, (T'.S.M.) .
T'a Sin Mim, harufi za kutamkwa kubainisha kuwa Qur'ani hii ni muujiza wa harufi hizi hizi za mazungumzo yenu, na ili kuwazindua wenye kusikia.
Arabische uitleg van de Qur'an:
تِلۡكَ ءَايَٰتُ ٱلۡكِتَٰبِ ٱلۡمُبِينِ
Hizi ni Aya za Kitabu kinacho bainisha.
Ewe Mtume! Aya hizi tunazo kufunulia wewe ni Aya za Qur'ani yenye kubainisha kwa uwazi, yenye kudhihirisha Haki iwe mbali na uwongo, na halali iwe mbali na haramu, na itoe ahadi ya kulipwa thawabu, na kuhadharisha na adhabu.
Arabische uitleg van de Qur'an:
نَتۡلُواْ عَلَيۡكَ مِن نَّبَإِ مُوسَىٰ وَفِرۡعَوۡنَ بِٱلۡحَقِّ لِقَوۡمٖ يُؤۡمِنُونَ
Tunakusomea khabari za Musa na Firauni kwa Haki kwa ajili ya watu wanao amini.
Tunakusimulia baadhi ya khabari za Musa na Firauni kwa ukweli, ili wapate kuzizingatia Waumini.
Arabische uitleg van de Qur'an:
إِنَّ فِرۡعَوۡنَ عَلَا فِي ٱلۡأَرۡضِ وَجَعَلَ أَهۡلَهَا شِيَعٗا يَسۡتَضۡعِفُ طَآئِفَةٗ مِّنۡهُمۡ يُذَبِّحُ أَبۡنَآءَهُمۡ وَيَسۡتَحۡيِۦ نِسَآءَهُمۡۚ إِنَّهُۥ كَانَ مِنَ ٱلۡمُفۡسِدِينَ
Hakika Firauni alitakabari katika nchi, na akawagawa wananchi makundi mbali mbali. Akalidhoofisha taifa moja miongoni mwao, akiwachinja watoto wao wanaume na akiwaacha watoto wao wanawake. Hakika yeye alikuwa katika mafisadi.
Hakika Firauni alipandwa na kiburi, na akapita mipaka katika udhalimu wake, na akatakabari mno katika nchi ya Misri. Akawafanya watu wa nchi hiyo makundi makundi, akiwanyanyua baadhi yao na akiwadhalilisha wenginewe, na khasa aliwadhoofisha Wana wa Israili. Akawa anawachinja watoto wao wanaume na akiwabakisha wanawake. Kwa hakika huyo alikuwa ni katika walio pita hadi katika ujabari na ufisadi.
Arabische uitleg van de Qur'an:
وَنُرِيدُ أَن نَّمُنَّ عَلَى ٱلَّذِينَ ٱسۡتُضۡعِفُواْ فِي ٱلۡأَرۡضِ وَنَجۡعَلَهُمۡ أَئِمَّةٗ وَنَجۡعَلَهُمُ ٱلۡوَٰرِثِينَ
Na tukataka kuwafadhili walio dhoofishwa katika nchi hiyo na kuwafanya wawe waongozi na kuwafanya ni warithi.
Na Mwenyezi Mungu akataka kuwafadhilisha alio wafanya wanyonge Firauni katika nchi, na awafanye ndio wa kuongoza katika njia za kheri, na awarithishe ufalme na madaraka ya nchi.
Arabische uitleg van de Qur'an:
 
Vertaling van de betekenissen Surah: Al-Qasas
Surah's Index Pagina nummer
 
Vertaling van de betekenissen Edele Qur'an - De Swahili vertaling - Ali Mohsen Al-Barwani - Index van vertaling

Vertaald door Ali Mohsen Al-Barwani.

Sluit