Vertaling van de betekenissen Edele Qur'an - Kiswahili vertaling - Ali Mohsin Al-Barwani * - Index van vertaling

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Vertaling van de betekenissen Vers: (94) Surah: Soerat An-nisa (de vrouwen)
يَٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ إِذَا ضَرَبۡتُمۡ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ فَتَبَيَّنُواْ وَلَا تَقُولُواْ لِمَنۡ أَلۡقَىٰٓ إِلَيۡكُمُ ٱلسَّلَٰمَ لَسۡتَ مُؤۡمِنٗا تَبۡتَغُونَ عَرَضَ ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَا فَعِندَ ٱللَّهِ مَغَانِمُ كَثِيرَةٞۚ كَذَٰلِكَ كُنتُم مِّن قَبۡلُ فَمَنَّ ٱللَّهُ عَلَيۡكُمۡ فَتَبَيَّنُوٓاْۚ إِنَّ ٱللَّهَ كَانَ بِمَا تَعۡمَلُونَ خَبِيرٗا
Enyi mlio amini! Mnapo safiri katika Njia ya Mwenyezi Mungu basi hakikisheni, wala msimwambie anaye kutoleeni salamu: Wewe si Muumini; kwa kutaka manufaa ya maisha ya dunia hii, hali ya kuwa kwa Mwenyezi Mungu zipo ghanima nyingi. Hivyo ndivyo mlivyo kuwa nyinyi zamani, na Mwenyezi Mungu akakuneemesheni. Basi chunguzeni sawa sawa. Hakika Mwenyezi Mungu anazo khabari za mnayo yatenda
Kutahadhari msije mkamuuwa Muumini ni waajibu katika wakati wa kwenda vitani. Mkisafiri kwa ajili ya Jihadi ya Njia ya Mwenyezi Mungu jijuvyeni hakika ya hao mnao pigana nao kabla ya kupambana. Je, hao wamesilimu au bado ni washirikina. Wala msimwambie anaye kutoleeni salamu kuwa ni ishara ya amani: Wewe si Muumini, kwa kuwa mnataka kumnyang'anya mali yake na kondoo wake. Bali ipokeeni salamu yake, kwani kwa Mwenyezi Mungu amekuahidini kupata ngawira nyingi nyenginezo. Na nyinyi, enyi Waumini! Mlikuwa hivyo hivyo katika ukafiri kabla ya hayo, na Mwenyezi Mungu amekuhidini. Basi hakikisheni mambo ya hao mnao wakuta. Na Mwenyezi Mungu anajua baraabara, na hapana chochote kinacho fichikana kwake. Na Yeye hakika ni Mwenye kuhisabu kwa mujibu wa ujuzi wake.
Arabische uitleg van de Qur'an:
 
Vertaling van de betekenissen Vers: (94) Surah: Soerat An-nisa (de vrouwen)
Surah's Index Pagina nummer
 
Vertaling van de betekenissen Edele Qur'an - Kiswahili vertaling - Ali Mohsin Al-Barwani - Index van vertaling

Vertaling van de betekenissen van de Heilige Koran naar het Swahili, vertaald door Ali Mohsin Al-Barwani.

Sluit