Check out the new design

ߞߎ߬ߙߣߊ߬ ߞߟߊߒߞߋ ߞߘߐ ߟߎ߬ ߘߟߊߡߌߘߊ - ߛߊߥߊ߯ߤߟߌߞߊ߲ ߘߟߊߡߌ߬ߘߊ - ߊ߳ߺߓߑߘߎ-ߟߟߊ߯ߤߌ߫ ߡߎ߬ߤߊߡߡߊߘߎ߫ ߣߌ߫ ߣߊ߯ߛ߫ߌߙߎ߫ ߞ߭ߊ߬ߡߌ߯ߛߎ߫ ߓߟߏ߫ * - ߘߟߊߡߌߘߊ ߟߎ߫ ߦߌ߬ߘߊ߬ߥߟߊ


ߞߘߐ ߟߎ߬ ߘߟߊߡߌ߬ߘߊ߬ߟߌ ߝߐߘߊ ߘߏ߫: ߌߡߎ߬ߙߊ߲߬ ߞߐߙߍ   ߟߝߊߙߌ ߘߏ߫:
فَٱنقَلَبُواْ بِنِعۡمَةٖ مِّنَ ٱللَّهِ وَفَضۡلٖ لَّمۡ يَمۡسَسۡهُمۡ سُوٓءٞ وَٱتَّبَعُواْ رِضۡوَٰنَ ٱللَّهِۗ وَٱللَّهُ ذُو فَضۡلٍ عَظِيمٍ
Basi wakarudi kutoka Ḥamrā’ al Asad kuja Madina wakiwa wana neema za Mwenyezi Mungu kwa kupata thawabu nyingi na nyongeza za daraja ya juu zitokazo Kwake, huku Imani na yakini zimeongezeka kwao, maadui wa Mwenyezi Mungu wamewadhalilisha, wamefaulu kwa kusalimika na kuuawa na kupigana, na wamefuata mambo ya kumridhisha Mwenyezi Mungu kwa kumtii Yeye na Mtume Wake. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye ihsani na vipawa vingi vyenye kuwaenea wao na wengineo.
ߊߙߊߓߎߞߊ߲ߡߊ ߞߘߐߦߌߘߊ ߟߎ߬:
إِنَّمَا ذَٰلِكُمُ ٱلشَّيۡطَٰنُ يُخَوِّفُ أَوۡلِيَآءَهُۥ فَلَا تَخَافُوهُمۡ وَخَافُونِ إِن كُنتُم مُّؤۡمِنِينَ
Hakika anyewazorotesha nyinyi katika hilo ni Shetani. Amewajia kuwafanya nyinyi muwaogope wasaidizi wake. Basi msiwaogope washirikina, kwani wao ni wanyonge, hakuna mwenye kuwanusuru. Niogopeni mimi kwa kuelekea kwangu kwa utiifu, iwapo nyinyi kweli mnaniamini na mnamfuata Mtume wangu.
ߊߙߊߓߎߞߊ߲ߡߊ ߞߘߐߦߌߘߊ ߟߎ߬:
وَلَا يَحۡزُنكَ ٱلَّذِينَ يُسَٰرِعُونَ فِي ٱلۡكُفۡرِۚ إِنَّهُمۡ لَن يَضُرُّواْ ٱللَّهَ شَيۡـٔٗاۚ يُرِيدُ ٱللَّهُ أَلَّا يَجۡعَلَ لَهُمۡ حَظّٗا فِي ٱلۡأٓخِرَةِۖ وَلَهُمۡ عَذَابٌ عَظِيمٌ
Wasikutie huzuni moyoni mwako hawa makafiri, ewe Mtume, kwa kukimbilia kwao kukanusha na kuingia kwenye upotevu. Hakika wao, kwa hilo, hawatamdhuru Mwenyezi Mungu chochote. Hakika ni kwamba wao wazidhuru nafsi zao kwa kuzinyima utamu wa Imani na thawabu kubwa. Mwenyezi Mungu Anataka Asiwape malipo mema yoyote huko Akhera, kwa kuwa wao wamejiepusha na ulinganizi wa haki. Na wao watapata adhabu kali.
ߊߙߊߓߎߞߊ߲ߡߊ ߞߘߐߦߌߘߊ ߟߎ߬:
إِنَّ ٱلَّذِينَ ٱشۡتَرَوُاْ ٱلۡكُفۡرَ بِٱلۡإِيمَٰنِ لَن يَضُرُّواْ ٱللَّهَ شَيۡـٔٗاۖ وَلَهُمۡ عَذَابٌ أَلِيمٞ
Hakika wale walioibadili Imani kwa kuandama ukafiri, hawatamdhuru Mwenyezi Mungu chochote. Bali madhara ya kitendo chao yatawarudia wenyewe. Na huko Akhera watapata adhabu iumizayo.
ߊߙߊߓߎߞߊ߲ߡߊ ߞߘߐߦߌߘߊ ߟߎ߬:
وَلَا يَحۡسَبَنَّ ٱلَّذِينَ كَفَرُوٓاْ أَنَّمَا نُمۡلِي لَهُمۡ خَيۡرٞ لِّأَنفُسِهِمۡۚ إِنَّمَا نُمۡلِي لَهُمۡ لِيَزۡدَادُوٓاْ إِثۡمٗاۖ وَلَهُمۡ عَذَابٞ مُّهِينٞ
Wala wasidhani wakanushaji kwamba sisi tukiwarefushia umri wao, tukawastarehesha kwa starehe za duniani na tusiwaadhibu kwa ukafiri wao na madhambi yao kwamba watakuwa wamepata heri ya nafsi zao. Hakika tunawacheleweshea adhabu na ajali zao ili wazidishe dhuluma na ukeukaji mipaka. Na watapata adhabu yenye kuwadhalilisha na kuwatweza.
ߊߙߊߓߎߞߊ߲ߡߊ ߞߘߐߦߌߘߊ ߟߎ߬:
مَّا كَانَ ٱللَّهُ لِيَذَرَ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ عَلَىٰ مَآ أَنتُمۡ عَلَيۡهِ حَتَّىٰ يَمِيزَ ٱلۡخَبِيثَ مِنَ ٱلطَّيِّبِۗ وَمَا كَانَ ٱللَّهُ لِيُطۡلِعَكُمۡ عَلَى ٱلۡغَيۡبِ وَلَٰكِنَّ ٱللَّهَ يَجۡتَبِي مِن رُّسُلِهِۦ مَن يَشَآءُۖ فَـَٔامِنُواْ بِٱللَّهِ وَرُسُلِهِۦۚ وَإِن تُؤۡمِنُواْ وَتَتَّقُواْ فَلَكُمۡ أَجۡرٌ عَظِيمٞ
Hakuwa Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuwaacha , enyi wenye kumuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na wenye kuzifuata Sheria Yake kivitendo, juu ya hivyo mlivyo ya kuchanganyikana mwenye Imani na mnafiki, mpaka Ampambanue muovu na mwema, ili ajulikune mnafiki na Muumini mkweli. Na haikuwa ni katika hekima ya Mwenyezi Mungu, enyi Waumini, kwamba Atawafunulia ghaibu Anayoijua kuhusu waja Wake, mkamjua Muumini kati yao na mnafiki. Lakini Yeye Anawapambanua kwa misukosuko na mitihani. Isipokuwa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, Anamteua Amtakaye katika wajumbe Wake ili kumuonesha ujuzi wa ghaibu kwa wahyi utokao Kwake. Basi muaminini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake. Na iwapo mtaamini, imani ya kweli, na mkamuogopa Mola wenu kwa kumtii, mtapata malipo makubwa mbele ya Mwenyezi Mungu.
ߊߙߊߓߎߞߊ߲ߡߊ ߞߘߐߦߌߘߊ ߟߎ߬:
وَلَا يَحۡسَبَنَّ ٱلَّذِينَ يَبۡخَلُونَ بِمَآ ءَاتَىٰهُمُ ٱللَّهُ مِن فَضۡلِهِۦ هُوَ خَيۡرٗا لَّهُمۖ بَلۡ هُوَ شَرّٞ لَّهُمۡۖ سَيُطَوَّقُونَ مَا بَخِلُواْ بِهِۦ يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِۗ وَلِلَّهِ مِيرَٰثُ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِۗ وَٱللَّهُ بِمَا تَعۡمَلُونَ خَبِيرٞ
Wala wasidhani wale wanaozifanyia ubakhili neema za Mwenyezi Mungu Alizowaneemesha kwa kuwafadhili kwamba ubakhili huo ni bora kwao. Bali hiyo ni shari kwao. Kwani mali hayo waliyoyakusanya yatakuwa ni kitanzi cha moto kitakachowekwa shingoni mwao Siku ya Kiyama. Na Mwenyezi Mungu, Aliyetakasika na kutukuka, Ndiye Mwenye kumiliki ufalme ; na Yeye Ndiye Atakayesalia baada ya kutoweka viumbe Wake wote. Yeye Ndiye Mtambuzi wa matendo yenu yote, na Atamlipa kila mtu kwa kadiri anayostahiki.
ߊߙߊߓߎߞߊ߲ߡߊ ߞߘߐߦߌߘߊ ߟߎ߬:
 
ߞߘߐ ߟߎ߬ ߘߟߊߡߌ߬ߘߊ߬ߟߌ ߝߐߘߊ ߘߏ߫: ߌߡߎ߬ߙߊ߲߬ ߞߐߙߍ
ߝߐߘߊ ߟߎ߫ ߦߌ߬ߘߊ߬ߥߟߊ ߞߐߜߍ ߝߙߍߕߍ
 
ߞߎ߬ߙߣߊ߬ ߞߟߊߒߞߋ ߞߘߐ ߟߎ߬ ߘߟߊߡߌߘߊ - ߛߊߥߊ߯ߤߟߌߞߊ߲ ߘߟߊߡߌ߬ߘߊ - ߊ߳ߺߓߑߘߎ-ߟߟߊ߯ߤߌ߫ ߡߎ߬ߤߊߡߡߊߘߎ߫ ߣߌ߫ ߣߊ߯ߛ߫ߌߙߎ߫ ߞ߭ߊ߬ߡߌ߯ߛߎ߫ ߓߟߏ߫ - ߘߟߊߡߌߘߊ ߟߎ߫ ߦߌ߬ߘߊ߬ߥߟߊ

ߞߓ. ߊ߳ߺߊߓߑߘߎ߫ ߊߑߟߟߊ߯ߤߌ߫ ߡߎ߬ߤ߭ߊߡߡߊߘߎ߫ ߊ߬ߓߎ߰-ߓߊߞߙߌ߫ ߣߌ߫ ߗߍ߬ߡߐ߯ ߣߊ߯ߛ߫ߌߙߎ߫ ߞ߭ߊߡߌ߯ߛ ߟߊ߫ ߘߟߊߡߌߘߊߟߌ ߟߋ߬.

ߘߊߕߎ߲߯ߠߌ߲