Check out the new design

ߞߎ߬ߙߣߊ߬ ߞߟߊߒߞߋ ߞߘߐ ߟߎ߬ ߘߟߊߡߌߘߊ - ߛߊߥߊ߯ߤߟߌߞߊ߲ ߘߟߊߡߌ߬ߘߊ - ߊ߳ߺߓߑߘߎ-ߟߟߊ߯ߤߌ߫ ߡߎ߬ߤߊߡߡߊߘߎ߫ ߣߌ߫ ߣߊ߯ߛ߫ߌߙߎ߫ ߞ߭ߊ߬ߡߌ߯ߛߎ߫ ߓߟߏ߫ * - ߘߟߊߡߌߘߊ ߟߎ߫ ߦߌ߬ߘߊ߬ߥߟߊ


ߞߘߐ ߟߎ߬ ߘߟߊߡߌ߬ߘߊ߬ߟߌ ߝߐߘߊ ߘߏ߫: ߌߡߎ߬ߙߊ߲߬ ߞߐߙߍ   ߟߝߊߙߌ ߘߏ߫:
وَيُكَلِّمُ ٱلنَّاسَ فِي ٱلۡمَهۡدِ وَكَهۡلٗا وَمِنَ ٱلصَّٰلِحِينَ
Na atasema na watu na hali yeye ni mtoto mchanga wa kunyonya kabla hajafikia wakati wa kusema. Na atawaita wao kwa Mwenyezi Mungu, akiwa mkubwa wakati ambapo nguvu zake zitakuwa zimeshikana na ubarobaro wake umekamilika, kwa yale aliyoletewa wahyi na Mwenyezi Mungu. Kusema huku ni kuhusu utume, ulinganizi na uongozi. Na yeye anahesabiwa kuwa ni mmoja wa watu wema na wenye utukufu wa maneno na vitendo.
ߊߙߊߓߎߞߊ߲ߡߊ ߞߘߐߦߌߘߊ ߟߎ߬:
قَالَتۡ رَبِّ أَنَّىٰ يَكُونُ لِي وَلَدٞ وَلَمۡ يَمۡسَسۡنِي بَشَرٞۖ قَالَ كَذَٰلِكِ ٱللَّهُ يَخۡلُقُ مَا يَشَآءُۚ إِذَا قَضَىٰٓ أَمۡرٗا فَإِنَّمَا يَقُولُ لَهُۥ كُن فَيَكُونُ
Maryam alisema kwa kustaajabu, «Vipi mimi nitakuwa na mtoto na sina mume wala si malaya?» Malaika akamuambia, «Tukio hili kwako si jambo lililo mbali kwa Mwenyezi Mungu Muweza Ambaye Anakipatisha chochote anachokitaka kutokana na kisichokuweko. Akitaka kitu chochote kipatikane Anakiambia, «Kuwa,» nacho kikawa.
ߊߙߊߓߎߞߊ߲ߡߊ ߞߘߐߦߌߘߊ ߟߎ߬:
وَيُعَلِّمُهُ ٱلۡكِتَٰبَ وَٱلۡحِكۡمَةَ وَٱلتَّوۡرَىٰةَ وَٱلۡإِنجِيلَ
Na Atamfundisha kuandika, njia ya kuufikia usawa katika kusema na kutenda, Taurati ambayo Mwenyezi Mungu Alimletea Musa, amani imshukie, kwa njia ya wahyi, na Injili ambayo Mwenyezi Mungu Alimteremshia yeye.
ߊߙߊߓߎߞߊ߲ߡߊ ߞߘߐߦߌߘߊ ߟߎ߬:
وَرَسُولًا إِلَىٰ بَنِيٓ إِسۡرَٰٓءِيلَ أَنِّي قَدۡ جِئۡتُكُم بِـَٔايَةٖ مِّن رَّبِّكُمۡ أَنِّيٓ أَخۡلُقُ لَكُم مِّنَ ٱلطِّينِ كَهَيۡـَٔةِ ٱلطَّيۡرِ فَأَنفُخُ فِيهِ فَيَكُونُ طَيۡرَۢا بِإِذۡنِ ٱللَّهِۖ وَأُبۡرِئُ ٱلۡأَكۡمَهَ وَٱلۡأَبۡرَصَ وَأُحۡيِ ٱلۡمَوۡتَىٰ بِإِذۡنِ ٱللَّهِۖ وَأُنَبِّئُكُم بِمَا تَأۡكُلُونَ وَمَا تَدَّخِرُونَ فِي بُيُوتِكُمۡۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗ لَّكُمۡ إِن كُنتُم مُّؤۡمِنِينَ
Na Atamjaalia awe Mtume kwa Wana wa Isrāīl na atawaambia wao, «Mimi nimewajia na alama kutoka kwa Mola wenu inayoonesha kuwa mimi nimetumilizwa kutoka kwa Mwenyezi Mungu. Nayo ni kuwa nitawafanyia kwa udongo kitu chenye mfano wa ndege, nitapuliza ndani yake na kitakuwa ndege wa kikweli kwa idhini ya Mwenyezi Mungu. Na nitamponya aliyezaliwa kipofu na mwenye barasi na nitamhuisha aliyekufa kwa idhini ya Mwenyezi Mungu. Na nitawaambia chakula mnachokula na mnachoweka akiba majumbani mwenu. Hakika katika mambo makubwa haya, ambayo hayako kwenye uwezo wa wanaadamu, pana dalili kwamba mimi ni Nabii wa Mwenyezi Mungu na Mtume Wake, iwapo nyinyi ni wenye kuamini hoja za Mwenyezi Mungu na alama Zake, ni wenye kukiri kumpwekesha.
ߊߙߊߓߎߞߊ߲ߡߊ ߞߘߐߦߌߘߊ ߟߎ߬:
وَمُصَدِّقٗا لِّمَا بَيۡنَ يَدَيَّ مِنَ ٱلتَّوۡرَىٰةِ وَلِأُحِلَّ لَكُم بَعۡضَ ٱلَّذِي حُرِّمَ عَلَيۡكُمۡۚ وَجِئۡتُكُم بِـَٔايَةٖ مِّن رَّبِّكُمۡ فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
«Na nimewajia nyinyi kuyasadikisha yaliyomo ndani ya Taurati, na ili niawahalalishie, kwa wahyi unaotoka kwa Mwenyezi Mungu, baadhi ya yale ambayo Mwenyezi Mungu Aliwaharamishia, yakiwa ni usahilishaji na huruma kutoka kwa Mwenyezi Mungu, na nimewajia na hoja kutoka kwa Mola wenu ya ukweli wa ninayowaambia. Basi Mcheni Mwenyezi Mungu na msiende kinyume na amri Yake na mnitii mimi katika yale ninayowafikishia kutoka kwa Mwenyezi Mungu.
ߊߙߊߓߎߞߊ߲ߡߊ ߞߘߐߦߌߘߊ ߟߎ߬:
إِنَّ ٱللَّهَ رَبِّي وَرَبُّكُمۡ فَٱعۡبُدُوهُۚ هَٰذَا صِرَٰطٞ مُّسۡتَقِيمٞ
«Hakika Mwenyezi Mungu Ambaye ninawalingania nyinyi Kwake Ndiye Peke Yake Mola wangu na Mola wenu, basi muabuduni Yeye. Mimi na nyinyi tuko sawa katika uja wetu na unyenyekevu wetu Kwake. Na hii ndio njia ambayo haina mpeteko.»
ߊߙߊߓߎߞߊ߲ߡߊ ߞߘߐߦߌߘߊ ߟߎ߬:
۞ فَلَمَّآ أَحَسَّ عِيسَىٰ مِنۡهُمُ ٱلۡكُفۡرَ قَالَ مَنۡ أَنصَارِيٓ إِلَى ٱللَّهِۖ قَالَ ٱلۡحَوَارِيُّونَ نَحۡنُ أَنصَارُ ٱللَّهِ ءَامَنَّا بِٱللَّهِ وَٱشۡهَدۡ بِأَنَّا مُسۡلِمُونَ
Alipohisi 'Īsā kutoka kwao ukakamavu juu ya ukafuri, aliita kwa watu wake halisi kwa kusema, «Ni nani atakayekuwa na mimi katika kuinusuru dini ya Mwenyezi Mungu.» Wale wasafiwa wa 'Īsā walisema, «Sisi ni wenye kuinusuru dini ya Mwenyezi Mungu na wenye kuilingania, tumemuamini Mwenyezi Mungu na tumekufuata; na ushuhudie, ewe 'Īsā, kuwa sisi tumejisalimisha kwa Mwenyezi Mungu kwa kumpwekesha na kumtii.
ߊߙߊߓߎߞߊ߲ߡߊ ߞߘߐߦߌߘߊ ߟߎ߬:
 
ߞߘߐ ߟߎ߬ ߘߟߊߡߌ߬ߘߊ߬ߟߌ ߝߐߘߊ ߘߏ߫: ߌߡߎ߬ߙߊ߲߬ ߞߐߙߍ
ߝߐߘߊ ߟߎ߫ ߦߌ߬ߘߊ߬ߥߟߊ ߞߐߜߍ ߝߙߍߕߍ
 
ߞߎ߬ߙߣߊ߬ ߞߟߊߒߞߋ ߞߘߐ ߟߎ߬ ߘߟߊߡߌߘߊ - ߛߊߥߊ߯ߤߟߌߞߊ߲ ߘߟߊߡߌ߬ߘߊ - ߊ߳ߺߓߑߘߎ-ߟߟߊ߯ߤߌ߫ ߡߎ߬ߤߊߡߡߊߘߎ߫ ߣߌ߫ ߣߊ߯ߛ߫ߌߙߎ߫ ߞ߭ߊ߬ߡߌ߯ߛߎ߫ ߓߟߏ߫ - ߘߟߊߡߌߘߊ ߟߎ߫ ߦߌ߬ߘߊ߬ߥߟߊ

ߞߓ. ߊ߳ߺߊߓߑߘߎ߫ ߊߑߟߟߊ߯ߤߌ߫ ߡߎ߬ߤ߭ߊߡߡߊߘߎ߫ ߊ߬ߓߎ߰-ߓߊߞߙߌ߫ ߣߌ߫ ߗߍ߬ߡߐ߯ ߣߊ߯ߛ߫ߌߙߎ߫ ߞ߭ߊߡߌ߯ߛ ߟߊ߫ ߘߟߊߡߌߘߊߟߌ ߟߋ߬.

ߘߊߕߎ߲߯ߠߌ߲