د قرآن کریم د معناګانو ژباړه - سواحلي ژباړه - عبد الله محمد او ناصر خمیس * - د ژباړو فهرست (لړلیک)


د معناګانو ژباړه آیت: (24) سورت: يونس
إِنَّمَا مَثَلُ ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَا كَمَآءٍ أَنزَلۡنَٰهُ مِنَ ٱلسَّمَآءِ فَٱخۡتَلَطَ بِهِۦ نَبَاتُ ٱلۡأَرۡضِ مِمَّا يَأۡكُلُ ٱلنَّاسُ وَٱلۡأَنۡعَٰمُ حَتَّىٰٓ إِذَآ أَخَذَتِ ٱلۡأَرۡضُ زُخۡرُفَهَا وَٱزَّيَّنَتۡ وَظَنَّ أَهۡلُهَآ أَنَّهُمۡ قَٰدِرُونَ عَلَيۡهَآ أَتَىٰهَآ أَمۡرُنَا لَيۡلًا أَوۡ نَهَارٗا فَجَعَلۡنَٰهَا حَصِيدٗا كَأَن لَّمۡ تَغۡنَ بِٱلۡأَمۡسِۚ كَذَٰلِكَ نُفَصِّلُ ٱلۡأٓيَٰتِ لِقَوۡمٖ يَتَفَكَّرُونَ
Hakika mfano wa uhai wa kilimwengu na yale mnayojifahiri nayo baina yenu ya mapambo na mali ni kama mfano wa mvua tulioiteremsha kutoka juu kushuka ardhini, tukaotesha kwayo aina za mimea zilizochanganyika miongoni mwa zile zinazoliwa na watu katika matunda na zinazoliwa na wanyama katika nyasi, mpaka ulipoonekana wazi uzuri wa hii ardhi na mng’aro wake, na watu wa ardhi hii wakadhani kwamba wao ni waweza wa kuyavuna na kufaidika nayo, hapo amri yetu na hukumu yetu iliyajia kuwa ile mimea iliyoko juu yake iangamie na uzuri wake uondoke, kipindi cha usiku au mchana, tukaifanya mimea hii na miti imevunwa imekatwa, hakuna kitu katika ardhi hiyo, kama kwamba hapakuwa na mazao na mimea iliokuwa imesimama kabla ya hapo juu ya uso wa ardhi. Hivyo ndivyo kutoweka kunakomaliza yale mnayojigamba nayo baina yenu ya ulimwengu wenu na pambo lake, Mwenyezi Mungu Akayamaliza na kuyaangamiza. Na kama tulivyowafafanulia, enyi watu, mfano wa ulimwengu huu, na tukawajulisha uhakika wake, ndivyo tunavyofafanua hoja zetu na dalili zetu kwa watu wanaofikiri juu ya aya za Mwenyezi Mungu na wanaozingatia yanayowafaa duniani na Akhera.
عربي تفسیرونه:
 
د معناګانو ژباړه آیت: (24) سورت: يونس
د سورتونو فهرست (لړلیک) د مخ نمبر
 
د قرآن کریم د معناګانو ژباړه - سواحلي ژباړه - عبد الله محمد او ناصر خمیس - د ژباړو فهرست (لړلیک)

په سواهیلي ژبه کې د قرآن کریم د معناګانو ژباړه، د ډاکټر عبدالله محمد ابوبکر او شیخ ناصر خمیس لخوا ژباړل شوی.

بندول