د قرآن کریم د معناګانو ژباړه - سواحلي ژباړه - عبد الله محمد او ناصر خمیس * - د ژباړو فهرست (لړلیک)


د معناګانو ژباړه آیت: (56) سورت: الأحزاب
إِنَّ ٱللَّهَ وَمَلَٰٓئِكَتَهُۥ يُصَلُّونَ عَلَى ٱلنَّبِيِّۚ يَٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ صَلُّواْ عَلَيۡهِ وَسَلِّمُواْ تَسۡلِيمًا
Hakika Mwenyezi Mungu Anamsifu Nabii, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, mbele ya Malaika waliokurubishwa. Na Malaika Wake wanamsifu Nabii na wanamuombea Mwenyezi Mungu, basi enyi mliomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na mkazifuata sheria Zake kivitendo, mswalieni Mtume wa Mwenyezi Mungu na mtakieni amani, kwa kumwamkia na kumtukuza. Na namna ya kumswalia Nabii, rehema na amani zimshukie, imethibiti kwenye Sunnah kwa aina mabalimbali, miongoni mwazo ni: «Ewe Mola! Mrehemu Muhammad na watu wa Muhammad, kama ulivyowarehemu watu wa Ibrāhīm, hakika wewe ni Mwingi wa kushukuriwa ni Mwingi wa kutukuzwa. Ewe Mola! Mbariki Muhammad na watu wa Muhammad kama ulivyowabariki watu wa Ibrāhīm, hakika wewe ni Mwingi wa kushukuriwa, ni Mwingi wa kutukuzwa.»
عربي تفسیرونه:
 
د معناګانو ژباړه آیت: (56) سورت: الأحزاب
د سورتونو فهرست (لړلیک) د مخ نمبر
 
د قرآن کریم د معناګانو ژباړه - سواحلي ژباړه - عبد الله محمد او ناصر خمیس - د ژباړو فهرست (لړلیک)

په سواهیلي ژبه کې د قرآن کریم د معناګانو ژباړه، د ډاکټر عبدالله محمد ابوبکر او شیخ ناصر خمیس لخوا ژباړل شوی.

بندول