د قرآن کریم د معناګانو ژباړه - سواحلي ژباړه - عبد الله محمد او ناصر خمیس * - د ژباړو فهرست (لړلیک)


د معناګانو ژباړه آیت: (6) سورت: الأنعام
أَلَمۡ يَرَوۡاْ كَمۡ أَهۡلَكۡنَا مِن قَبۡلِهِم مِّن قَرۡنٖ مَّكَّنَّٰهُمۡ فِي ٱلۡأَرۡضِ مَا لَمۡ نُمَكِّن لَّكُمۡ وَأَرۡسَلۡنَا ٱلسَّمَآءَ عَلَيۡهِم مِّدۡرَارٗا وَجَعَلۡنَا ٱلۡأَنۡهَٰرَ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهِمۡ فَأَهۡلَكۡنَٰهُم بِذُنُوبِهِمۡ وَأَنشَأۡنَا مِنۢ بَعۡدِهِمۡ قَرۡنًا ءَاخَرِينَ
Kwani hawayajui, hawa wanaoukanusha upweke wa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, na kustahiki Kwake, Peke Yake, kuabudiwa na wanaomkanusha Mtume Wake Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie,, yale yaliyowashukia watu waliokanusha kabla yao ya maangamivu na uharibifu? Hao tuliwapa utulivu kwenye ardhi kwa namna ambayo hatukuwapa nyinyi, enyi makafiri, utulivu kama huo na tuliwaneemesha kwa kuwateremshia mivua na kupita mito chini ya makao yao kwa njia ya kuwanyoshea na kuwapa muhula, wakazikanusha neema za Mwenyezi Mungu na wakawakanusha Mitume. Hapo tuliwaangamiza kwa sababu ya madhambi yao na tukawaumba baada yao watu wengine walioshika nafasi zao katika kuiamirisha ardhi.
عربي تفسیرونه:
 
د معناګانو ژباړه آیت: (6) سورت: الأنعام
د سورتونو فهرست (لړلیک) د مخ نمبر
 
د قرآن کریم د معناګانو ژباړه - سواحلي ژباړه - عبد الله محمد او ناصر خمیس - د ژباړو فهرست (لړلیک)

په سواهیلي ژبه کې د قرآن کریم د معناګانو ژباړه، د ډاکټر عبدالله محمد ابوبکر او شیخ ناصر خمیس لخوا ژباړل شوی.

بندول