Check out the new design

د قرآن کریم د معناګانو ژباړه - سواحلي ژباړه - عبد الله محمد او ناصر خمیس * - د ژباړو فهرست (لړلیک)


د معناګانو ژباړه سورت: مدثر   آیت:
فَقُتِلَ كَيۡفَ قَدَّرَ
Hivyo basi akalaaniwa na akastahili, kwa hilo, maangamivu: alijiandaa vipi ndani ya nafsi yake kwa hayo matukano?
عربي تفسیرونه:
ثُمَّ قُتِلَ كَيۡفَ قَدَّرَ
Kisha pia akalaaniwa.
عربي تفسیرونه:
ثُمَّ نَظَرَ
Kisha yeye alifikiria kuhusu kile alichokipanga na kukitayarisha cha kuitia dosari Qur’ani.
عربي تفسیرونه:
ثُمَّ عَبَسَ وَبَسَرَ
Kisha akafinya uso wake na akazidi katika hali ile ya ukunjaji uso kwa kukosa hila za kufanya na kutopata ila yoyote ya kuitia dosari Qur’ani.
عربي تفسیرونه:
ثُمَّ أَدۡبَرَ وَٱسۡتَكۡبَرَ
Kisha akarudi kuipa mgongo haki na akajiona ni mkubwa wa kutofaa kuikubali,
عربي تفسیرونه:
فَقَالَ إِنۡ هَٰذَآ إِلَّا سِحۡرٞ يُؤۡثَرُ
hapo akasema kuhusu Qur’ani, «Haya anayoyasema Muhammad si chochote isipokuwa ni uchawi uliopokewa kutoka kwa watu wa mwanzo waliopita.
عربي تفسیرونه:
إِنۡ هَٰذَآ إِلَّا قَوۡلُ ٱلۡبَشَرِ
Haikuwa hi Qur’ani isipokuwa ni maneno ya viumbe ambayo Muhammad amejifunza kutoka kwao kisha akadai kuwa yanatoka kwa Mwenyezi Mungu.»
عربي تفسیرونه:
سَأُصۡلِيهِ سَقَرَ
Basi nitamuingiza kwenye moto wa Jahanamu ili alionje joto lake na achomeke kwa moto wake.
عربي تفسیرونه:
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا سَقَرُ
Na ni lipi lililokujulisha wewe ni kitu gani hiyo Jahanamu?
عربي تفسیرونه:
لَا تُبۡقِي وَلَا تَذَرُ
Haibakishi nyama wala haiachi mfupa isipokuwa huvichoma.
عربي تفسیرونه:
لَوَّاحَةٞ لِّلۡبَشَرِ
Unageuza ngozi ya mwili, unazifanya ngozi kuwa nyeusi na unazichoma.
عربي تفسیرونه:
عَلَيۡهَا تِسۡعَةَ عَشَرَ
Wanasimamia mambo yake na kushikilia kazi ya kuwatesa watu wake Malaika kumi na tisa katika washika zamu wa Motoni wenye nguvu.
عربي تفسیرونه:
وَمَا جَعَلۡنَآ أَصۡحَٰبَ ٱلنَّارِ إِلَّا مَلَٰٓئِكَةٗۖ وَمَا جَعَلۡنَا عِدَّتَهُمۡ إِلَّا فِتۡنَةٗ لِّلَّذِينَ كَفَرُواْ لِيَسۡتَيۡقِنَ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ وَيَزۡدَادَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ إِيمَٰنٗا وَلَا يَرۡتَابَ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ وَٱلۡمُؤۡمِنُونَ وَلِيَقُولَ ٱلَّذِينَ فِي قُلُوبِهِم مَّرَضٞ وَٱلۡكَٰفِرُونَ مَاذَآ أَرَادَ ٱللَّهُ بِهَٰذَا مَثَلٗاۚ كَذَٰلِكَ يُضِلُّ ٱللَّهُ مَن يَشَآءُ وَيَهۡدِي مَن يَشَآءُۚ وَمَا يَعۡلَمُ جُنُودَ رَبِّكَ إِلَّا هُوَۚ وَمَا هِيَ إِلَّا ذِكۡرَىٰ لِلۡبَشَرِ
Na hatukuwafanya washika hazina wa Motoni isipokuwa miongoni mwa Malaika washupavu. Na hatukuiweka idadi hiyo isipokuwa kuwatahini wale waliomkufuru Mwenyezi Mungu, na ili imani ya yakini ipatikane kwa wale Mayahudi na Wanaswara waliopewa Vitabu kwamba yaliyokuja ndani ya Qur’ani juu ya washika hazina wa Motoni ni ukweli utokao kwa Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, kwani hayo yanaafikiana na vitabu vyao, na ili Waumini wazidi kumuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na waifuate Sheria Yake kivitendo, na ili wasilifanyie shaka hilo wale Mayahudi na Wanaswara waliopewa Vitabu wala wale wenye kumuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake, na ili wapate kusema wale wenye unafiki ndani ya nyoyo zao na makafiri, «Ni lipi alilolikusudia Mwenyezi Mungu kwa idadi hii ya ajabu?» Kwa mfano wa hayo yaliyotajwa, Mwenyezi Mungu Anampoteza Anayetaka kumpoteza na Anamuongoza Anayetaka kumuongoza. Na hakuna ajuwaye idadi ya askari wa Mola wako, na miongoni mwao ni Malaika, isipokuwa Mwenyezi Mungu Peke Yake. Na haukuwa huu Moto isipokuwa ni ukumbusho na mazingatio kwa watu.
عربي تفسیرونه:
كَلَّا وَٱلۡقَمَرِ
Mambo sivyo kama walivyotaja ya ukanushaji Mtume katika yale aliyokuja nayo! Anaapa Mwenyezi Mungu, Aliyetakasika na kila sifa ya upungufu, kwa mwezi,
عربي تفسیرونه:
وَٱلَّيۡلِ إِذۡ أَدۡبَرَ
na kwa usiku unapogeuka kwenda zake,
عربي تفسیرونه:
وَٱلصُّبۡحِ إِذَآ أَسۡفَرَ
na kwa asubuhi inapotoa mwangaza na kufunuka,
عربي تفسیرونه:
إِنَّهَا لَإِحۡدَى ٱلۡكُبَرِ
hakika Moto ni mojawapo ya mambo makubwa,
عربي تفسیرونه:
نَذِيرٗا لِّلۡبَشَرِ
kwa ajili ya kuwaonya na kuwatisha watu,
عربي تفسیرونه:
لِمَن شَآءَ مِنكُمۡ أَن يَتَقَدَّمَ أَوۡ يَتَأَخَّرَ
kwa anayetaka miongoni mwenu kujiweka karibu na Mola wake kwa kufanya matendo ya utiifu, au kujikalisha nyuma kwa kufanya matendo ya uasi.
عربي تفسیرونه:
كُلُّ نَفۡسِۭ بِمَا كَسَبَتۡ رَهِينَةٌ
Kila nafsi imefungwa na kuwekwa rahani kwa ilichokitenda, miongoni mwa matendo mema au mabaya, kwa kukichuma. Haifunguliwi mpaka itekeleze haki zilizo juu ya lazima yake na ipatiwe mateso yanayostahili kupatiwa.
عربي تفسیرونه:
إِلَّآ أَصۡحَٰبَ ٱلۡيَمِينِ
Isipokuwa Waislamu waliotakaswa, watu wa upande wa kulia waliojikomboa shingo zao kwa utiifu.
عربي تفسیرونه:
فِي جَنَّٰتٖ يَتَسَآءَلُونَ
Wao watakuwa kwenye mabustani ya Peponi ambayo sifa zake hazifikiwi ukomo. Watakuwa wakiulizana wao kwa wao
عربي تفسیرونه:
عَنِ ٱلۡمُجۡرِمِينَ
kuhusu makafiri waliojikosea nafsi zao,
عربي تفسیرونه:
مَا سَلَكَكُمۡ فِي سَقَرَ
«Ni lipi lililowaingiza kwenye moto wa Jahanamu na likawafanya
عربي تفسیرونه:
قَالُواْ لَمۡ نَكُ مِنَ ٱلۡمُصَلِّينَ
mlionje joto lake lililo kali sana?» Wahalifu waseme , «Hatukuwa ni miongoni mwa wanaoswali duniani,
عربي تفسیرونه:
وَلَمۡ نَكُ نُطۡعِمُ ٱلۡمِسۡكِينَ
na hatukuwa tukitoa sadaka na kuwafanyia wema wahitaji na maskini,
عربي تفسیرونه:
وَكُنَّا نَخُوضُ مَعَ ٱلۡخَآئِضِينَ
na tulikuwa tukizungumza maneno ya ubatilifu na watu wa upotofu na upotevu,
عربي تفسیرونه:
وَكُنَّا نُكَذِّبُ بِيَوۡمِ ٱلدِّينِ
na tulikuwa tukiikanusha Siku ya kuhesabiwa na kulipwa,
عربي تفسیرونه:
حَتَّىٰٓ أَتَىٰنَا ٱلۡيَقِينُ
mpaka kifo kikatujia na hali sisi tuko kwenye mambo hayo mabaya ya upotevu.
عربي تفسیرونه:
 
د معناګانو ژباړه سورت: مدثر
د سورتونو فهرست (لړلیک) د مخ نمبر
 
د قرآن کریم د معناګانو ژباړه - سواحلي ژباړه - عبد الله محمد او ناصر خمیس - د ژباړو فهرست (لړلیک)

ژباړوونکي: ډاکټر عبدالله محمد ابوبکر او شیخ ناصر خمیس.

بندول