د قرآن کریم د معناګانو ژباړه - سواحلي ژباړه - علی محسن البرواني * - د ژباړو فهرست (لړلیک)

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

د معناګانو ژباړه آیت: (220) سورت: البقرة
فِي ٱلدُّنۡيَا وَٱلۡأٓخِرَةِۗ وَيَسۡـَٔلُونَكَ عَنِ ٱلۡيَتَٰمَىٰۖ قُلۡ إِصۡلَاحٞ لَّهُمۡ خَيۡرٞۖ وَإِن تُخَالِطُوهُمۡ فَإِخۡوَٰنُكُمۡۚ وَٱللَّهُ يَعۡلَمُ ٱلۡمُفۡسِدَ مِنَ ٱلۡمُصۡلِحِۚ وَلَوۡ شَآءَ ٱللَّهُ لَأَعۡنَتَكُمۡۚ إِنَّ ٱللَّهَ عَزِيزٌ حَكِيمٞ
--Katika mambo ya dunia na mambo ya Akhera. Na wanakuuliza juu ya mayatima. Sema: Kuwatengenezea ndio kheri. Na mkichanganyika nao basi ni ndugu zenu; na Mwenyezi Mungu anamjua mharibifu na mtengenezaji. Na Mwenyezi Mungu angeli penda angeli kutieni katika udhia. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu na Mwenye hikima.
Na wanakuuliza khabari ya mayatima: katika Uislamu inapasa watendejwe? Sema ni kheri yenu na yao kuwatendea wema. Wawekeni katika nyumba zenu pamoja nanyi, na changanyikeni nao kwa makusudio ya kheri si ya fisadi, kwani wao ni ndugu zenu duniani, wanahitaji kwenu mchanganyiko huu. Na Mwenyezi Mungu anamjua mharibifu na mtengenezaji katika nyinyi. Basi tahadharini! Na Mwenyezi Mungu angeli penda angeli kupeni taabu, akakulazimisheni kuwaangalia mayatima bila ya kuchanganyika nao, au angeli kuacheni bila ya kubainisha waajibu wanao pasa kutendewa. Kwa hivyo wangeli kulia kuchukia watu, na hayo yange pelekea kufisidika na kuleta shida kwa jamii zenu. Kwani kuwakahirisha mayatima na kuwadhili huwafanya wawachukie hao jamaa wawatendao vibaya. Na hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu na Mwenye kushinda katika amri yake, lakini naye ni Mwenye hikima halazimishi katika sharia ila lenye maslaha yenu.
عربي تفسیرونه:
 
د معناګانو ژباړه آیت: (220) سورت: البقرة
د سورتونو فهرست (لړلیک) د مخ نمبر
 
د قرآن کریم د معناګانو ژباړه - سواحلي ژباړه - علی محسن البرواني - د ژباړو فهرست (لړلیک)

سواحلې ژبې ته د قرآن کریم د معناګانو ژباړه، علی محسن البرواني ژباړلې ده

بندول