Check out the new design

د قرآن کریم د معناګانو ژباړه - سواحلي ژباړه - علی محسن البرواني * - د ژباړو فهرست (لړلیک)

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

د معناګانو ژباړه سورت: آل عمران   آیت:
إِذۡ هَمَّت طَّآئِفَتَانِ مِنكُمۡ أَن تَفۡشَلَا وَٱللَّهُ وَلِيُّهُمَاۗ وَعَلَى ٱللَّهِ فَلۡيَتَوَكَّلِ ٱلۡمُؤۡمِنُونَ
Makundi mawili miongoni mwenu yakaingiwa na woga kuwa watashindwa - na hali Mwenyezi Mungu ndiye Mlinzi wao; na Waumini wamtegemee Mwenyezi Mungu tu.
Ilipo tokea kuwa vikundi viwili vya Waumini kuingiwa na khofu ya kushindwa na wakataka kurejea nyuma, Mwenyezi Mungu aliwalinda akawapa moyo wa kuthibiti, wakasonga mbele katika vita. Kwani hakika Mwenyezi Mungu ndiye mwenye utawala katika mambo yao mawili, na ndiye wa kuwalinda na kuwawezesha kwa kuwapa tawfiqi. Basi Waumini nawachukue funzo kutokana na haya, na wamtegemee Yeye ili awanusuru.
عربي تفسیرونه:
وَلَقَدۡ نَصَرَكُمُ ٱللَّهُ بِبَدۡرٖ وَأَنتُمۡ أَذِلَّةٞۖ فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ لَعَلَّكُمۡ تَشۡكُرُونَ
Na Mwenyezi Mungu alikwisha kunusuruni katika Badri nanyi mlikuwa wanyonge. Basi mcheni Mwenyezi Mungu ili mpate kushukuru.
Mwenyezi Mungu amewakumbusha Waumini ile neema ya nusura aliyo wapa katika vita vya Badri waliposubiri. Akawahakikishia kuwa Yeye ndiye aliye wapa ushindi katika vita vile na ingawa walikuwa wachache na wapungufu wa silaha; akawataka wamt'ii kuwa ni shukrani kwa neema hiyo. Badri ipo mwendo wa kiasi ya maili 120 kusini magharibi ya Madina. Mpambano hapo baina ya Waislamu na Makureshi ulikuwa siku ya Jumaane 17 Ramadhani mwaka wa pili wa Hijra (13 Machi 624 B.K.). Mtume s.a.w. na Masahaba wake walitoka Madina taarikh 8-9 ya Ramadhani mwaka wa pili wa Hijra (5 Machi 624 B.K.) Idadi ya wapiganaji wa Kiislamu katika vita hivi ilikuwa kiasi watu mia tatu au zaidi kidogo, na Washirikina walizidi mara tatu kuliko hao. Mwenyezi Mungu alitimiza ahadi yake katika vita hivi, Waumini wakashinda juu ya kuwa ni wachache, kwa kuwa Imani yao juu ya haki na uadilifu ilikuwa kubwa. Na kuungwa mkono na Mwenyezi Mungu pamoja na kuwa na moyo wenyewe kulikuwa ni sababu za ushindi kuliko wingi wa watu na ubora wa silaha. Ushindi huu ulio dhaahiri ukawa ndio sababu ya kuenea Neno la Imani na kutukuka likawa juu. Na hichi ni chanzo cha yaliyo kuja baadae, na kivuli cha Uislamu kikatanda Arabuni kote, na kisha kwengineko ulimwenguni.
عربي تفسیرونه:
إِذۡ تَقُولُ لِلۡمُؤۡمِنِينَ أَلَن يَكۡفِيَكُمۡ أَن يُمِدَّكُمۡ رَبُّكُم بِثَلَٰثَةِ ءَالَٰفٖ مِّنَ ٱلۡمَلَٰٓئِكَةِ مُنزَلِينَ
Ulipo waambia Waumini: Je, haitakutosheni ikiwa Mola wenu atakusaidieni kwa Malaika elfu tatu walio teremshwa?
Ushindi ulipatikana Mtume alipo waambia Waumini: Haitatosha kukutulizeni nafsi zenu Mola wenu Mlezi ikusaidieni kwa Malaika elfu tatu watakao letwa ili kukutieni nguvu?
عربي تفسیرونه:
بَلَىٰٓۚ إِن تَصۡبِرُواْ وَتَتَّقُواْ وَيَأۡتُوكُم مِّن فَوۡرِهِمۡ هَٰذَا يُمۡدِدۡكُمۡ رَبُّكُم بِخَمۡسَةِ ءَالَٰفٖ مِّنَ ٱلۡمَلَٰٓئِكَةِ مُسَوِّمِينَ
Kwani! Ikiwa mtavumilia na mkamchamngu na hata maadui wakikutokeeni kwa ghafla, basi hapo Mola wenu Mlezi atakusaidieni kwa Malaika elfu tano wanao shambulia kwa nguvu.
Ndio! Msaada huo unakutosheni. Na pindi mkivumilia vita, na mkashikilia uchamngu, na hata maadui zenu wakikutokeeni kwa ghafla, Mola wenu Mlezi atawaongeza hao Malaika mpaka wafike elfu tano ili kukupeni nguvu.wakikutokeeni kwa ghafla, Mola wenu Mlezi atawaongeza hao Malaika mpaka wafike elfu tano ili kukupeni nguvu.
عربي تفسیرونه:
وَمَا جَعَلَهُ ٱللَّهُ إِلَّا بُشۡرَىٰ لَكُمۡ وَلِتَطۡمَئِنَّ قُلُوبُكُم بِهِۦۗ وَمَا ٱلنَّصۡرُ إِلَّا مِنۡ عِندِ ٱللَّهِ ٱلۡعَزِيزِ ٱلۡحَكِيمِ
Na Mwenyezi Mungu hakufanya haya ila kuwa ni bishara kwenu, na ili nyoyo zenu zipate kutua. Na msaada hautoki isipo kuwa kwa Mwenyezi Mungu, Aliye tukuka, Mwenye nguvu na Mwenye hikima.
Na wala Mwenyezi Mungu hakujaalia huko kukuleteeni msaada wa Malaika ila iwe ni bishara tu kwenu ya ushindi, na zipate kutulia nyoyo zenu. Na hapana ushindi ila unao tokana na Mwenyezi Mungu Mwenye Kushinda wote, ambaye anapanga kila kitu kwa pahala pake, na anaye wapangia mambo waja wake Waumini.
عربي تفسیرونه:
لِيَقۡطَعَ طَرَفٗا مِّنَ ٱلَّذِينَ كَفَرُوٓاْ أَوۡ يَكۡبِتَهُمۡ فَيَنقَلِبُواْ خَآئِبِينَ
Haya ni kwa ajili awakate sehemu katika walio kufuru, au awahizi wapate kurejea nyuma nao wamepwelewa.
Naye Mwenyezi Mungu amekupeni ushindi ili wateketee baadhi ya wale walio kufuru kwa kuuwawa, au wadhalilike na awakasirishe kwa kushindwa na aibu na hizaya, wapate kurejea nao wameemewa.
عربي تفسیرونه:
لَيۡسَ لَكَ مِنَ ٱلۡأَمۡرِ شَيۡءٌ أَوۡ يَتُوبَ عَلَيۡهِمۡ أَوۡ يُعَذِّبَهُمۡ فَإِنَّهُمۡ ظَٰلِمُونَ
Wewe huna lako jambo katika haya - ama atawahurumia au atawaadhibu, kwani wao ni madhaalimu.
Huna lako katika ninayo wafanyia waja wangu, kwani mambo yote ni ya Mwenyezi Mungu. Ama atawasamehe kwa Imani, au atawaadhibu kwa kuuwawa na hizaya na mateso ya Siku ya Kiyama, kwani hao ni madhaalimu.
عربي تفسیرونه:
وَلِلَّهِ مَا فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَمَا فِي ٱلۡأَرۡضِۚ يَغۡفِرُ لِمَن يَشَآءُ وَيُعَذِّبُ مَن يَشَآءُۚ وَٱللَّهُ غَفُورٞ رَّحِيمٞ
Na ni vya Mwenyezi Mungu vyote vilivyomo katika Mbingu na vilivyomo katika Ardhi. Yeye humsamehe na humuadhibu amtakaye. Na Mwenyezi Mungu ni Msamehevu Mwenye kurehemu.
Bila ya shaka vitu vyote vilioko katika Mbingu na katika Ardhi ni vya Mwenyezi Mungu peke yake, kwa kuviumba na kuvimiliki. Na Yeye ndiye Mwenye uwezo juu ya kila kitu, kila kitu kimo mikononi mwake. Yeye humsamehe ampendaye na akamuadhibu amtakaye. Lakini kusamehe kwake ndiko kulio karibu zaidi, na rehema yake ni ya kutarajiwa sana zaidi. Kwani Yeye hakika ni mwingi wa kusamehe na kurehemu.
عربي تفسیرونه:
يَٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ لَا تَأۡكُلُواْ ٱلرِّبَوٰٓاْ أَضۡعَٰفٗا مُّضَٰعَفَةٗۖ وَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ لَعَلَّكُمۡ تُفۡلِحُونَ
Enyi mlio amini! Msile riba mkizidisha juu kwa juu, na mcheni Mwenyezi Mungu ili mpate kufanikiwa.
Enyi mlio amini! Mkikopesha msichukue katika deni ila rasilmali yenu tu. Msifanye kuzidisha juu ya deni faida ya kuzidi mwaka kwa mwaka ikawa kuzidi juu kwa juu. Msiyale mali ya watu kwa upotovu. Hakika nyinyi mtaongokewa na mtafuzu pindi mkiepukana na riba, ikiwa ndogo au kubwa.
عربي تفسیرونه:
وَٱتَّقُواْ ٱلنَّارَ ٱلَّتِيٓ أُعِدَّتۡ لِلۡكَٰفِرِينَ
Na uogopeni Moto ambao umeandaliwa kwa ajili ya makafiri.
Tahadharini na Moto ulio andaliwa kwa ajili ya makafiri kwa kujiepusha kutafuta kuihalalisha riba.
عربي تفسیرونه:
وَأَطِيعُواْ ٱللَّهَ وَٱلرَّسُولَ لَعَلَّكُمۡ تُرۡحَمُونَ
Na mt'iini Mwenyezi Mungu na Mtume ili mpate kurehemewa.
Na mt'iini Mwenyezi Mungu, na mt'iini Mtume katika kila wanacho amrisha na kila wanacho kikataza ili mpate kurehemeka duniani na Akhera.
عربي تفسیرونه:
 
د معناګانو ژباړه سورت: آل عمران
د سورتونو فهرست (لړلیک) د مخ نمبر
 
د قرآن کریم د معناګانو ژباړه - سواحلي ژباړه - علی محسن البرواني - د ژباړو فهرست (لړلیک)

علی محسن البرواني ژباړلې ده.

بندول