Check out the new design

د قرآن کریم د معناګانو ژباړه - سواحلي ژباړه - د رواد الترجمة مرکز * - د ژباړو فهرست (لړلیک)


د معناګانو ژباړه سورت: ذاریات   آیت:
وَٱلسَّمَآءِ ذَاتِ ٱلۡحُبُكِ
Ninaapa kwa mbingu zenye njia.
عربي تفسیرونه:
إِنَّكُمۡ لَفِي قَوۡلٖ مُّخۡتَلِفٖ
Hakika nyinyi bila ya shaka mmo katika kauli inayohitalifiana.
عربي تفسیرونه:
يُؤۡفَكُ عَنۡهُ مَنۡ أُفِكَ
Anageuzwa kutokana na haki mwenye kugeuzwa.
عربي تفسیرونه:
قُتِلَ ٱلۡخَرَّٰصُونَ
Wazushi wameangamizwa.
عربي تفسیرونه:
ٱلَّذِينَ هُمۡ فِي غَمۡرَةٖ سَاهُونَ
Ambao wameghafilika katika ujinga.
عربي تفسیرونه:
يَسۡـَٔلُونَ أَيَّانَ يَوۡمُ ٱلدِّينِ
Wanauliza: 'Ni lini hiyo siku ya malipo?'
عربي تفسیرونه:
يَوۡمَ هُمۡ عَلَى ٱلنَّارِ يُفۡتَنُونَ
Hiyo ni siku watakayoadhibiwa Motoni.
عربي تفسیرونه:
ذُوقُواْ فِتۡنَتَكُمۡ هَٰذَا ٱلَّذِي كُنتُم بِهِۦ تَسۡتَعۡجِلُونَ
Onjeni adhabu yenu! Haya ndiyo mliyokuwa mkiyafanyia haraka.
عربي تفسیرونه:
إِنَّ ٱلۡمُتَّقِينَ فِي جَنَّٰتٖ وَعُيُونٍ
Hakika wacha Mungu watakuwa katika Mabustani ya mbinguni na chemchemi.
عربي تفسیرونه:
ءَاخِذِينَ مَآ ءَاتَىٰهُمۡ رَبُّهُمۡۚ إِنَّهُمۡ كَانُواْ قَبۡلَ ذَٰلِكَ مُحۡسِنِينَ
Wanapokea yale aliyowapa Mola wao Mlezi. Kwa hakika hao walikuwa kabla ya haya wakifanya mema.
عربي تفسیرونه:
كَانُواْ قَلِيلٗا مِّنَ ٱلَّيۡلِ مَا يَهۡجَعُونَ
Walikuwa wakilala kidogo tu usiku.
عربي تفسیرونه:
وَبِٱلۡأَسۡحَارِ هُمۡ يَسۡتَغۡفِرُونَ
Na kabla ya alfajiri wakiomba maghfira.
عربي تفسیرونه:
وَفِيٓ أَمۡوَٰلِهِمۡ حَقّٞ لِّلسَّآئِلِ وَٱلۡمَحۡرُومِ
Na katika mali yao ipo haki ya mwenye kuomba na asiyeomba.
عربي تفسیرونه:
وَفِي ٱلۡأَرۡضِ ءَايَٰتٞ لِّلۡمُوقِنِينَ
Na katika ardhi zipo Ishara kwa wenye yakini.
عربي تفسیرونه:
وَفِيٓ أَنفُسِكُمۡۚ أَفَلَا تُبۡصِرُونَ
Na pia katika nafsi zenu - Je, hamwoni?
عربي تفسیرونه:
وَفِي ٱلسَّمَآءِ رِزۡقُكُمۡ وَمَا تُوعَدُونَ
Na katika mbingu ziko riziki zenu na yale mnayoahidiwa.
عربي تفسیرونه:
فَوَرَبِّ ٱلسَّمَآءِ وَٱلۡأَرۡضِ إِنَّهُۥ لَحَقّٞ مِّثۡلَ مَآ أَنَّكُمۡ تَنطِقُونَ
Basi ninaapa kwa Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, hakika haya ni kweli kama ilivyo kweli kuwa nyinyi mnasema.
عربي تفسیرونه:
هَلۡ أَتَىٰكَ حَدِيثُ ضَيۡفِ إِبۡرَٰهِيمَ ٱلۡمُكۡرَمِينَ
Je, imekufikia hadithi ya wageni wa Ibrahim wanaoheshimiwa?
عربي تفسیرونه:
إِذۡ دَخَلُواْ عَلَيۡهِ فَقَالُواْ سَلَٰمٗاۖ قَالَ سَلَٰمٞ قَوۡمٞ مُّنكَرُونَ
Walipoingia kwake na wakasema: 'Salama!' Na yeye akasema: 'Salama! Nyinyi ni watu nisiowajua.'
عربي تفسیرونه:
فَرَاغَ إِلَىٰٓ أَهۡلِهِۦ فَجَآءَ بِعِجۡلٖ سَمِينٖ
Basi akaenda kwa ahali yake na akaja na ndama aliyenona.
عربي تفسیرونه:
فَقَرَّبَهُۥٓ إِلَيۡهِمۡ قَالَ أَلَا تَأۡكُلُونَ
Akawakaribishia, akasema: 'Mbona hamli?'
عربي تفسیرونه:
فَأَوۡجَسَ مِنۡهُمۡ خِيفَةٗۖ قَالُواْ لَا تَخَفۡۖ وَبَشَّرُوهُ بِغُلَٰمٍ عَلِيمٖ
Kwa hivyo, akahisi kuwaogopa katika nafsi yake. Wakasema: 'Usiwe na hofu.' Basi wakambashiria kupata kijana mwenye elimu.
عربي تفسیرونه:
فَأَقۡبَلَتِ ٱمۡرَأَتُهُۥ فِي صَرَّةٖ فَصَكَّتۡ وَجۡهَهَا وَقَالَتۡ عَجُوزٌ عَقِيمٞ
Ndipo mkewe akawaelekea, na huku anasema na akijipiga usoni kwa mastaajabu, na kusema: Mimi ni kikongwe na tasa!
عربي تفسیرونه:
قَالُواْ كَذَٰلِكِ قَالَ رَبُّكِۖ إِنَّهُۥ هُوَ ٱلۡحَكِيمُ ٱلۡعَلِيمُ
Wakasema: Ndivyo vivyo hivyo alivyosema Mola wako Mlezi. Hakika Yeye ni Mwenye hekima, Mwenye kujua.
عربي تفسیرونه:
 
د معناګانو ژباړه سورت: ذاریات
د سورتونو فهرست (لړلیک) د مخ نمبر
 
د قرآن کریم د معناګانو ژباړه - سواحلي ژباړه - د رواد الترجمة مرکز - د ژباړو فهرست (لړلیک)

دا ژباړه د مرکز رواد الترجمة ټیم لخوا د ربوہ د تبلیغ ټولنې او د اسلامي منځپانګې د خدماتو ټولنې په همکارۍ شوې.

بندول