Check out the new design

Tradução dos significados do Nobre Qur’an. - Tradução Suaíli - Abdullah Muhammad e Nasser Khamis * - Índice de tradução


Tradução dos significados Surah: Hud   Versículo:
فَلَمَّا جَآءَ أَمۡرُنَا جَعَلۡنَا عَٰلِيَهَا سَافِلَهَا وَأَمۡطَرۡنَا عَلَيۡهَا حِجَارَةٗ مِّن سِجِّيلٖ مَّنضُودٖ
Basi amri yetu ilipokuja, ya adhabu kuwashukia, tuliifanya sehamu ya juu ya kijiji chao ambayo walikuwa wakiishi juu yake kuwa chini kwa kukigeuza. Na tuliwateremshia majiwe ya udongo ulio mgumu wenye nguvu, yamepangwa baadhi yake juu ya mengine na yamefuatana,
Os Tafssir em língua árabe:
مُّسَوَّمَةً عِندَ رَبِّكَۖ وَمَا هِيَ مِنَ ٱلظَّٰلِمِينَ بِبَعِيدٖ
yamewekwa alama huko kwa Mwenyezi Mungu kwa alama inayojulikana, hayafanani na majiwe yaliyo ardhini. Na hayakuwa majiwe haya ambayo Mwenyezi Mungu aliwateremshia watu wa Lūṭ, yako mbali na makafiri wa kikureshi kuwa watateremshiwa mfano wake. Katika haya kuna onyo kwa kila aliyeasi aliyeshindana na Mwenyezi Mungu.
Os Tafssir em língua árabe:
۞ وَإِلَىٰ مَدۡيَنَ أَخَاهُمۡ شُعَيۡبٗاۚ قَالَ يَٰقَوۡمِ ٱعۡبُدُواْ ٱللَّهَ مَا لَكُم مِّنۡ إِلَٰهٍ غَيۡرُهُۥۖ وَلَا تَنقُصُواْ ٱلۡمِكۡيَالَ وَٱلۡمِيزَانَۖ إِنِّيٓ أَرَىٰكُم بِخَيۡرٖ وَإِنِّيٓ أَخَافُ عَلَيۡكُمۡ عَذَابَ يَوۡمٖ مُّحِيطٖ
Na tulimtuma kwenda kwa watu wa Madyan ndugu yao Shu'ayb, akasema , «Enyi watu wangu, muabuduni Mwenyezi Mungu, Peke Yake. Nyinyi hamuna mungu yoyote anayestahiki kuabudiwa isipokuwa Yeye, Aliyetukuka na kuwa juu, basi mtakasieni ibada.. Wala msiwapunguzie watu haki zao katika vipimo vyao na mizani zao. Mimi nawaona nyinyi muko kwenye ukunjufu wa maisha, na mimi nawachelea, kwa sababu ya kupunguza vipimo na mizani, adhabu ya siku itakayowazunguka
Os Tafssir em língua árabe:
وَيَٰقَوۡمِ أَوۡفُواْ ٱلۡمِكۡيَالَ وَٱلۡمِيزَانَ بِٱلۡقِسۡطِۖ وَلَا تَبۡخَسُواْ ٱلنَّاسَ أَشۡيَآءَهُمۡ وَلَا تَعۡثَوۡاْ فِي ٱلۡأَرۡضِ مُفۡسِدِينَ
«Na enyi watu wangu, timizeni vipimo vya vibaba na mizani kwa usawa Wala msiwapunguzie watu haki zao katika jumala ya vitu vyao. Wala msiende katika ardhi mkifanya mambo ya kumuasi Mwenyezi Mungu na kueneza uharibifu.
Os Tafssir em língua árabe:
بَقِيَّتُ ٱللَّهِ خَيۡرٞ لَّكُمۡ إِن كُنتُم مُّؤۡمِنِينَۚ وَمَآ أَنَا۠ عَلَيۡكُم بِحَفِيظٖ
«Kile kitakachosalia kwenu cha faida ya halali, baada ya kutimiza vipimo na mizani, kina baraka na ni chema kwenu kuliko kile mkichukuacho cha pato la haramu kwa njia ya kupunja na mfano wake. Iwapo nyinyi mnamuamini Mwenyezi Mungu kikweli, basi fuateni amri Yake. Na mimi si mtunzi kwenu wa kuwahesabia matendo yenu.»
Os Tafssir em língua árabe:
قَالُواْ يَٰشُعَيۡبُ أَصَلَوٰتُكَ تَأۡمُرُكَ أَن نَّتۡرُكَ مَا يَعۡبُدُ ءَابَآؤُنَآ أَوۡ أَن نَّفۡعَلَ فِيٓ أَمۡوَٰلِنَا مَا نَشَٰٓؤُاْۖ إِنَّكَ لَأَنتَ ٱلۡحَلِيمُ ٱلرَّشِيدُ
Wakasema, «Ewe Shu'ayb, je swala hii ambayo unaendelea nayo ndiyo inayokuamuru wewe kwamba sisi tuache masanamu na mizimu ambayo baba zetu wanaabudu, au kwamba sisi tujizuie tusitumie njia tuziwezazo za hila na vitimbi katika kuchuma mali yetu?» Wakasema kwa njia ya kumcheza shere, «Wewe ndiye mwenye akili na hodari wa mipango ya usimamizi wa mali.»
Os Tafssir em língua árabe:
قَالَ يَٰقَوۡمِ أَرَءَيۡتُمۡ إِن كُنتُ عَلَىٰ بَيِّنَةٖ مِّن رَّبِّي وَرَزَقَنِي مِنۡهُ رِزۡقًا حَسَنٗاۚ وَمَآ أُرِيدُ أَنۡ أُخَالِفَكُمۡ إِلَىٰ مَآ أَنۡهَىٰكُمۡ عَنۡهُۚ إِنۡ أُرِيدُ إِلَّا ٱلۡإِصۡلَٰحَ مَا ٱسۡتَطَعۡتُۚ وَمَا تَوۡفِيقِيٓ إِلَّا بِٱللَّهِۚ عَلَيۡهِ تَوَكَّلۡتُ وَإِلَيۡهِ أُنِيبُ
Akasema Shu'ayb, «Enyi watu wangu, Mwaonaje iwapo mimi niko kwenye njia iliyo wazi itokayo kwa Mola wangu katika yale ninayowaitia ya kumtakasia Yeye ibada, na katika yale ninayowakataza ya kuharibu mali, na Akawa Ameniruzuku riziki ya ukunjufu ya halali iliyo nzuri? Na sitaki kuenda kinyume na nyinyi, nikafanya jambo nililowakataza; na sitaki, katika niwaamrishalo na niwakatazalo, isipokuwa ni kuwarakibisha kadiri ya uweza wangu na kujimudu kwangu. Na kuafikiwa kwangu, katika kuipata haki na kujaribu kuwarakibisha, kuko kwa Mwenyezi Mungu. Kwake Yeye, Peke Yake, nimejitegemeza, na Kwake Yeye narejea kwa kutubia na kuelekea.
Os Tafssir em língua árabe:
 
Tradução dos significados Surah: Hud
Índice de capítulos Número de página
 
Tradução dos significados do Nobre Qur’an. - Tradução Suaíli - Abdullah Muhammad e Nasser Khamis - Índice de tradução

Traduzido pelo Dr. Abdalla Mohamed Abubakar e Sheikh Nassor Khamis.

Fechar