Check out the new design

Tradução dos significados do Nobre Qur’an. - Tradução Suaíli - Abdullah Muhammad e Nasser Khamis * - Índice de tradução


Tradução dos significados Surah: Maryam   Versículo:
وَنَٰدَيۡنَٰهُ مِن جَانِبِ ٱلطُّورِ ٱلۡأَيۡمَنِ وَقَرَّبۡنَٰهُ نَجِيّٗا
Na tulimuita upande wa jabali la Ṭūr Sīnā’ kuliani kwake (Mūsā), na tukamleta karibu na tukamtukuza kwa kusema na yeye. Katika hii pana kuthibitisha sifa ya kusema kwa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, kama inavyonasibiana na utukufu Wake na ukamilifu Wake.
Os Tafssir em língua árabe:
وَوَهَبۡنَا لَهُۥ مِن رَّحۡمَتِنَآ أَخَاهُ هَٰرُونَ نَبِيّٗا
Na tulimtunukia Mūsā, kutokana na rehema zetu, ndugu yake Hārūn akawa Nabii mwenye kumtilia nguvu na kumsaidia.
Os Tafssir em língua árabe:
وَٱذۡكُرۡ فِي ٱلۡكِتَٰبِ إِسۡمَٰعِيلَۚ إِنَّهُۥ كَانَ صَادِقَ ٱلۡوَعۡدِ وَكَانَ رَسُولٗا نَّبِيّٗا
Na utaje, ewe Mtume, katika hii Qur’ani habari ya Ismāīl, amani imshukiye. Yeye alikuwa ni mkweli katika ahadi, hakuahidi kitu isipokuwa hukitekeleza, na alikuwa ni Mtume na ni Nabii.
Os Tafssir em língua árabe:
وَكَانَ يَأۡمُرُ أَهۡلَهُۥ بِٱلصَّلَوٰةِ وَٱلزَّكَوٰةِ وَكَانَ عِندَ رَبِّهِۦ مَرۡضِيّٗا
Na alikuwa akiwaamrisha watu wake kusimamisha Swala na kutoa Zaka, na alikuwa kwa Mola wake, Aliyeshinda na kutukuka, ni mwenye kuridhiwa.
Os Tafssir em língua árabe:
وَٱذۡكُرۡ فِي ٱلۡكِتَٰبِ إِدۡرِيسَۚ إِنَّهُۥ كَانَ صِدِّيقٗا نَّبِيّٗا
Na utaje, ewe Mtume, katika hii Qur’ani habari ya Idris, amani imshukiye. Yeye alikuwa ni mkweli mkubwa katika maneno yake na vitendo vyake, ni Nabii aaliyeletewa wahyi.
Os Tafssir em língua árabe:
وَرَفَعۡنَٰهُ مَكَانًا عَلِيًّا
Na tukauinua utajo wake kwa viumbe wote na cheo chake kwa wale waliosongezwa karibu. Akawa ni mwenye utajo wa juu na, ni mwenye cheo cha juu.
Os Tafssir em língua árabe:
أُوْلَٰٓئِكَ ٱلَّذِينَ أَنۡعَمَ ٱللَّهُ عَلَيۡهِم مِّنَ ٱلنَّبِيِّـۧنَ مِن ذُرِّيَّةِ ءَادَمَ وَمِمَّنۡ حَمَلۡنَا مَعَ نُوحٖ وَمِن ذُرِّيَّةِ إِبۡرَٰهِيمَ وَإِسۡرَٰٓءِيلَ وَمِمَّنۡ هَدَيۡنَا وَٱجۡتَبَيۡنَآۚ إِذَا تُتۡلَىٰ عَلَيۡهِمۡ ءَايَٰتُ ٱلرَّحۡمَٰنِ خَرُّواْۤ سُجَّدٗاۤ وَبُكِيّٗا۩
Hawa niliokusimulia habari zao, ewe Mtume, ni wale ambao Mwenyezi Mungu Amewaneemesha kwa nyongeza Zake na taufiki Yake, Akawafanya ni Mitume miongoni mwa kizazi cha Ādam, na miongoni mwa kizazi cha wale tuliowabeba pamoja na Nūḥ, katika jahazi, na miongoni mwa kizazi cha Ibrāhīm, na miongoni mwa kizazi cha Ya’qūb, na miongoni mwa wale tuliowaongoza kwenye Imani na tukawateua kwa utume na unabii. Wasomewapo aya za Mwingi wa rehema zinazokusanya upweke Wake na hoja Zake wanajipomosha chini hali ya kumsujudia Mwenyezi Mungu kwa kunyenyekea na kujidhalilisha , na wanalia kwa kumcha Yeye, kutakata ni Kwake na kutukuka ni Kwake.
Os Tafssir em língua árabe:
۞ فَخَلَفَ مِنۢ بَعۡدِهِمۡ خَلۡفٌ أَضَاعُواْ ٱلصَّلَوٰةَ وَٱتَّبَعُواْ ٱلشَّهَوَٰتِۖ فَسَوۡفَ يَلۡقَوۡنَ غَيًّا
Wakaja, baada ya hawa walioneemeshwa, wafuasi wabaya, waliacha Swala kabisa au waliitoa nje ya wakati wake au waliacha nguzo zake na mambo yake ya lazima na wakafuata yanayolingana na kunasibiana na matamanio yao. Basi hao watapata shari na upotevu na kupita patupu ndani ya Jahanamu.
Os Tafssir em língua árabe:
إِلَّا مَن تَابَ وَءَامَنَ وَعَمِلَ صَٰلِحٗا فَأُوْلَٰٓئِكَ يَدۡخُلُونَ ٱلۡجَنَّةَ وَلَا يُظۡلَمُونَ شَيۡـٔٗا
Lakini aliyetubia dhambi zake miongoni mwao, akamuamini Mola wake na akafanya mema kusadikisha toba yake, hao Mwenyezi Mungu Atakubali toba yao, na wataingia Peponi pamoja na Waumini, na hawatapunguziwa chochote katika matendo yao mema.
Os Tafssir em língua árabe:
جَنَّٰتِ عَدۡنٍ ٱلَّتِي وَعَدَ ٱلرَّحۡمَٰنُ عِبَادَهُۥ بِٱلۡغَيۡبِۚ إِنَّهُۥ كَانَ وَعۡدُهُۥ مَأۡتِيّٗا
Pepo yenye mabustani ya milele na makazi ya daima, nayo ni ile ambayo Mwingi wa rehema Aliwaahidi waja Wake na kuifanya wasiione, nao wakaiamini bila ya kuwa wameiona. Hakika agizo la Mwenyezi Mungu kwa waja Wake la hii Pepo ni lenye kuja, hapana budi.
Os Tafssir em língua árabe:
لَّا يَسۡمَعُونَ فِيهَا لَغۡوًا إِلَّا سَلَٰمٗاۖ وَلَهُمۡ رِزۡقُهُمۡ فِيهَا بُكۡرَةٗ وَعَشِيّٗا
Watu wa Peponi hawatasikia maneno ya batili humo, lakini watasikia ‘salamu’ ikiwa ndio maamkizi yao. Na watapata riziki yao humo ya chakula na kinywaji daima, kila wanapotaka, asubuhi na jioni, haina kiasi wala hadi maalumu.
Os Tafssir em língua árabe:
تِلۡكَ ٱلۡجَنَّةُ ٱلَّتِي نُورِثُ مِنۡ عِبَادِنَا مَن كَانَ تَقِيّٗا
Hiyo ndiyo Pepo inayosifiwa kwa sifa hizo, hiyo ndiyo ambayo tutairithisha na kuitoa kuwapa waja wetu wanaotucha kwa kufuata amri zetu na kujiepusha na makatazo yetu.
Os Tafssir em língua árabe:
وَمَا نَتَنَزَّلُ إِلَّا بِأَمۡرِ رَبِّكَۖ لَهُۥ مَا بَيۡنَ أَيۡدِينَا وَمَا خَلۡفَنَا وَمَا بَيۡنَ ذَٰلِكَۚ وَمَا كَانَ رَبُّكَ نَسِيّٗا
Na useme, ewe Jibrili, kumwambia Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukiye, «Sisi, Malaika, hatuteremki kutoka mbinguni kuja ardhini isipokuwa kwa amri ya Mola wako kwetu, ni Yake yaliyoko mbele yetu yanayotukabili ya mambo ya Akhera na yale yaliyoko nyuma yetu yaliyopita katika ulimwengu na yale yaliyoko baina ya ulimwengu na Akhera. Amri yote ni Yake ya mahali na wakati. Na hakuwa Mola wako ni Mwenye kusahau kitu chochote miongoni mwa vitu.
Os Tafssir em língua árabe:
 
Tradução dos significados Surah: Maryam
Índice de capítulos Número de página
 
Tradução dos significados do Nobre Qur’an. - Tradução Suaíli - Abdullah Muhammad e Nasser Khamis - Índice de tradução

Traduzido pelo Dr. Abdalla Mohamed Abubakar e Sheikh Nassor Khamis.

Fechar