Tradução dos significados do Nobre Qur’an. - Tradução Suaíli - Abdullah Muhammad e Nasser Khamis * - Índice de tradução


Tradução dos significados Versículo: (140) Surah: Suratu An-Nisaa
وَقَدۡ نَزَّلَ عَلَيۡكُمۡ فِي ٱلۡكِتَٰبِ أَنۡ إِذَا سَمِعۡتُمۡ ءَايَٰتِ ٱللَّهِ يُكۡفَرُ بِهَا وَيُسۡتَهۡزَأُ بِهَا فَلَا تَقۡعُدُواْ مَعَهُمۡ حَتَّىٰ يَخُوضُواْ فِي حَدِيثٍ غَيۡرِهِۦٓ إِنَّكُمۡ إِذٗا مِّثۡلُهُمۡۗ إِنَّ ٱللَّهَ جَامِعُ ٱلۡمُنَٰفِقِينَ وَٱلۡكَٰفِرِينَ فِي جَهَنَّمَ جَمِيعًا
Mola wenu Amewateremshia, enyi Waumini, katika Kitabu Chake kwamba mkisikia aya za Mwenyezi Mungu zinakanushwa na zinafanyiwa shere, basi msikae pamoja na wakanushaji hao wanaofanya shere, isipokuwa wakiingia kwenye mazungumzo yasiokuwa mazungumzo ya kukanusha na kuzifanyia shere aya za Mwenyezi Mungu. Nyinyi mkikaa nao, na wao wako katika hali hiyo, mtakuwa ni kama wao, kwa kuwa nyinyi mmeridhika na ukafiri wao na uchezaji shere wao. Na mwenye kuridhika na maasia ni kama mwenye kuyafanya. Hakika Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, ni Mwenye Atawakusanya wanafiki na makafiri wote ndani ya Moto wa Jahanamu ambapo humo watakumbana na ukali wa adhabu.
Os Tafssir em língua árabe:
 
Tradução dos significados Versículo: (140) Surah: Suratu An-Nisaa
Índice de capítulos Número de página
 
Tradução dos significados do Nobre Qur’an. - Tradução Suaíli - Abdullah Muhammad e Nasser Khamis - Índice de tradução

Tradução dos significados do Alcorão em suaíli pelo Dr. Abdalla Mohamed Abubakar e Nassor Khamis

Fechar