Tradução dos significados do Nobre Qur’an. - Tradução Suaíli - Abdullah Muhammad e Nasser Khamis * - Índice de tradução


Tradução dos significados Versículo: (29) Surah: Suratu Al-Fath
مُّحَمَّدٞ رَّسُولُ ٱللَّهِۚ وَٱلَّذِينَ مَعَهُۥٓ أَشِدَّآءُ عَلَى ٱلۡكُفَّارِ رُحَمَآءُ بَيۡنَهُمۡۖ تَرَىٰهُمۡ رُكَّعٗا سُجَّدٗا يَبۡتَغُونَ فَضۡلٗا مِّنَ ٱللَّهِ وَرِضۡوَٰنٗاۖ سِيمَاهُمۡ فِي وُجُوهِهِم مِّنۡ أَثَرِ ٱلسُّجُودِۚ ذَٰلِكَ مَثَلُهُمۡ فِي ٱلتَّوۡرَىٰةِۚ وَمَثَلُهُمۡ فِي ٱلۡإِنجِيلِ كَزَرۡعٍ أَخۡرَجَ شَطۡـَٔهُۥ فَـَٔازَرَهُۥ فَٱسۡتَغۡلَظَ فَٱسۡتَوَىٰ عَلَىٰ سُوقِهِۦ يُعۡجِبُ ٱلزُّرَّاعَ لِيَغِيظَ بِهِمُ ٱلۡكُفَّارَۗ وَعَدَ ٱللَّهُ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّٰلِحَٰتِ مِنۡهُم مَّغۡفِرَةٗ وَأَجۡرًا عَظِيمَۢا
Muhammad ni Mtume wa Mwenyezi Mungu, na wale walio pamoja na yeye katika dini yake, ni wakali juu ya makafiri, wanahurumiana wao kwa wao, utawaona wakirukuu na kumsujudia Mwenyezi Mungu katika Swala yao, wakimtarajia Mola wao Awatunuku fadhila Zake, Awatie Peponi na Awe radhi nao. Alama ya utiifu wao kwa Mwenyezi Mungu iko wazi kwenye nyuso zao kwa alama ya kusujudu na kuabudu. Hiii ndiyo sifa yao kwenye Taurati. Na sifa yao katika Injili ni kama sifa ya mmea wa nafaka uliotoa kijiti chake na tawi lake, kisha matawi yakawa mengi baada ya hapo, na mmea ukashikana, ukapata nguvu na ukasimama juu ya kigogo chake ukiwa na mandhari mazuri yanayowapendeza wakulima, ili kuwatia hasira kwa Waumini hawa, kwa wingi wao na uzuri wa mandhari yao, makafiri. Katika haya pana dalili ya ukafiri wa wenye kuwachukia Maswahaba, radhi za Mwenyezi Mungu ziwashukie, kwa kuwa yule ambaye Mwenyezi Mungu Anamtia hasira kwa Maswahaba basi ishapatikana kwake sababu ya hasira nayo ni ukafiri. Mwenyezi Mungu Amewaahidi waliomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake kati yao kusamehewa dhambi zao na kupewa malipo mema mengi yasiyokatika, nayo ni Pepo. (Na ahadi ya Mwenyezi Mungu ni ya ukweli unaoaminiwa usioenda kinyume. Na kila mwenye kufuata nyayo za Maswahaba, radhi za Mwenyezi Mungu ziwashukie, basi yeye anaingia kwenye hukumu yao ya kustahiki msamaha na malipo makubwa, na wao wana ubora, kutangulia mbele na ukamilifu ambao hakuna yoyote katika ummah huu atakayewafikia, radhi za Mwenyezi Mungu ziwashukie na Awaridhishe).
Os Tafssir em língua árabe:
 
Tradução dos significados Versículo: (29) Surah: Suratu Al-Fath
Índice de capítulos Número de página
 
Tradução dos significados do Nobre Qur’an. - Tradução Suaíli - Abdullah Muhammad e Nasser Khamis - Índice de tradução

Tradução dos significados do Alcorão em suaíli pelo Dr. Abdalla Mohamed Abubakar e Nassor Khamis

Fechar