Tradução dos significados do Nobre Qur’an. - Tradução Suaíli - Abdullah Muhammad e Nasser Khamis * - Índice de tradução


Tradução dos significados Versículo: (9) Surah: Suratu Al-Hujurat
وَإِن طَآئِفَتَانِ مِنَ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ ٱقۡتَتَلُواْ فَأَصۡلِحُواْ بَيۡنَهُمَاۖ فَإِنۢ بَغَتۡ إِحۡدَىٰهُمَا عَلَى ٱلۡأُخۡرَىٰ فَقَٰتِلُواْ ٱلَّتِي تَبۡغِي حَتَّىٰ تَفِيٓءَ إِلَىٰٓ أَمۡرِ ٱللَّهِۚ فَإِن فَآءَتۡ فَأَصۡلِحُواْ بَيۡنَهُمَا بِٱلۡعَدۡلِ وَأَقۡسِطُوٓاْۖ إِنَّ ٱللَّهَ يُحِبُّ ٱلۡمُقۡسِطِينَ
Na mapote mawili ya Waumini yakipigana, fanyeni upatanishi, enyi Waumini, baina yao kwa kuyaita yakubali kuamuliwa na Kitabu cha Mwenyezi Mungu na Sunnah ya Mtume Wake, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, na kuridhika na uamuzi wa hivyo viwili. Iwapo pote mojawapo ya yale mawili litalifanyia uadui pote lingine na litakataa kukubali mwito huo wa upatanishi, basi lipigeni vita mpaka lirudi kwenye uamuzi wa Mwenyezi Mungu na Mtume Wake, na likirudi fanyani upatanishi baina ya hayo mawili kwa haki, na mfanyeni uadilifu katika uamuzi wenu kwa kutotoka nje ya hukumu ya wenyezi Mungu na hukumu ya Mtume Wake katika uamuzi wenu. Hakika Mwenyezi Mungu Anawapenda waadilifu katika uamuzi wao, wanaohukumu baina ya viumbe Vyake kwa haki. Katika aya hii pana kuthibitisha sifa ya mapenzi kwa Mwenyezi Mungu kihakika, kama inavyonasibiana na utukufu Wake Aliyetakasika na kila sifa ya upungufu.
Os Tafssir em língua árabe:
 
Tradução dos significados Versículo: (9) Surah: Suratu Al-Hujurat
Índice de capítulos Número de página
 
Tradução dos significados do Nobre Qur’an. - Tradução Suaíli - Abdullah Muhammad e Nasser Khamis - Índice de tradução

Tradução dos significados do Alcorão em suaíli pelo Dr. Abdalla Mohamed Abubakar e Nassor Khamis

Fechar