Tradução dos significados do Nobre Qur’an. - Tradução em Swahili - Áli Muhsin * - Índice de tradução

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Tradução dos significados Versículo: (23) Surah: Suratu Yunus
فَلَمَّآ أَنجَىٰهُمۡ إِذَا هُمۡ يَبۡغُونَ فِي ٱلۡأَرۡضِ بِغَيۡرِ ٱلۡحَقِّۗ يَٰٓأَيُّهَا ٱلنَّاسُ إِنَّمَا بَغۡيُكُمۡ عَلَىٰٓ أَنفُسِكُمۖ مَّتَٰعَ ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَاۖ ثُمَّ إِلَيۡنَا مَرۡجِعُكُمۡ فَنُنَبِّئُكُم بِمَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ
Lakini akisha waokoa, mara wanafanya jeuri tena katika nchi bila ya haki. Enyi watu! Jeuri zenu zitakudhuruni wenyewe. Hii ni starehe ya maisha ya dunia tu. Kisha marejeo yenu ni kwetu, na hapo tutakuambieni mliyo kuwa mkiyatenda.
Na akisha waokoa kutokana na khatari ya kuteketea, wanavunja ahadi yao, na mara wanarejea kwenye fisadi walizo kuwa nazo kabla! Enyi watu mvunjao ahadi! Hakika matokeo ya kupindukia mipaka ya starehe na kudhulumu kwenu yatarejea juu yenu peke yenu. Na hakika hizo starehe mnazo zistarehea katika dunia yenu ni starehe za kidunia zenye mwisho. Kisha marejeo yenu ya mwisho ni kwa Mwenyezi Mungu, na Yeye atakulipeni kwa vitendo vyenu mlivyo vitanguliza duniani.
Os Tafssir em língua árabe:
 
Tradução dos significados Versículo: (23) Surah: Suratu Yunus
Índice de capítulos Número de página
 
Tradução dos significados do Nobre Qur’an. - Tradução em Swahili - Áli Muhsin - Índice de tradução

Tradução dos significados do Alcorão para o Swahili, pelo Ali Muhsin

Fechar