Tradução dos significados do Nobre Qur’an. - Tradução em Swahili - Áli Muhsin * - Índice de tradução

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Tradução dos significados Versículo: (18) Surah: Suratu Ar-Raad
لِلَّذِينَ ٱسۡتَجَابُواْ لِرَبِّهِمُ ٱلۡحُسۡنَىٰۚ وَٱلَّذِينَ لَمۡ يَسۡتَجِيبُواْ لَهُۥ لَوۡ أَنَّ لَهُم مَّا فِي ٱلۡأَرۡضِ جَمِيعٗا وَمِثۡلَهُۥ مَعَهُۥ لَٱفۡتَدَوۡاْ بِهِۦٓۚ أُوْلَٰٓئِكَ لَهُمۡ سُوٓءُ ٱلۡحِسَابِ وَمَأۡوَىٰهُمۡ جَهَنَّمُۖ وَبِئۡسَ ٱلۡمِهَادُ
Walio muitikia Mola wao Mlezi watapata wema. Na wasio muitikia, hata wangeli kuwa navyo vyote viliomo katika ardhi na mfano wa hivyo, bila ya shaka wangeli vitoa kujikombolea! Hao watapata hisabu mbaya kabisa, na makao yao ni Jahannamu. Na hapo ni pahala pabaya mno!
Watu kwa mujibu wa kupokea kwao uwongofu ni mafungu mawili. Fungu moja lilio itikia wito wa Mwenyezi Mungu Muumba Mwenye kupanga. Hilo litapata malipo mema duniani na Akhera. Fungu jengine lisilo itikia wito wa Aliye waumba. Hawa watapata malipo maovu Akhera. Na lau kuwa wanamiliki kila kiliomo duniani na mfano wake mara ya pili, hawawezi kujikinga na hayo malipo maovu! Lakini watapata kumiliki hayo? Kwa hivyo yao wao ni hisabu ya kuwaudhi, na wataishia katika Jahannamu, na huko ni pahali paovu mno pa kuishi.
Os Tafssir em língua árabe:
 
Tradução dos significados Versículo: (18) Surah: Suratu Ar-Raad
Índice de capítulos Número de página
 
Tradução dos significados do Nobre Qur’an. - Tradução em Swahili - Áli Muhsin - Índice de tradução

Tradução dos significados do Alcorão para o Swahili, pelo Ali Muhsin

Fechar