Tradução dos significados do Nobre Qur’an. - Tradução em Swahili - Áli Muhsin * - Índice de tradução

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Tradução dos significados Versículo: (33) Surah: Suratu Ar-Raad
أَفَمَنۡ هُوَ قَآئِمٌ عَلَىٰ كُلِّ نَفۡسِۭ بِمَا كَسَبَتۡۗ وَجَعَلُواْ لِلَّهِ شُرَكَآءَ قُلۡ سَمُّوهُمۡۚ أَمۡ تُنَبِّـُٔونَهُۥ بِمَا لَا يَعۡلَمُ فِي ٱلۡأَرۡضِ أَم بِظَٰهِرٖ مِّنَ ٱلۡقَوۡلِۗ بَلۡ زُيِّنَ لِلَّذِينَ كَفَرُواْ مَكۡرُهُمۡ وَصُدُّواْ عَنِ ٱلسَّبِيلِۗ وَمَن يُضۡلِلِ ٱللَّهُ فَمَا لَهُۥ مِنۡ هَادٖ
Je! Anaye isimamia kila nafsi kwa yale iliyo yachuma? Na wamemfanyia Mwenyezi Mungu kuwa na washirika! Sema watajeni. Au ndio mnampa khabari ya yale asiyo yajua katika ardhi; au ni maneno matupu? Bali walio kufuru wamepambiwa vitimbi vyao na wamezuiliwa njia. Na ambaye Mwenyezi Mungu amemwacha apotee basi hana wa kumwongoa.
Hakika washirikina wamefanya upumbavu katika kukanya kwao, wakamfanyia Mwenyezi Mungu washirika wa kuwaabudu. Kwani ati huyo ambaye ndiye Mwenye kuhifadhi na kuangalia kila nafsi, na kuipimia kwa kuilipa kheri na shari inayo ichuma, atakuwa wa kufananishwa na haya masanamu? Ewe Nabii! Waambie: Yaelezeni yalivyo kweli! Je, hayo masanamu ya hai? Yanaweza kujikinga na madhara? Yakiwa mawe hayanufaishi wala hayadhuru, basi mbona mnajidanganya nafsi zenu kuwa miungu hiyo ndio imemwambia Mwenyezi Mungu hayo ambayo mnadhani kuwa Yeye hayajui ya ardhi hii? Au mnaiweka kwenye cheo cha kuiabudu kwa maneno yanayo toka katika ndimi zenu? Hakika iliyopo ni kuwa watu hawa wamezugwa na mazingatio yao na mawazo yao ya upotovu. Na kwa sababu hiyo wameiacha Njia ya Haki wakabaki wakitanga tanga! Na wenye kupotea kama hao, basi hawana wa kuwaongoa yeyote, kwani wameziachisha nafsi zao Njia ya Uwongofu.
Os Tafssir em língua árabe:
 
Tradução dos significados Versículo: (33) Surah: Suratu Ar-Raad
Índice de capítulos Número de página
 
Tradução dos significados do Nobre Qur’an. - Tradução em Swahili - Áli Muhsin - Índice de tradução

Tradução dos significados do Alcorão para o Swahili, pelo Ali Muhsin

Fechar