Tradução dos significados do Nobre Qur’an. - Tradução em Swahili - Áli Muhsin * - Índice de tradução

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Tradução dos significados Versículo: (32) Surah: Suratu Az-Zukhruf
أَهُمۡ يَقۡسِمُونَ رَحۡمَتَ رَبِّكَۚ نَحۡنُ قَسَمۡنَا بَيۡنَهُم مَّعِيشَتَهُمۡ فِي ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَاۚ وَرَفَعۡنَا بَعۡضَهُمۡ فَوۡقَ بَعۡضٖ دَرَجَٰتٖ لِّيَتَّخِذَ بَعۡضُهُم بَعۡضٗا سُخۡرِيّٗاۗ وَرَحۡمَتُ رَبِّكَ خَيۡرٞ مِّمَّا يَجۡمَعُونَ
Kwani wao ndio wanao gawa rehema za Mola wako Mlezi? Sisi tumewagawanyia baina yao maisha yao katika uhai wa duniani, na tukawanyanyua baadhi yao juu ya wengine kwa daraja nyingi; kwa hivyo baadhi yao wanawafanya wenginewe wawatumikie. Na rehema za Mwenyezi Mungu ni bora kuliko hayo wanayo yakusanya.
Funguo za Utume hazimo katika mikono ya washirikina, hata wao wawakabidhi watu wenye vyeo. Sisi tumewapangia maisha yao kwa kuwa wao wenyewe hawajiwezi. Na tumewafadhilisha baadhi juu ya wengine katika riziki na vyeo, na kwa hivyo baadhi yao huwafanya wengineo wawasaidie na wawatumikie katika kutimiza haja zao, ili wategemeane katika kutafuta maisha na kupanga uhai. Na Unabii na yaliyo khusiana nayo katika neema za Akhera na dunia, ni bora kuliko vyeo vyote vya duniani.
Os Tafssir em língua árabe:
 
Tradução dos significados Versículo: (32) Surah: Suratu Az-Zukhruf
Índice de capítulos Número de página
 
Tradução dos significados do Nobre Qur’an. - Tradução em Swahili - Áli Muhsin - Índice de tradução

Tradução dos significados do Alcorão para o Swahili, pelo Ali Muhsin

Fechar