Tradução dos significados do Nobre Qur’an. - Tradução em Swahili - Áli Muhsin * - Índice de tradução

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Tradução dos significados Versículo: (71) Surah: Suratu Al-Maidah
وَحَسِبُوٓاْ أَلَّا تَكُونَ فِتۡنَةٞ فَعَمُواْ وَصَمُّواْ ثُمَّ تَابَ ٱللَّهُ عَلَيۡهِمۡ ثُمَّ عَمُواْ وَصَمُّواْ كَثِيرٞ مِّنۡهُمۡۚ وَٱللَّهُ بَصِيرُۢ بِمَا يَعۡمَلُونَ
Na wakadhani kuwa hapatakuwa majaribio; basi wakawa vipofu na viziwi. Kisha Mwenyezi Mungu akawapokelea toba zao. Kisha tena wengi katika wao wakawa vipofu na viziwi. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuyaona hayo wayatendayo.
Na hao Wana wa Israili walidhani hawatapata majaribio, yaani shida za kuwafafanua baina ya walio simama imara na wasio simama imara. Kwa hivyo hawakuweza kustahamili, bali wengi wao walipotea wakawa kama vipofu na viziwi. Wakaiacha Haki, na Mwenyezi Mungu akawapatiliza kwa madhila. Baadae walipo rejea kwa Mwenyezi Mungu na wakatubu, alikubali toba zao, na akawarejeshea utukufu wao. Lakini baadae tena wakaingia katika upotofu, na wakawa kama vipofu na viziwi! Na Mwenyezi Mungu anawajua vyema, na atashuhudia vitendo vyao, na atawalipa kwavyo.
Os Tafssir em língua árabe:
 
Tradução dos significados Versículo: (71) Surah: Suratu Al-Maidah
Índice de capítulos Número de página
 
Tradução dos significados do Nobre Qur’an. - Tradução em Swahili - Áli Muhsin - Índice de tradução

Tradução dos significados do Alcorão para o Swahili, pelo Ali Muhsin

Fechar