Ibisobanuro bya qoran ntagatifu - Ibisobanuro mu giswahili - abdullah muhamad na nasoor khamis * - Ishakiro ry'ibisobanuro


Ibisobanuro by'amagambo Umurongo: (12) Isura: Hud (Umuhanuzi Hud)
فَلَعَلَّكَ تَارِكُۢ بَعۡضَ مَا يُوحَىٰٓ إِلَيۡكَ وَضَآئِقُۢ بِهِۦ صَدۡرُكَ أَن يَقُولُواْ لَوۡلَآ أُنزِلَ عَلَيۡهِ كَنزٌ أَوۡ جَآءَ مَعَهُۥ مَلَكٌۚ إِنَّمَآ أَنتَ نَذِيرٞۚ وَٱللَّهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ وَكِيلٌ
Huenda wewe, ewe Mtume, kwa ukafiri na ukanushaji mkubwa unaouona kwao, ukawa ni mwenye kuyaacha baaadhi ya yale unaoyoletewa wahyi kati ya yale ambayo Mwenyezi Mungu Alikuteremshia na Akakuamuru kuyafikisha, na kifua chako kikawa ni chenye kuhisi dhiki kwa hayo, kwa kuogopa wasije wakataka baadhi ya mambo kutoka kwako kwa njia ya kukusumbua, kama vile kusema, «Kwa nini asiteremshiwe mali mengi, au asijiwe na Malaika ambaye atamuamini katika ujumbe wake?» Basi wafikishie yale niliyokuletea wahyi kwayo, kwani lako wewe si lingine isipokuwa ni kuonya kwa yale uliyoletewa wahyi. Na Mwenyezi Mungu ni Mtunzi wa kila kitu, Anaendesha mambo yote ya viumbe vyake.
Ibisobanuro by'icyarabu:
 
Ibisobanuro by'amagambo Umurongo: (12) Isura: Hud (Umuhanuzi Hud)
Urutonde rw'amasura numero y'urupapuro
 
Ibisobanuro bya qoran ntagatifu - Ibisobanuro mu giswahili - abdullah muhamad na nasoor khamis - Ishakiro ry'ibisobanuro

Guhindura ibisobanuro bya Quran mu giswahili byasobanuwe na Dr Abdallah Mohamed abubakar na nassor khamis

Gufunga