Check out the new design

Ibisobanuro bya qoran ntagatifu - Ibisobanuro bya Qur'an mu rurimi rw'igiswahili - Abdallah Mohamed na Nassor Khamis * - Ishakiro ry'ibisobanuro


Ibisobanuro by'amagambo Isura: Al Qaswasw   Umurongo:
قُلۡ أَرَءَيۡتُمۡ إِن جَعَلَ ٱللَّهُ عَلَيۡكُمُ ٱلَّيۡلَ سَرۡمَدًا إِلَىٰ يَوۡمِ ٱلۡقِيَٰمَةِ مَنۡ إِلَٰهٌ غَيۡرُ ٱللَّهِ يَأۡتِيكُم بِضِيَآءٍۚ أَفَلَا تَسۡمَعُونَ
Sema, ewe Mtume, «Nipeni habari, enyi watu, iwapo Mwenyezi Mungu Angaliwaekea usiku wa daima mpaka Siku ya Kiyama, ni mungu gani asiyekuwa Mwenyezi Mungu angaliwaletea mwangaza wa nyinyi kupata kuona? Basi kwani nyinyi hamsikii kwa namna ya kufahamu na kukubali?»
Ibisobanuro by'icyarabu:
قُلۡ أَرَءَيۡتُمۡ إِن جَعَلَ ٱللَّهُ عَلَيۡكُمُ ٱلنَّهَارَ سَرۡمَدًا إِلَىٰ يَوۡمِ ٱلۡقِيَٰمَةِ مَنۡ إِلَٰهٌ غَيۡرُ ٱللَّهِ يَأۡتِيكُم بِلَيۡلٖ تَسۡكُنُونَ فِيهِۚ أَفَلَا تُبۡصِرُونَ
Waambie, «Nipeni habari iwapo Mwenyezi Mungu Angaliwaekea mchana wa daima mpaka Siku ya Kiyama, ni mungu gani asiyekuwa Mwenyezi Mungu angaliwaletea usiku wa nyinyi kutulia na kupumzika ndani yake? Basi hamuoni kwa maangalizi yenu kule kupishana kwa usiku na mchana?»
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَمِن رَّحۡمَتِهِۦ جَعَلَ لَكُمُ ٱلَّيۡلَ وَٱلنَّهَارَ لِتَسۡكُنُواْ فِيهِ وَلِتَبۡتَغُواْ مِن فَضۡلِهِۦ وَلَعَلَّكُمۡ تَشۡكُرُونَ
Na miongoni mwa rehema Yake kwenu, enyi watu, ni kuwafanyia usiku na mchana Akatafautisha baina ya viwili hivi, Akaufanya huu usiku kuwa ni giza, ili mutulie humo na miili yenu ipumzike. Na Akawafanyia mchana kuwa ni mwangaza, ili mutafute maisha yenu na ili mumshukuru Yeye kwa kuwapa nyinyi neema zake hizo.
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَيَوۡمَ يُنَادِيهِمۡ فَيَقُولُ أَيۡنَ شُرَكَآءِيَ ٱلَّذِينَ كُنتُمۡ تَزۡعُمُونَ
Na Siku ambayo Mwenyezi Mungu Atawaita hawa washirikina Awaambie, «Wako wapi washirika wangu ambao mulikuwa mukidai duniani kwamba wao ni washirika wangu?».
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَنَزَعۡنَا مِن كُلِّ أُمَّةٖ شَهِيدٗا فَقُلۡنَا هَاتُواْ بُرۡهَٰنَكُمۡ فَعَلِمُوٓاْ أَنَّ ٱلۡحَقَّ لِلَّهِ وَضَلَّ عَنۡهُم مَّا كَانُواْ يَفۡتَرُونَ
Na tutamtoa kwenye kila ummah, miongoni mwa ummah zenye kukanusha, shahidi, naye ni Nabii wao, atakayetoa ushahidi juu ya yaliyopita duniani ya ushirikina wao na ukanushaji wao Mitume wao. Tukaziambia ummah hizo zilizokanusha Mitume wake na yale waliyoyaleta kutoka kwa Mwenyezi Mungu, «Leteni hoja yenu juu ya kile mlichomshirikisha nacho Mwenyezi Mungu.» Wakati huo watajua kuwa hoja nzuri ni ya Mwenyezi Mungu juu yao, kuwa haki ni ya Mwenyezi Mungu, na kitawaondokea kile walichokuwa wakimzulia Mola wao kisiwanufaishe hiko, bali kiwadhuru na kiwafikishe kwenye Moto wa Jahanamu.
Ibisobanuro by'icyarabu:
۞ إِنَّ قَٰرُونَ كَانَ مِن قَوۡمِ مُوسَىٰ فَبَغَىٰ عَلَيۡهِمۡۖ وَءَاتَيۡنَٰهُ مِنَ ٱلۡكُنُوزِ مَآ إِنَّ مَفَاتِحَهُۥ لَتَنُوٓأُ بِٱلۡعُصۡبَةِ أُوْلِي ٱلۡقُوَّةِ إِذۡ قَالَ لَهُۥ قَوۡمُهُۥ لَا تَفۡرَحۡۖ إِنَّ ٱللَّهَ لَا يُحِبُّ ٱلۡفَرِحِينَ
Hakika Qārūn alikuwa ni miongoni mwa watu wa jamii ya Mūsā, rehema na amani zimshukiye, akakiuka mpaka wake katika kuwa na kiburi na ujabari juu yao. Na tulimpa Qārūn mahazina mengi ya mali, mpaka ikafikia kiwango cha kuwa funguo zake zinawaelemea idadi kubwa ya watu wenye nguvu kuzibeba. Walipomuambia watu wake, «Usifanye kiburi ukawa na gogi la furaha kwa mali uliyonayo. Hakika Mwenyezi Mungu Hawapendi kati ya waja wake wale wenye kiburi ambao hawamshukuru Mwenyezi Mungu Aliyetukuka kwa kile Alichowapa.
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَٱبۡتَغِ فِيمَآ ءَاتَىٰكَ ٱللَّهُ ٱلدَّارَ ٱلۡأٓخِرَةَۖ وَلَا تَنسَ نَصِيبَكَ مِنَ ٱلدُّنۡيَاۖ وَأَحۡسِن كَمَآ أَحۡسَنَ ٱللَّهُ إِلَيۡكَۖ وَلَا تَبۡغِ ٱلۡفَسَادَ فِي ٱلۡأَرۡضِۖ إِنَّ ٱللَّهَ لَا يُحِبُّ ٱلۡمُفۡسِدِينَ
«Na utafute, kwa mali Aliyokupa Mwenyezi Mungu, malipo mema ya Nyumba ya Akhera, kwa kufanyia mambo ya kumtii Mwenyezi Mungu duniani, na usiache fungu lako la duniani la kustarehe humo kwa halali bila kupita kiasi, na uwafanyie watu hisani kwa kuwapa sadaka kama vile Mwenyezi Mungu Alivyokufanyia hisani kwa kukupa mali mengi haya, na usitafute kile Alichokiharamisha Mwenyezi Mungu cha kuwadhulumu watu wako, kwani hakika Mwenyezi Mungu Hawapendi waharibifu, na Atawalipa kwa matendo yao mabaya.»
Ibisobanuro by'icyarabu:
 
Ibisobanuro by'amagambo Isura: Al Qaswasw
Urutonde rw'amasura numero y'urupapuro
 
Ibisobanuro bya qoran ntagatifu - Ibisobanuro bya Qur'an mu rurimi rw'igiswahili - Abdallah Mohamed na Nassor Khamis - Ishakiro ry'ibisobanuro

Byasobanuwe na Dr. Abdalla Mohamed Abubakar na Sheikh Nassor Khamis.

Gufunga