Ibisobanuro bya qoran ntagatifu - Ibisobanuro mu giswahili - abdullah muhamad na nasoor khamis * - Ishakiro ry'ibisobanuro


Ibisobanuro by'amagambo Umurongo: (119) Isura: Al Im’ran (Umuryango Wa Imurani)
هَٰٓأَنتُمۡ أُوْلَآءِ تُحِبُّونَهُمۡ وَلَا يُحِبُّونَكُمۡ وَتُؤۡمِنُونَ بِٱلۡكِتَٰبِ كُلِّهِۦ وَإِذَا لَقُوكُمۡ قَالُوٓاْ ءَامَنَّا وَإِذَا خَلَوۡاْ عَضُّواْ عَلَيۡكُمُ ٱلۡأَنَامِلَ مِنَ ٱلۡغَيۡظِۚ قُلۡ مُوتُواْ بِغَيۡظِكُمۡۗ إِنَّ ٱللَّهَ عَلِيمُۢ بِذَاتِ ٱلصُّدُورِ
Huu ndio ushahidi wa makosa yenu kwa kuwapenda wao. Nyinyi mnawapenda na mnawafanyia wema, na wao hawawapendi. Na wanawabebea nyinyi uadui na chuki, ilhali nyinyi mnaviamini vitabu vyote vlivyoteremshwa, kikiwemo kitabu chao, na wao hawakiamini kitabu chenu. Basi vipi mtawapenda? Na wanapokutana na nyinyi wanasema kinafiki, «Tumeamini na tumesadiki.» Na wanapokuwa faragha, wenyewe kwa wenyewe, yaonekena wana kero na masikitiko. Hapo huwa wakiziuma ncha za vidole vyao, kutokana na hasira kali walionayo juu ya mshikamano wa Waislamu, kuwa neno lao ni moja, kuwa Uislamu umepata nguvu na kuwa wao wamekuwa wanyonge kwa sababu ya kupata nguvu Uislamu. Waambie, ewe Mtume, «Kufeni kwa hasira zenu kali mlizonazo. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuyaona yanayofichwa ndani ya vifua na Atamlipa kila mmoja kwa aliyoyatanguliza ya kheri au ya shari.»
Ibisobanuro by'icyarabu:
 
Ibisobanuro by'amagambo Umurongo: (119) Isura: Al Im’ran (Umuryango Wa Imurani)
Urutonde rw'amasura numero y'urupapuro
 
Ibisobanuro bya qoran ntagatifu - Ibisobanuro mu giswahili - abdullah muhamad na nasoor khamis - Ishakiro ry'ibisobanuro

Guhindura ibisobanuro bya Quran mu giswahili byasobanuwe na Dr Abdallah Mohamed abubakar na nassor khamis

Gufunga