Check out the new design

Ibisobanuro bya qoran ntagatifu - Ibisobanuro bya Qur'an mu rurimi rw'igiswahili - Abdallah Mohamed na Nassor Khamis * - Ishakiro ry'ibisobanuro


Ibisobanuro by'amagambo Isura: Az-zumar   Umurongo:
قُلۡ إِنِّيٓ أُمِرۡتُ أَنۡ أَعۡبُدَ ٱللَّهَ مُخۡلِصٗا لَّهُ ٱلدِّينَ
Sema, ewe Mtume, uwaambie watu, «Mwenyezi Mungu Ameniamrisha mimi na anayenifuata kumtakasia Yeye ibada, Peke Yake, bila mwingine,
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَأُمِرۡتُ لِأَنۡ أَكُونَ أَوَّلَ ٱلۡمُسۡلِمِينَ
na Ameniamrisha niwe wa kwanza kujisalimisha miongoni mwa ummah wangu, akasalimu amri Kwake kwa kumpwekesha na kumtakasia Ibada na akajiepusha na kila kisichokuwa Yeye miongoni mwa waungu.
Ibisobanuro by'icyarabu:
قُلۡ إِنِّيٓ أَخَافُ إِنۡ عَصَيۡتُ رَبِّي عَذَابَ يَوۡمٍ عَظِيمٖ
Sema, ewe Mtume, uwaambie watu, «Mimi ninachelea nikimuasi Mola wangu, katika kile alichoniamuru cha kumuabudu na kumtakasia katika kumtii, adhabu ya Siku hiyo ambayo kituko chake ni kikubwa.
Ibisobanuro by'icyarabu:
قُلِ ٱللَّهَ أَعۡبُدُ مُخۡلِصٗا لَّهُۥ دِينِي
Sema, ewe Mtume, «Kwa hakika Mimi ninamuabudu Mwenyezi Mungu, Peke Yake, Asiye na mshirika, nikimtakasia ibada yangu na utiifu wangu.
Ibisobanuro by'icyarabu:
فَٱعۡبُدُواْ مَا شِئۡتُم مِّن دُونِهِۦۗ قُلۡ إِنَّ ٱلۡخَٰسِرِينَ ٱلَّذِينَ خَسِرُوٓاْ أَنفُسَهُمۡ وَأَهۡلِيهِمۡ يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِۗ أَلَا ذَٰلِكَ هُوَ ٱلۡخُسۡرَانُ ٱلۡمُبِينُ
Basi nyinyi, enyi washirikina, abuduni mnachotaka badala ya Mwenyezi Mungu miongoni mwa mizimu na masanamu na visiokuwa hivyo katika viumbe Vyake, kwani hilo halinidhuru mimi chochote.» Na hili ni onyo na tahadharisho kwa anayemuabudu asiyekuwa Mwenyezi Mungu na akamshirikisha mwingine pamoja na Yeye. Sema, ewe Mtume, «Hakika wale wenye hasara kikweli ni wale watakaohasirika nafsi zao na watu wao Siku ya Kiyama.» Na hiyo ni kwa sababu ya kuwapoteza duniani na kuwapotosha na njia ya Imani. Jua utanabahi kwamba hawa washirikina kupata hasara ya nafsi zao na watu wao Siku ya Kiyama ndiko kupata hasara kuliofunuka waziwazi.
Ibisobanuro by'icyarabu:
لَهُم مِّن فَوۡقِهِمۡ ظُلَلٞ مِّنَ ٱلنَّارِ وَمِن تَحۡتِهِمۡ ظُلَلٞۚ ذَٰلِكَ يُخَوِّفُ ٱللَّهُ بِهِۦ عِبَادَهُۥۚ يَٰعِبَادِ فَٱتَّقُونِ
Hao wenye kupata hasara watawekewa juu yau Siku ya Kiyama, wakiwa ndani ya Jahanamu, vipande vya adhabu juu yao vinavyotokana na Moto, kama kwamba ni sakafu zilizojengewa na pia chini yao. Adhabu hiyo yenye sifa hizo ndio ile ambayo Mweyezi Mungu anawaogopesha nayo waja Wake ili wajihadhari nayo. Hivyo basi, enyi waja wangu, nicheni kwa kuzifuata amri zangu na kujiepusha na matendo ya kuniasi.
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَٱلَّذِينَ ٱجۡتَنَبُواْ ٱلطَّٰغُوتَ أَن يَعۡبُدُوهَا وَأَنَابُوٓاْ إِلَى ٱللَّهِ لَهُمُ ٱلۡبُشۡرَىٰۚ فَبَشِّرۡ عِبَادِ
Na wale waliojiepusha kumtii Shetani na kuabudu asiyekuwa Mwenyezi Mungu na wakatubia kwa Mwenyezi Mungu kwa kumuabudu na kumtakasia Dini, basi hao wana bishara njema duniani ya kutajwa vyema na kuafikiwa na Mwenyezi Mungu, na bishara njema huko Akhera ya kupata radhi za Mwenyezi Mungu na starehe za daima Peponi. Basi wape habari njema, ewe Nabii, waja wangu
Ibisobanuro by'icyarabu:
ٱلَّذِينَ يَسۡتَمِعُونَ ٱلۡقَوۡلَ فَيَتَّبِعُونَ أَحۡسَنَهُۥٓۚ أُوْلَٰٓئِكَ ٱلَّذِينَ هَدَىٰهُمُ ٱللَّهُۖ وَأُوْلَٰٓئِكَ هُمۡ أُوْلُواْ ٱلۡأَلۡبَٰبِ
ambao wanasikiliza maneno na kufuata yaliyo sawa zaidi. Na maneno mazuri zaidi na yaliyo sawa zaidi ni maneno ya Mwenyezi Mungu kisha ni maneno ya Mtume Wake. Hao ndio wale ambao Mwenyezi Mungu Amewaafikia kwenye usawa na haki na akawaongoza kwenye tabia na matendo bora zaidi; hao ndio watu wenye akili zilizotimia.
Ibisobanuro by'icyarabu:
أَفَمَنۡ حَقَّ عَلَيۡهِ كَلِمَةُ ٱلۡعَذَابِ أَفَأَنتَ تُنقِذُ مَن فِي ٱلنَّارِ
Je, yule ambaye lilipasa juu yake neno la adhabu, kwa kuendelea kwenye upotevu na upotovu wake, kwani huna, ewe Mtume, njia yoyote ya kumuongoa. Je, unaweza kumuokoa aliye Motoni? Wewe si mwenye kuweza hilo.
Ibisobanuro by'icyarabu:
لَٰكِنِ ٱلَّذِينَ ٱتَّقَوۡاْ رَبَّهُمۡ لَهُمۡ غُرَفٞ مِّن فَوۡقِهَا غُرَفٞ مَّبۡنِيَّةٞ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُۖ وَعۡدَ ٱللَّهِ لَا يُخۡلِفُ ٱللَّهُ ٱلۡمِيعَادَ
Lakini wale waliomcha Mola wao, kwa kumtii na kwa kumtakasia ibada, watakuwa na vyumba, huko Peponi, vilivyojengewa baadhi yake juu ya vingine, ambavyo chini ya miti yake mito inapita. Mwenyezi Mungu amewaahidi (vyumba hivyo) waja Wake wachamungu, ahadi ambayo ni yenye kutimia kwa uhakika, na Mwenyezi Mungu Haendi kinyume na ahadi,
Ibisobanuro by'icyarabu:
أَلَمۡ تَرَ أَنَّ ٱللَّهَ أَنزَلَ مِنَ ٱلسَّمَآءِ مَآءٗ فَسَلَكَهُۥ يَنَٰبِيعَ فِي ٱلۡأَرۡضِ ثُمَّ يُخۡرِجُ بِهِۦ زَرۡعٗا مُّخۡتَلِفًا أَلۡوَٰنُهُۥ ثُمَّ يَهِيجُ فَتَرَىٰهُ مُصۡفَرّٗا ثُمَّ يَجۡعَلُهُۥ حُطَٰمًاۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَذِكۡرَىٰ لِأُوْلِي ٱلۡأَلۡبَٰبِ
Je, huoni, ewe Mtume, kuwa Mwenyezi Mungu Anateremsha mvua kutoka mawinguni, akaitia ardhini, akaifanya ni mikondo yenye kuchimbuka na maji yenye kutiririka, kisha anatoa kwa maji hayo mimea yenye rangi tafauti na aina mbalimbali, kisha inakauka baada ya ubichi wake na mng’aro wake, hapo utaiona imebadilika kuwa rangi ya manjano, kisha Anaifanya kuwa ni mapepe yaliyovunjikavunjika na kumumunyuka? Kwa hakika, katika kitendo hiko cha Mwenyezi Mungu pana ukumbusho na mawaidha kwa wenye akili timamu.
Ibisobanuro by'icyarabu:
 
Ibisobanuro by'amagambo Isura: Az-zumar
Urutonde rw'amasura numero y'urupapuro
 
Ibisobanuro bya qoran ntagatifu - Ibisobanuro bya Qur'an mu rurimi rw'igiswahili - Abdallah Mohamed na Nassor Khamis - Ishakiro ry'ibisobanuro

Byasobanuwe na Dr. Abdalla Mohamed Abubakar na Sheikh Nassor Khamis.

Gufunga