Ibisobanuro bya qoran ntagatifu - Ibisobanuro mu giswahili - abdullah muhamad na nasoor khamis * - Ishakiro ry'ibisobanuro


Ibisobanuro by'amagambo Umurongo: (13) Isura: Al Maidat
فَبِمَا نَقۡضِهِم مِّيثَٰقَهُمۡ لَعَنَّٰهُمۡ وَجَعَلۡنَا قُلُوبَهُمۡ قَٰسِيَةٗۖ يُحَرِّفُونَ ٱلۡكَلِمَ عَن مَّوَاضِعِهِۦ وَنَسُواْ حَظّٗا مِّمَّا ذُكِّرُواْ بِهِۦۚ وَلَا تَزَالُ تَطَّلِعُ عَلَىٰ خَآئِنَةٖ مِّنۡهُمۡ إِلَّا قَلِيلٗا مِّنۡهُمۡۖ فَٱعۡفُ عَنۡهُمۡ وَٱصۡفَحۡۚ إِنَّ ٱللَّهَ يُحِبُّ ٱلۡمُحۡسِنِينَ
Kwa sababu ya hawa Mayahudi kuvunja ahadi zao zilizotiliwa mkazo, tuliwafukuza kutoka kwenye rehama yetu na tukazijaalia nyoyo zao kuwa ngumu, hazilainiki kwa Imani, wanayageuza maneno ya Mwenyezi Mungu ambayo Alimteremshia Mūsā, nayo ni Taurati, na wakaacha kuitumia sehemu ya yale waliyokumbushwa nayo. Na utaendelea , ewe Mtume, kupata kutoka kwa Mayahudi uhaini na uvunjaji ahadi, kwani wao wako kwenye njia ya mababu zao, isipokuwa wachache miongoni mwao. Basi samehe kwa mabaya wanayokutendea na usiwe na chuki juu yao. Hakika Mwenyezi Mungu Anampenda anayefanya uzuri wa kusamehe na kutokuwa na chuki kwa aliyemfanyia ubaya. (Hivi ndivyo vile watu wapotovu wanapata njia ya kufikia malengo yao mabaya kwa kuyapotoa maneno ya Mwenyezi Mungu na kuyapa maana ambayo siyo yake. Wakishindwa kupotoa na kugeuza maana, wanayaacha yale yasioafikiana na matamanio yao katika sheria ya Mwenyezi Mungu ambayo hawatathibiti juu yake isipokuwa wachache waliyohifadhiwa na Mwenyezi Mungu kati yao).
Ibisobanuro by'icyarabu:
 
Ibisobanuro by'amagambo Umurongo: (13) Isura: Al Maidat
Urutonde rw'amasura numero y'urupapuro
 
Ibisobanuro bya qoran ntagatifu - Ibisobanuro mu giswahili - abdullah muhamad na nasoor khamis - Ishakiro ry'ibisobanuro

Guhindura ibisobanuro bya Quran mu giswahili byasobanuwe na Dr Abdallah Mohamed abubakar na nassor khamis

Gufunga