Ibisobanuro bya qoran ntagatifu - Ibisobanuro mu giswahili - abdullah muhamad na nasoor khamis * - Ishakiro ry'ibisobanuro


Ibisobanuro by'amagambo Umurongo: (32) Isura: Al Maidat
مِنۡ أَجۡلِ ذَٰلِكَ كَتَبۡنَا عَلَىٰ بَنِيٓ إِسۡرَٰٓءِيلَ أَنَّهُۥ مَن قَتَلَ نَفۡسَۢا بِغَيۡرِ نَفۡسٍ أَوۡ فَسَادٖ فِي ٱلۡأَرۡضِ فَكَأَنَّمَا قَتَلَ ٱلنَّاسَ جَمِيعٗا وَمَنۡ أَحۡيَاهَا فَكَأَنَّمَآ أَحۡيَا ٱلنَّاسَ جَمِيعٗاۚ وَلَقَدۡ جَآءَتۡهُمۡ رُسُلُنَا بِٱلۡبَيِّنَٰتِ ثُمَّ إِنَّ كَثِيرٗا مِّنۡهُم بَعۡدَ ذَٰلِكَ فِي ٱلۡأَرۡضِ لَمُسۡرِفُونَ
Kwa sababu ya uhalifu huu wa mauaji, tuliwaekea sheria Wana wa Isrāīl kwamba yoyote mwenye kumuua mtu pasi na sababu ya kulipiza kisasi au ya uharibifu katika ardhi, kwa aina yoyote kati ya aina za uharibifu zinazopelekea mauaji, kama ushirikina na uharamia, atakuwa ni kama kwamba amewaua watu wote kwa jinsi atakavyostahili mateso makubwa kutoka kwa Mwenyezi Mungu, na kwamba yule atakayejizuia asiue mtu ambaye Mwenyezi Mungu Ameharamisha kuuawa, ni kama kwamba amewahuisha watu wote. Hivyo basi, kulinda heshima ya binadamu mmoja ni kulinda heshima ya binadamu wote. Hakika Mitume wetu waliwajia Wana wa Isrāīl kwa hoja na dalili juu ya usawa wa yale waliyowalingania kwayo ya kumuamini Mola wao na kuyatekeleza yale yaliyofanywa wajibu kwao na Mola wao. Kisha, wengi kati yao, baada ya kujiwa na Mitume ni wenye kupita mipaka ya Mwenyezi Mungu kwa kuyafanya yaliyoharamishwa na Mwenyezi Mungu na kuyaacha maamrisho yake.
Ibisobanuro by'icyarabu:
 
Ibisobanuro by'amagambo Umurongo: (32) Isura: Al Maidat
Urutonde rw'amasura numero y'urupapuro
 
Ibisobanuro bya qoran ntagatifu - Ibisobanuro mu giswahili - abdullah muhamad na nasoor khamis - Ishakiro ry'ibisobanuro

Guhindura ibisobanuro bya Quran mu giswahili byasobanuwe na Dr Abdallah Mohamed abubakar na nassor khamis

Gufunga