Ibisobanuro bya qoran ntagatifu - Ibisobanuro mu giswahili - abdullah muhamad na nasoor khamis * - Ishakiro ry'ibisobanuro


Ibisobanuro by'amagambo Umurongo: (97) Isura: Al Maidat
۞ جَعَلَ ٱللَّهُ ٱلۡكَعۡبَةَ ٱلۡبَيۡتَ ٱلۡحَرَامَ قِيَٰمٗا لِّلنَّاسِ وَٱلشَّهۡرَ ٱلۡحَرَامَ وَٱلۡهَدۡيَ وَٱلۡقَلَٰٓئِدَۚ ذَٰلِكَ لِتَعۡلَمُوٓاْ أَنَّ ٱللَّهَ يَعۡلَمُ مَا فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَمَا فِي ٱلۡأَرۡضِ وَأَنَّ ٱللَّهَ بِكُلِّ شَيۡءٍ عَلِيمٌ
Mwenyezi Mungu Amewafadhili waja Wake kwa kuijaalia Alkaba, Nyumba takatifu, ni utengenefu wa Dini yao na amani ya uhai wao. Hivyo ni kwa kuwa wamemuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na wakasimamisha faradhi Zake. Na Ameharamisha uadui na kupigana katika miezi mitakatifu (nayo ni Mfungopili, Mfungotatu, Mfungone na Rajabu) ili mtu yoyote asimfanyie mwingine uadui katika miezi hiyo. Na Ameharamisha, Aliyetukuka, kuwavamia wanyama- howa wanaotolewa kuwa ni tunu kwa Haram. Kadhalika, Ameharamisha kuvivunjia heshima qalaid, navyo ni vitu vilivyovishwa shingoni mwa hao wanyama kuonyesha kuwa wanakusudiwa kuchinjwa kwa ibada. Hivyo basi, ni mupate kujua kuwa Mwenyezi Mungu Anayajua yote yaliyo mbinguni na ardhini, miongoni mwayo ni sheria Alizoziweka kuwahami viumbe Wake wasidhuriane wao kwa wao. Na pia mupate kujua kwamba Mwenyezi Mungu kwa kila kitu ni Mjuzi, hakuna chochote chenye kufichika Kwake.
Ibisobanuro by'icyarabu:
 
Ibisobanuro by'amagambo Umurongo: (97) Isura: Al Maidat
Urutonde rw'amasura numero y'urupapuro
 
Ibisobanuro bya qoran ntagatifu - Ibisobanuro mu giswahili - abdullah muhamad na nasoor khamis - Ishakiro ry'ibisobanuro

Guhindura ibisobanuro bya Quran mu giswahili byasobanuwe na Dr Abdallah Mohamed abubakar na nassor khamis

Gufunga