Ibisobanuro bya qoran ntagatifu - Ibisobanuro mu giswahili - abdullah muhamad na nasoor khamis * - Ishakiro ry'ibisobanuro


Ibisobanuro by'amagambo Umurongo: (17) Isura: Al An’fal
فَلَمۡ تَقۡتُلُوهُمۡ وَلَٰكِنَّ ٱللَّهَ قَتَلَهُمۡۚ وَمَا رَمَيۡتَ إِذۡ رَمَيۡتَ وَلَٰكِنَّ ٱللَّهَ رَمَىٰ وَلِيُبۡلِيَ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ مِنۡهُ بَلَآءً حَسَنًاۚ إِنَّ ٱللَّهَ سَمِيعٌ عَلِيمٞ
Nyinyi, enyi Waumini, hamukuwaua washirikina siku ya Badr, lakini Mwenyezi Mungu ndiye Aliwaua, kwa kuwa Aliwasaidia nyinyi kufanya hilo. Na hukurusha uliporusha, ewe Nabii, lakini ni Mwenyezi Mungu Aliyerusha, kwa kuwa Alikifikisha kile ulichokirusha kwenye nyuso za washirikina; na ili Mwenyezi Mungu Awafanyie mtihani wenye kumuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake, na Awafikishe kwa sababu ya jihadi kwenye daraja za juu, na Awajulisha wao neema Zake kwao wapate kumshukuru, kutakata na sifa za upungufu ni Kwake, kwa hilo. Hakika Mwenyezi Mungu ni Msikizi wa dua zenu na maneno yenu mliyoyaficha na mliyoyafanya waziwazi, ni Mjuzi wa yenye nafuu kwa waja Wake.
Ibisobanuro by'icyarabu:
 
Ibisobanuro by'amagambo Umurongo: (17) Isura: Al An’fal
Urutonde rw'amasura numero y'urupapuro
 
Ibisobanuro bya qoran ntagatifu - Ibisobanuro mu giswahili - abdullah muhamad na nasoor khamis - Ishakiro ry'ibisobanuro

Guhindura ibisobanuro bya Quran mu giswahili byasobanuwe na Dr Abdallah Mohamed abubakar na nassor khamis

Gufunga