Ibisobanuro bya qoran ntagatifu - Ibisobanuro mu giswahili - Ali Muhsen AL barwany * - Ishakiro ry'ibisobanuro

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Ibisobanuro by'amagambo Umurongo: (63) Isura: An Nur (Urumuri)
لَّا تَجۡعَلُواْ دُعَآءَ ٱلرَّسُولِ بَيۡنَكُمۡ كَدُعَآءِ بَعۡضِكُم بَعۡضٗاۚ قَدۡ يَعۡلَمُ ٱللَّهُ ٱلَّذِينَ يَتَسَلَّلُونَ مِنكُمۡ لِوَاذٗاۚ فَلۡيَحۡذَرِ ٱلَّذِينَ يُخَالِفُونَ عَنۡ أَمۡرِهِۦٓ أَن تُصِيبَهُمۡ فِتۡنَةٌ أَوۡ يُصِيبَهُمۡ عَذَابٌ أَلِيمٌ
Msifanye wito wa Mtume baina yenu kama wito wa nyinyi kwa nyinyi. Hakika Mwenyezi Mungu anawajua miongoni mwenu wanao ondoka kwa uficho. Basi nawatahadhari wanao khalifu amri yake, usije ukawapata msiba au ikawapata adhabu chungu.
Fanyeni hima kuhishimu wito wa Mtume kukuiteni kukusanyika kwa mambo muhimu. Na muitikieni huo wito wake, wala msifanye wito huo kama mnavyo itana nyinyi kwa nyinyi, kuwa inafaa kupuuza na kuondoka mpendavyo. Wala msiondoke ila baada ya kutaka ruhusa na mkakubaliwa, na tena iwe katika mipaka ya ufinyo kabisa, na dharura za shida. Na Mwenyezi Mungu Subhanahu anawajua wanao ondoka bila ya idhini wakijificha ficha kati ya watu ili ati Mtume asiwaone. Na watahadhari wanao kwenda kinyume na amri ya Mwenyezi Mungu asije Subhanahu akawapatiliza kwa uasi wao wakapata mateso makali duniani kama ukame na mitetemeko, au akawapa adhabu yenye wingi wa uchungu aliyo waandalia Akhera, nayo ni ya Motoni.
Ibisobanuro by'icyarabu:
 
Ibisobanuro by'amagambo Umurongo: (63) Isura: An Nur (Urumuri)
Urutonde rw'amasura numero y'urupapuro
 
Ibisobanuro bya qoran ntagatifu - Ibisobanuro mu giswahili - Ali Muhsen AL barwany - Ishakiro ry'ibisobanuro

Guhindura ibisobanuro bya Quran mu giswahili byasobanuwe na Ali Muhsen AL barwaniy

Gufunga