Ibisobanuro bya qoran ntagatifu - Ibisobanuro mu giswahili - Ali Muhsen AL barwany * - Ishakiro ry'ibisobanuro

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Ibisobanuro by'amagambo Umurongo: (97) Isura: Annisau (Abagore)
إِنَّ ٱلَّذِينَ تَوَفَّىٰهُمُ ٱلۡمَلَٰٓئِكَةُ ظَالِمِيٓ أَنفُسِهِمۡ قَالُواْ فِيمَ كُنتُمۡۖ قَالُواْ كُنَّا مُسۡتَضۡعَفِينَ فِي ٱلۡأَرۡضِۚ قَالُوٓاْ أَلَمۡ تَكُنۡ أَرۡضُ ٱللَّهِ وَٰسِعَةٗ فَتُهَاجِرُواْ فِيهَاۚ فَأُوْلَٰٓئِكَ مَأۡوَىٰهُمۡ جَهَنَّمُۖ وَسَآءَتۡ مَصِيرًا
Hakika Malaika watawaambia wale ambao wamewafisha nao wamejidhulumu nafsi zao: Mlikuwa vipi? Watasema: Tulikuwa tunaonewa. Watawaambia: Kwani ardhi ya Mwenyezi Mungu haikuwa na wasaa wa kuhamia humo? Basi hao makaazi yao ni Jahannamu, nayo ni marejeo mabaya kabisa.
Na hakika ni waajibu wa Muislamu kuhamia kwenye dola ya Kiislamu asiishi katika udhalili. Malaika watawauliza wakisha kufa: Mlikuwaje hata mkaridhia maisha ya unyonge na kudharauliwa? Na wao watajibu: Tulikuwa wanyonge katika nchi hiyo tukionewa. Malaika watawaambia: Kwani ardhi ya Mwenyezi Mungu haikuwa kunjufu ina wasaa, mkaweza kuhama badala ya kuishi katika uonevu? Watu hao wanao kubali uonevu, na wao wanaweza kuondoka, makao yao yatakuwa ni Jahannamu. Na hayo ni mashukio maovu kabisa. Basi Muislamu haimfalii kuishi katika udhalili, bali aishi na utukufu wake na hishima yake.
Ibisobanuro by'icyarabu:
 
Ibisobanuro by'amagambo Umurongo: (97) Isura: Annisau (Abagore)
Urutonde rw'amasura numero y'urupapuro
 
Ibisobanuro bya qoran ntagatifu - Ibisobanuro mu giswahili - Ali Muhsen AL barwany - Ishakiro ry'ibisobanuro

Guhindura ibisobanuro bya Quran mu giswahili byasobanuwe na Ali Muhsen AL barwaniy

Gufunga