Check out the new design

Ibisobanuro bya qoran ntagatifu - Ibisobanuro bya Qur'an mu rurimi rw'igiswahili - Ali Muhsin Al-Barwani. * - Ishakiro ry'ibisobanuro

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Ibisobanuro by'amagambo Isura: Zukh’ruf   Umurongo:
وَٱلَّذِي نَزَّلَ مِنَ ٱلسَّمَآءِ مَآءَۢ بِقَدَرٖ فَأَنشَرۡنَا بِهِۦ بَلۡدَةٗ مَّيۡتٗاۚ كَذَٰلِكَ تُخۡرَجُونَ
Na ambaye ndiye aliye teremsha kutoka mbinguni maji kwa kiasi, na kwa hayo tukaifufua nchi iliyo kufa. Na namna hivi ndivyo mtakavyo tolewa.
Na ambaye aliye kuteremshieni maji kwa kiasi ya haja kutoka mbinguni tukaihuisha nchi kavu isiyo na mimea. Kuhuisha kama huko ndivyo mtavyo fufuliwa kutoka makaburini kwenu kwa ajili ya hisabu. Basi yawaje mnakukataa?
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَٱلَّذِي خَلَقَ ٱلۡأَزۡوَٰجَ كُلَّهَا وَجَعَلَ لَكُم مِّنَ ٱلۡفُلۡكِ وَٱلۡأَنۡعَٰمِ مَا تَرۡكَبُونَ
Na ambaye ndiye aliye umba katika kila kitu jike na dume, na akakufanyieni marikebu na wanyama mnao wapanda.
Na ambaye aliye kuumbieni namna zote za viumbe, akavifanya vikutumikieni vyombo vya baharini na ngamia kuwa ni vipando katika safari zenu kutimiza haja zenu.
Ibisobanuro by'icyarabu:
لِتَسۡتَوُۥاْ عَلَىٰ ظُهُورِهِۦ ثُمَّ تَذۡكُرُواْ نِعۡمَةَ رَبِّكُمۡ إِذَا ٱسۡتَوَيۡتُمۡ عَلَيۡهِ وَتَقُولُواْ سُبۡحَٰنَ ٱلَّذِي سَخَّرَ لَنَا هَٰذَا وَمَا كُنَّا لَهُۥ مُقۡرِنِينَ
Ili mkae vizuri migongoni mwao, kisha mkumbuke neema za Mola wenu Mlezi mnapokaa sawa sawa juu yao na mseme: Ametakasika aliye mfanya huyu atutumikie, na tusingeli weza kufanya haya wenyewe.
Ili mtulie juu yao, kisha mkumbuke neema za Muumba wenu na Mlezi wenu kwa kuvifanya hivyo vikutumikieni mnapo tulia juu yao, na kwa kuadhimisha kule kuvifanya vinyonge kwa njia ya ajabu, na kutambua uweza mlio wezeshwa kuvidhibiti na kuvitawala, mseme: Subhana, Ametakasika aliye mfanya huyu (au hichi) kuwa dhalili kututumikia na sisi wenyewe tusingeli weza kumdhalilisha.
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَإِنَّآ إِلَىٰ رَبِّنَا لَمُنقَلِبُونَ
Na hakika sisi tutarudi kwa Mola wetu Mlezi.
Na hakika sisi ni wenye kurejea kwa Muumba wetu baada ya maisha haya, ili ahisabiwe kila mmoja kwa iliyo tanguliza mikono yake.
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَجَعَلُواْ لَهُۥ مِنۡ عِبَادِهِۦ جُزۡءًاۚ إِنَّ ٱلۡإِنسَٰنَ لَكَفُورٞ مُّبِينٌ
Na wanamfanyia katika waja wake fungu. Kwa hakika mwanaadamu ni mtovu wa fadhila aliye dhaahiri.
Na makafiri washirikina wamemfanyia Mwenyezi Mungu Subhanahu katika viumbe vyake mwana wakaamini kuwa ni sehemu ya nafsi yake. Hakika mwanaadamu kwa kitendo chake hichi hadi amepita ukomo katika ukafiri wake, na upinzani wake uwazi.
Ibisobanuro by'icyarabu:
أَمِ ٱتَّخَذَ مِمَّا يَخۡلُقُ بَنَاتٖ وَأَصۡفَىٰكُم بِٱلۡبَنِينَ
Au amejichukulia watoto wanawake katika vile alivyo viumba, na akakuteulieni nyinyi watoto wanaume?
Ati mnadai kwamba Yeye amejitwalia katika viumbe vyake watoto wa kike, na nyinyi akakukhiarieni watoto wanaume? Ama hakika haya ni mambo ya ajabu kweli!
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَإِذَا بُشِّرَ أَحَدُهُم بِمَا ضَرَبَ لِلرَّحۡمَٰنِ مَثَلٗا ظَلَّ وَجۡهُهُۥ مُسۡوَدّٗا وَهُوَ كَظِيمٌ
Na anapo bashiriwa mmoja wao kwa yale aliyo mpigia mfano Mwenyezi Mungu, uso wake husawijika na hujaa hasira.
Wamekuzulia Wewe hayo, na ilhali wao akipewa khabari mmoja wao kwamba amepata mtoto wa kike uso wake husawajika kwa kuudhika, naye kajaa masikitiko na huzuni kwa kuona anapewa khabari mbaya.
Ibisobanuro by'icyarabu:
أَوَمَن يُنَشَّؤُاْ فِي ٱلۡحِلۡيَةِ وَهُوَ فِي ٱلۡخِصَامِ غَيۡرُ مُبِينٖ
Ati aliye lelewa katika mapambo, na katika mabishano hawezi kusema kwa bayana?
Hivyo hawa wana fanya jeuri ya kumpachikia Mwenyezi Mungu mwana, ambaye kwa maumbile yake amelelewa katika mapambo, na hata hawezi kujadiliana na kupambana kwa hoja kwa nuksani yake ya kubaini. Ama hili ni jambo la ajabu!
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَجَعَلُواْ ٱلۡمَلَٰٓئِكَةَ ٱلَّذِينَ هُمۡ عِبَٰدُ ٱلرَّحۡمَٰنِ إِنَٰثًاۚ أَشَهِدُواْ خَلۡقَهُمۡۚ سَتُكۡتَبُ شَهَٰدَتُهُمۡ وَيُسۡـَٔلُونَ
Na wakawafanya Malaika, ambao ni waja wa Mwingi wa Rehema, ni wanawake! Kwani wameshuhudia kuumbwa kwao? Ushahidi wao utaandikwa na wao watahojiwa!
Na ati wakawaita Malaika, viumbe vya Mwenyezi Mungu, kuwa ni wanawake. Kwani wao waliwashuhudia walipo umbwa, hata watoe hukumu kwa jambo hilo? Hawakuliona! Sisi tutausajili uzushi wao huu. Na Siku ya Kiyama watakuja hisabiwa.
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَقَالُواْ لَوۡ شَآءَ ٱلرَّحۡمَٰنُ مَا عَبَدۡنَٰهُمۗ مَّا لَهُم بِذَٰلِكَ مِنۡ عِلۡمٍۖ إِنۡ هُمۡ إِلَّا يَخۡرُصُونَ
Nao husema: Angeli penda Mwingi wa Rehema tusingeli waabudu sisi. Hawana ujuzi wowote wa hayo! Hawana ila kusema uwongo tu!
Na washirikina husema ati: Lau kuwa Mwingi wa Rehema angeli kuwa anataka tusiiabudu hii miungu basi tusingeli iabudu. Wanakusudia kudai kuwa ati Mwenyezi Mungu yu radhi kuabudiwa hiyo miungu. Wanasema hayo bila ya kuwa na ilimu yoyote ya kuyategemezea wayasemayo. Hawa si chochote ila ni wenye kudhani tu. Hunena maneno yasio na ushahidi wowote.
Ibisobanuro by'icyarabu:
أَمۡ ءَاتَيۡنَٰهُمۡ كِتَٰبٗا مِّن قَبۡلِهِۦ فَهُم بِهِۦ مُسۡتَمۡسِكُونَ
Kwani tuliwapa Kitabu kabla ya hichi, na ikawa wao wanakishikilia hicho?
Kwani tuliwapa Kitabu kabla ya Qur'ani cha kuunga mkono huu uzushi wao, ndio maana wakashikamana nao kwa nguvu hivi? Hatukuwateremshia Kitabu namna hiyo. Basi hawana hoja ya kuinukulu.
Ibisobanuro by'icyarabu:
بَلۡ قَالُوٓاْ إِنَّا وَجَدۡنَآ ءَابَآءَنَا عَلَىٰٓ أُمَّةٖ وَإِنَّا عَلَىٰٓ ءَاثَٰرِهِم مُّهۡتَدُونَ
Bali wanasema: Hakika sisi tuliwakuta baba zetu wanashika dini makhsusi, basi na sisi tunaongoza nyayo zao.
Lakini washirikina walipo shindwa na hoja zote walisema: Hakika sisi tumewakuta baba zetu wakifuata dini hii; na sisi tunaendelea kufuata nyayo zao.
Ibisobanuro by'icyarabu:
 
Ibisobanuro by'amagambo Isura: Zukh’ruf
Urutonde rw'amasura numero y'urupapuro
 
Ibisobanuro bya qoran ntagatifu - Ibisobanuro bya Qur'an mu rurimi rw'igiswahili - Ali Muhsin Al-Barwani. - Ishakiro ry'ibisobanuro

byasobanuwe na Ali Muhsen Al-Barwaniy.

Gufunga