Ibisobanuro bya qoran ntagatifu - Ibisobanuro mu giswahili - Ali Muhsen AL barwany * - Ishakiro ry'ibisobanuro

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Ibisobanuro by'amagambo Umurongo: (4) Isura: Al Maidat
يَسۡـَٔلُونَكَ مَاذَآ أُحِلَّ لَهُمۡۖ قُلۡ أُحِلَّ لَكُمُ ٱلطَّيِّبَٰتُ وَمَا عَلَّمۡتُم مِّنَ ٱلۡجَوَارِحِ مُكَلِّبِينَ تُعَلِّمُونَهُنَّ مِمَّا عَلَّمَكُمُ ٱللَّهُۖ فَكُلُواْ مِمَّآ أَمۡسَكۡنَ عَلَيۡكُمۡ وَٱذۡكُرُواْ ٱسۡمَ ٱللَّهِ عَلَيۡهِۖ وَٱتَّقُواْ ٱللَّهَۚ إِنَّ ٱللَّهَ سَرِيعُ ٱلۡحِسَابِ
Wanakuuliza wamehalalishiwa nini? Sema: Mmehalalishiwa kila vilivyo vizuri na mlicho wafundisha wanyama kukiwinda. Mnawafundisha alivyo kufunzeni Mwenyezi Mungu. Basi kuleni walicho kukamatieni, na mkisomee jina la Mwenyezi Mungu. Na mcheni Mwenyezi Mungu; hakika Mwenyezi Mungu ni Mwepesi wa kuhisabu.
Ewe Mtume! Waumini wanakuuliza nini walicho halalishiwa katika vyakula na vyenginevyo? Waambie: Mwenyezi Mungu amekuhalalishieni kila chema kipendacho nafsi njema. Na pia amekuhalalishieni kula kinacho windwa na wanyama wenu mlio wafunza kuwinda, kwa kutokana na alivyo kufunzeni Mwenyezi Mungu. Basi kuleni wanacho winda wanyama hao mlio watuma, na mtaje jina la Mwenyezi Mungu pale mnapo watomeza. Na mcheni Mwenyezi Mungu kwa kuzishika sharia zake, wala msikiuke mipaka yake. Tahadharini kumkhalifu Mwenyezi Mungu katika hayo, kwani Yeye ni Mwepesi wa kuhisabu.
Ibisobanuro by'icyarabu:
 
Ibisobanuro by'amagambo Umurongo: (4) Isura: Al Maidat
Urutonde rw'amasura numero y'urupapuro
 
Ibisobanuro bya qoran ntagatifu - Ibisobanuro mu giswahili - Ali Muhsen AL barwany - Ishakiro ry'ibisobanuro

Guhindura ibisobanuro bya Quran mu giswahili byasobanuwe na Ali Muhsen AL barwaniy

Gufunga