Përkthimi i kuptimeve të Kuranit Fisnik - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني * - Përmbajtja e përkthimeve

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Përkthimi i kuptimeve Ajeti: (15) Surja: Suretu En Nahl
وَأَلۡقَىٰ فِي ٱلۡأَرۡضِ رَوَٰسِيَ أَن تَمِيدَ بِكُمۡ وَأَنۡهَٰرٗا وَسُبُلٗا لَّعَلَّكُمۡ تَهۡتَدُونَ
 Na kaweka katika ardhi milima ili ardhi isiyumbe yumbe nanyi.Na mito, na njia ili mpate kuongoka.
Na Mwenyezi Mungu amefanya katika ardhi milima iliyo simama imara, ili kuizuia isiyumbe yumbe.(Mwaka 1956 wataalamu wa geology, ilimu ya tabaka za ardhi, wamegundua kuwa kweli milima inasaidia kuizuia ardhi isitaharaki na kuachana. Wamevumbua kuwa mabara, continents, yamo katika kutaharaki. Kwa mfano kusini ya Amerika iliambatana na Afrika ya Magharibi, na ilisota mpaka ikafanyikana milima ya Andes. Hali kadhaalika Milima ya Himalaya ikazuia kusota kwa Bara Hindi. Pia wamegundua kuwa maki ya gamba la ardhi kwa kawaida halizidi kilomita 6, lakini chini ya milima hufika hata kilomita 35. Basi ni kweli kuwa milima ni kama vigingi vya kuzuia ardhi isiyumbe, kama ilivyo sema Qur'ani miaka 1400 iliyo pita.) Na Mwenyezi Mungu amefanya katika ardhi mito inayo pita na maji yanayo faa kunywa na kunyweshea makulima, na njia zilizo tengenezwa ili mpate kuzipitia kwendea mtakako.
Tefsiret në gjuhën arabe:
 
Përkthimi i kuptimeve Ajeti: (15) Surja: Suretu En Nahl
Përmbajtja e sureve Numri i faqes
 
Përkthimi i kuptimeve të Kuranit Fisnik - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني - Përmbajtja e përkthimeve

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها علي محسن البرواني.

Mbyll