Kisha Siku ya Kiyama atawahizi na atasema: Wako wapi hao washirika wangu ambao kwao mkiwakutisha (Manabii) mashaka? Watasema walio pewa ilimu:Hakika leo ndiyo hizaya na adhabu itawashukia makafiri,
Na kisha huko Akhera watapo fufuliwa watu na wakahisabiwa kwa vitendo vyao, Mwenyezi Mungu atawasimamisha msimamo wa hizaya na fedheha, atapo wafedhehi na afichue waliyo kuwa wakiyaficha vifuani mwao. Atawaambia: Wako wapi hao miungu mliyo ifanya kuwa ni washirika wangu kwa kuwaabudu? Nanyi kwa ajili yao mlikuwa mkinipiga vita Mimi na Mitume wangu! Wako wapi wapate kukuungeni mkono, kama mlivyo kuwa mkidai? Hawatoweza kujibu! Na hapo tena wale wanao ijua Haki, miongoni mwa Manabii, na Waumini, na Malaika, watasema: Leo ndiyo hizaya na adhabu mbaya kabisa zitawashukia makafiri!
Ambao Malaika waliwafisha nao wamejidhulumu nafsi zao! Basi watasalimu amri, waseme: Hatukuwa tukifanya uovu wowote. (Wataambiwa): Kwani! Hakika Mwenyezi Mungu anajua sana mliyo kuwa mkiyatenda.
Hizaya itawashukia makafiri walio endelea na ukafiri wao mpaka Malaika walipo watoa roho, nao wamejidhulumu nafsi zao kwa ushirikina na kutenda maovu, na wakasalimu amri tena baada ya inadi ndefu walipo jua hakika ya makosa yao. Wakasema uwongo kwa jinsi walivyo shituka: Hatukuwa duniani tukifanya maasi yoyote! Malaika na Manabii watawaambia: Hasha! Hakika nyinyi ni waongo, bali mmetenda maasi maovu kabisa! Na Mwenyezi Mungu, Subhanahu, anajua vyema kila dogo na kubwa mlilo kuwa mkilitenda katika dunia yenu. Hakukuleteeni faida yoyote huko kukataa kwenu!
Basi ingieni milango ya Jahannamu, humo mdumu. Ni maovu mno makaazi ya wafanyao kiburi!
Na baada ya hayo wataambiwa: Mwisho wenu ni kuingia Motoni, na adhabu ya huko ni ya milele, haikatiki! Na mbaya mno nyumba ya Jahannamu kuwa ni makaazi ya kila mwenye kutakabari akakataa kufuata Haki na Imani ya Mwenyezi Mungu na Mitume wake.
Na wataambiwa walio mcha Mungu: Mola wenu Mlezi kateremsha nini? Watasema: Kheri. Walio fanya wema katika dunia hii watapata wema. Na nyumba ya Akhera ni bora zaidi, na njema mno nyumba ya wachamngu.
Na walio muamini Mwenyezi Mungu na wakajikinga na kila linalo mghadhibisha Yeye ikiwa neno, au kitendo, au itikadi, wataambiwa: Mola wenu Mlezi kamteremshia nini Mtume wake? Wao watasema: Amemteremshia Qur'ani...ndani yake mna kheri ya duniani na Akhera kwa watu wote, na kwa hivyo wakawa miongoni mwa watu wema. Na Mwenyezi Mungu Subhanahu huwalipa wema kwa maisha mazuri katika uhai huu wa duniani. Na pahala pao Akhera ni bora na pazuri zaidi kuliko waliyo yapata duniani. Na nyumba watayo ikaa wachamngu Akhera ni hadi ya raha yake!
Bustani za milele wataziingia; iwe inapita kati yake mito. Humo watapata watakacho. Hivi ndivyo Mwenyezi Mungu awalipavyo wenye kumcha.
Nazo ni Bustani madhubuti za kudumu, zenye kupitiwa na mito chini ya majumba na miti yake. Na hao watapata kila neema waipendayo. Na mfano kama huu ndio malipo ya mema anayo walipa Mwenyezi Mungu wachamngu wote wanao muamini, na wakajikinga na yanayo mkasirisha, na wakavifanya vyema vitendo vyao.
Wale ambao Malaika huwafisha katika hali njema, wanawaambia:Amani iwe juu yenu! Ingieni Peponi kwa sababu ya yale mliyo kuwa mkiyatenda.
Na ndio hao Malaika huzichukua roho zao na hali wamesafika na uchafu wa ushirikina na maasi. Na Malaika watawaambia kwa kuwatuza: Amani kwenu itokayo kwa Mwenyezi Mungu! Baada ya hii leo hamtopata la karaha. Na ifurahieni Pepo mtakayo ingia kwa sababu ya vitendo vyema mlivyo vitanguliza katika dunia yenu.
Wanangojea jengine hawa ila Malaika wawafikie, au iwafikie amri ya Mola wako Mlezi? Kama hivyo walitenda walio kuwa kabla yao. Na MwenyeziMungu hakuwadhulumu, lakini walijidhulumu wenyewe.
Hao ndio wachamngu walio jitengenezea Akhera yao. Na hayo ndiyo malipo yao. Ama washirikina kwa sababu ya inadi yao na kubakia kwao kwenye ushirikina wao, hawataraji ila Malaika waje kunyakua roho zao nao wamezidhulumu nafsi zao kwa ushirikina na vitendo vya shari. Na itawajia adhabu ya Mola wako Mlezi iwateketeze wote. Na kama walivyo fanya makafiri hawa, basi walikwisha wafanyia Manabii wao wale walio watangulia, na Mwenyezi Mungu akawaadhibu kwa vitendo vyao. Wala Yeye hakuwadhulumu pale alipo waadhibu, lakini wao wenyewe walizidhulumu nafsi zao walipo zitia katika adhabu kwa ukafiri wao.
Contents of the translations can be downloaded and re-published, with the following terms and conditions:
1. No modification, addition, or deletion of the content.
2. Clearly referring to the publisher and the source (QuranEnc.com).
3. Mentioning the version number when re-publishing the translation.
4. Keeping the transcript information inside the document.
5. Notifying the source (QuranEnc.com) of any note on the translation.
6. Updating the translation according to the latest version issued from the source (QuranEnc.com).
7. Inappropriate advertisements must not be included when displaying translations of the meanings of the Noble Quran.
தேடல் முடிவுகள்:
API specs
Endpoints:
Sura translation
GET / https://quranenc.com/api/v1/translation/sura/{translation_key}/{sura_number} description: get the specified translation (by its translation_key) for the speicified sura (by its number)
Parameters: translation_key: (the key of the currently selected translation) sura_number: [1-114] (Sura number in the mosshaf which should be between 1 and 114)
Returns:
json object containing array of objects, each object contains the "sura", "aya", "translation" and "footnotes".
GET / https://quranenc.com/api/v1/translation/aya/{translation_key}/{sura_number}/{aya_number} description: get the specified translation (by its translation_key) for the speicified aya (by its number sura_number and aya_number)
Parameters: translation_key: (the key of the currently selected translation) sura_number: [1-114] (Sura number in the mosshaf which should be between 1 and 114) aya_number: [1-...] (Aya number in the sura)
Returns:
json object containing the "sura", "aya", "translation" and "footnotes".